Connect with us

News

Wahudumu wa Sekta ya Uchukuzi Wanahimiza Ukarabati wa Barabara ya Kibaoni-Ganze-Bamba

Published

on

Wahudumu wa sekta ya uchukuzi mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanashinikiza serikali kuu na ile ya kaunti kuzingatia ukarabati wa barabara ya Kibaoni-Ganze hadi Bamba licha ya kushinikizwa kusitisha maandamano ya kufunga barabara hiyo.

Wakizungumza na Coco FM, wahudumu hao wamesema barabara hiyo ingali na hitilafu nyingi na wanahofia huenda ikaharibika vibaya msumu huu wa mvua.

Wakiongozwa na Praise Majimbo ambaye ni mhudumu wa bodaboda, wamesema hatua ya kulima barabara hiyo kwa tinga tinga haitoshi kwani bado kuna vumbi na mashimo hali inayowatatiza shughuli zao za kibiashara. 

Kwa sasa kidogo iko na afadhali lakini bado hatujaridhika na kile chenye tunapitia, kwa sababu kwengine kushatengenezwa na mvua imenyesha tayari sasa hivi mashimo yako mengi, vyenye niko tayari nyewe nimechoka kutoka Kakanjuni mpaka barabara vyenye iko kwa ukweli, vumbi na mashimo pia yashaongezeka kwa sababu ya mvua”, alisema Majimbo. 

Nao wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma wakilongozwa na Samson Kitsao Wako, wanasema wanapitia changamoto za kukarabati magari yao kila mara kutokana na hali mbaya ya barabara hiyo.

“Lakini kwa saa tutasema inaafadhali kwa sababu, tuliandamana na tukafunga na baadaye serikali ikaleta tinga tinga ikapiga msasa kutoka hapa Kibaoni mpaka Silala, lakini sasa kutoka Ganze mpaka Bamba ndio barabara ni mbaya sana, mvua ikianza kunyesha tutapata shida sana kwa sababu barabara wakati wa mvua hua inateleza”, alisema Kitsao. 

Vile vile wachuuzi wa vyakula kando ya barabara hiyo Wakiongozwa na Fiki Kenga wanasema idadi ya wateja imekuwa ikipungua kutokana na vumbi linalotoka barabarani kila mara, wakisinikiza serikali kuzingatia kilio chao.

“Tunapata taharuki hata vyakula vyetu huwa haviendi vizuri kila siku, hii barabara ilifanya kukwaruzwa kwaruzwa huko, angalau tusiumizwe na hili vumbi, barabara iko na vumbi wateja wanalalamika kwa sababu vumbi si nzuri kwa chakula, kwa hivyo tunaomba msaada tuwe nasi tutakaa vizuri mahali tuko”, waliongeza baadhi ya wachuuzi.

Aidha wameshinikiza serikali kuangazia matatizo wanayopitia baadhi yao wakidai wanawake wajawazito wamekuwa wakipoteza watoto wachanga hasa wanaposafirishwa kwa pikipiki kuelekea hospitali kujifungua kutokana na ubovu wa barabara hiyo. 

Itakumbukwa kwamba wakaazi pamoja na wahudumu wa uchukuzi wa umma waliandamana na kufunga barabara hiyo kwa majuma kadhaa na kutatiza shughuli za usafiri.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kindiki, ataka makubaliano kati ya serikali kuu na kaunti kutekelezwa

Published

on

By

Naibu wa rais Prof. Kithure Kindiki ametaka makubaliano yote kati ya serikali za kaunti na ile ya kitaifa kutekelezwa kabla ya mwezi Disemba mwaka huu wa 2025.

Akizungumza katika makao yake ya Karen jijini Nairobi Jumatatu 23, Juni 2025, kwenye mkutano wa 27 kati ya serikali kuu na zile za kaunti kuhusu bajeti IBEC, Kindiki alisema kumekuwa na makubaliano ambayo yamekuwa hayafuatiliwi ili kutekelezwa.

Kindiki alisema serikali kuu imejitolea kuhakikisha serikali za kaunti zinafanikisha miradi mbalimbali na kuwataka maafisa wa serikali za kaunti na ile ya kitaifa kushirikiana kwa majadiliano.

Wakati huo huo alisisitiza haja ya kutafuta suluhu la matatizo yanayoathiri utendakazi wa serikali za kaunti huku akipuzilia mbali uwepo wa mzozo wowote baina ya serikali kuu na zile za kaunti.

Taarifa ya Janet Mumbi.

Continue Reading

News

Spika Teddy, adai wabunge wa kitaifa wanachangia kutimuliwa kwake ofisini

Published

on

By

Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi Teddy Mwambire ameibua madai kwamba baadhi ya wabunge wa kitaifa kutoka kaunti ya Kilifi ndio ambao wanaendeleza njama ya kumuondoa kama spika wa bunge hilo.

Kupitia video ambayo imekuwa ikisambaa kwenye mitandao ya kijamii, Spika Mwambire alisema viongozi hao wameshirikiana na baadhi ya Wawakilishi wa wadi wa bunge la kaunti ya Kilifi ili kuhakikisha wanafanikiwa kumbandua mamlakani.

Mwambire alisema viongozi pamoja na gavana wa kaunti ya Kilifi Gedion Maitha Mung’aro wako na njama fiche ili kuhakikisha wanatimiza malengo yao ilhali hakuna sababu zozote za kimsingi.

Aidha, Mwambire alisema hadi kufikia sasa hajajua sababu kuu ambazo zinasababisha kutaka kumbandua kama Spika wa bunge la kaunti ya Kilifi.

Vilevile, alisema hatajiuzulu kama spika wa bunge la kaunti ya Kilifi na kuwakosoa wanaomtaka kuomba msamaha bila kumfahamisha makosa yake.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending