Connect with us

News

Wakaazi Kilifi washinikiza serikali kukusanya maoni kabla miradi kuanza.

Published

on

Serikali kuu imeandaa kikao cha kukusanya maoni ya umma pamoja na wadau mbali mbali kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na serikali ya kitaifa kaunti ya Kilifi katika chuo kikuu cha pwani.

Akizungumza katika kikao hicho katibu mkuu wa maswala ya uratibu katika ofisi ya mkuu wa mawaziri Ahmed Abdisalam, alisema kikao hicho kinatoa fursa kwa wananchi kufahamu namna serikali inavyotekeleza miradi yake kuanzia mwanzo hadi mwisho.

Abdisalam aliongeza kuwa wananchi wanamchango mkubwa katika kutambua changamoto zozote zinazojitokeza kwenye mchakato wa utekelezaji wa miradi hiyo, akidokeza kuwa kaunti ya kilifi ni miongoni mwa kaunti zinazofaidi miradi mingi ya serikali.

“Tunataka kuhakikisha tunatembea na wananchi kutoka hatua ya kutambua miradi, utekelezaji na pia inapokamilika, malengo ni kusistiza uhusika wa wananchi ili kuwa na uendelevu wakati wa kutekeleza miradi ya serikali kuu”, alisema Abdisalam.

Kwa upande wake kamishna wa kaunti ya Kilifi Josephat Biwot alidokeza kuwa serikali kwa sasa inaendeleza miradi mbali ikiwepo ujenzi wa nyumba za bei nafuu eneo la Tezo na Mtwapa pamoja na ujenzi wa soko eneo la Watamu.

Biwot vile vile alisema serikali inajenga vyumba vya malazi ya zaidi ya wanafunzi 1,700 katika chuo kikuu cha pwani pamoja na ujenzi wa barabara ya Bamba kuelekea Ganze huku ile ya Mwakirunge ikitarajiwa kuanza karibuni.

“Tuko na miradi mipya iliyoanzishwa na serikali iliyomamlakani kama ujenzi ya nyumba za bei nafuu, tuko na miradi wa Tezo na Mtwapa ambayo inaendelea na pia tuko na ujenzi wa masoko unaendelea, watamu liko zaidi ya asilimia 70 kukamilika”, alisema kamishna Biwot.

Kwa upande wao baadhi ya wanachi waliohudhuria kikao hicho waliikata serikali kuhakikisha inahusisha wananchi kabla miradi kuanza kutekelezwa, wakidai serikali imekuwa ikitafuta maoni ya umma wakati miradi ikiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Joho, awahimiza wakenya kujisajili katika “Boma Yangu”

Published

on

By

Waziri wa Madini na Uchumi wa raslimali za bahari Ali Hassan Joho, aliwahimiza wakenya kujisajili katika mpango wa “Boma Yangu” ili kunufaika na nyumba za bei nafuu zinazojengwa katika maeneo mbalimbali nchini.

Waziri Joho alipongeza mradi huo wa serikali, akisema unalenga kuwaondoa wakenya kutoka kwenye makaazi duni na kuwapatia makaazi bora yenye hadhi na mazingira salama ya kuishi.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa baada ya swala ya Eid-ul-Adha, Joho aliwahimiza wakaazi wa eneo la Pwani kuchukua hatua za haraka kujisajili ili wasikose fursa hiyo muhimu ya kuboresha maisha yao.

“Kuna huu mradi unaitwa Affordable Housing, huu mradi mmeona umefanywa mahali kwingi sana na sai usajili wa ule mradi ambao utafanyika pale VOK eneo bunge la Nyali, nyumba 1,976 zitajengwa na mambo mengine, nawasihi kwa heshima kubwa sana waingie kwa Boma Yangu wajisajili”, alisema Joho.

Kwa upande wake Kamishna wa kaunti ya Mombasa Mohamed Nur aliwahimiza vijana kujitokeza kwa wingi kutuma maombi ya nafasi za ajira katika mpango wa kazi mtaani kwa vijana.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

News

KHRC: Wasichana elfu moja ni wajawazito, Lamu

Published

on

By

Takribani wasichana elfu moja kaunti ya Lamu wameripotiwa kupata mimba za utotoni kati ya mwaka wa 2024/25 huku visa vingi vikichangiwa na dhulma za kingono na ndoa za mapema.

Kulingana na Masharika ya kutetea haki za kibinadamu la MUHURI pamoja na lile la Kenya Human Rights Commission, KHRC serikali imeshindwa kuwakabili kisheria wahusika huku waathiriwa ambao ni wasichana wadogo wakiendelea kuhangaika.

Takwimu kutoka kwa kamati ya jinsia kaunti ya Lamu, iliwasilisha kwa kamati ya kitaifa inayoangazia masuala ya dhulma za jinsia kuwa kaunti hiyo ilinakili visa zaidi ya 700 vya mimba za utotoni mwaka wa 2024.

Takwimu hioz pia ziliweka wazi kwamba visa vingine zaidi ya 200 viliripotiwa kati ya mwezi Januari na Mei mwaka huu wa 2025.

Kulingana na ripoti kutoka kwa baraza la kitaifa la kudhibiti magonjwa NSDCC ilieonysha kwamba wasichana wanarika zaidi ya 600 nchini walipata mimba mwaka 2023.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending