Connect with us

News

Wahudumu wa Sekta ya Uchukuzi Wanahimiza Ukarabati wa Barabara ya Kibaoni-Ganze-Bamba

Published

on

Wahudumu wa sekta ya uchukuzi mjini Kilifi kaunti ya Kilifi wanashinikiza serikali kuu na ile ya kaunti kuzingatia ukarabati wa barabara ya Kibaoni-Ganze hadi Bamba licha ya kushinikizwa kusitisha maandamano ya kufunga barabara hiyo.

Wakizungumza na Coco FM, wahudumu hao wamesema barabara hiyo ingali na hitilafu nyingi na wanahofia huenda ikaharibika vibaya msumu huu wa mvua.

Wakiongozwa na Praise Majimbo ambaye ni mhudumu wa bodaboda, wamesema hatua ya kulima barabara hiyo kwa tinga tinga haitoshi kwani bado kuna vumbi na mashimo hali inayowatatiza shughuli zao za kibiashara. 

Kwa sasa kidogo iko na afadhali lakini bado hatujaridhika na kile chenye tunapitia, kwa sababu kwengine kushatengenezwa na mvua imenyesha tayari sasa hivi mashimo yako mengi, vyenye niko tayari nyewe nimechoka kutoka Kakanjuni mpaka barabara vyenye iko kwa ukweli, vumbi na mashimo pia yashaongezeka kwa sababu ya mvua”, alisema Majimbo. 

Nao wahudumu wa magari ya uchukuzi wa umma wakilongozwa na Samson Kitsao Wako, wanasema wanapitia changamoto za kukarabati magari yao kila mara kutokana na hali mbaya ya barabara hiyo.

“Lakini kwa saa tutasema inaafadhali kwa sababu, tuliandamana na tukafunga na baadaye serikali ikaleta tinga tinga ikapiga msasa kutoka hapa Kibaoni mpaka Silala, lakini sasa kutoka Ganze mpaka Bamba ndio barabara ni mbaya sana, mvua ikianza kunyesha tutapata shida sana kwa sababu barabara wakati wa mvua hua inateleza”, alisema Kitsao. 

Vile vile wachuuzi wa vyakula kando ya barabara hiyo Wakiongozwa na Fiki Kenga wanasema idadi ya wateja imekuwa ikipungua kutokana na vumbi linalotoka barabarani kila mara, wakisinikiza serikali kuzingatia kilio chao.

“Tunapata taharuki hata vyakula vyetu huwa haviendi vizuri kila siku, hii barabara ilifanya kukwaruzwa kwaruzwa huko, angalau tusiumizwe na hili vumbi, barabara iko na vumbi wateja wanalalamika kwa sababu vumbi si nzuri kwa chakula, kwa hivyo tunaomba msaada tuwe nasi tutakaa vizuri mahali tuko”, waliongeza baadhi ya wachuuzi.

Aidha wameshinikiza serikali kuangazia matatizo wanayopitia baadhi yao wakidai wanawake wajawazito wamekuwa wakipoteza watoto wachanga hasa wanaposafirishwa kwa pikipiki kuelekea hospitali kujifungua kutokana na ubovu wa barabara hiyo. 

Itakumbukwa kwamba wakaazi pamoja na wahudumu wa uchukuzi wa umma waliandamana na kufunga barabara hiyo kwa majuma kadhaa na kutatiza shughuli za usafiri.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Alubbe: Tutazuru kaunti za Pwani kushughulikia suala tata la ardhi

Published

on

By

Mkurugenzi mkuu wa shirika la utetezi wa haki za ardhi nchini Kenya Land Alliance Faith Alubbe amesema wameanzisha mchakato wa kuzuru kaunti zote 6 za pwani kuangazia suala tata la mizozo ya ardhi.

Akizungumza mjini Kilifi, Alubbe alisema kwamba ukanda wa Pwani ni mojawapo ya maeneo humu nchini ambayo yamesheheni dhulma za kihistoria kwenye masuala ya umiliki wa ardhi.

Alubbe ambaye pia ni Wakili wa masuala ya ardhi alihoji kwamba mikakati yao katika mchakato huu ni kuhakikisha kuwa wapwani wanaelewa kwa kina haki zao kuhusiana na umiliki wa ardhi za kibinafsi lakini pia za kijamii.

“Kuna hazina ya ardhi ambayo ilibuniwa baada ya mswada kuhusiana na hazina hiyo kupitishwa. Rais William Ruto tayari aliwekeza fedha kwenye hazina hiyo ila idadi kubwa ya wakaazi wa pwani hawana ufahamu kuhusu hazina hiyo” alisema Alubbe.

Alubbe alisema kuwa watahakikisha kuwa wapwani wanapata hamasa za kutosha kuhusiana na suala hilo lakini pia haki zao za ardhi kwa jumla.

“Inaweza kuwa muhimu watu wa pwani kuambiwa kuhusu hii hazina, ili wakapate kuelewa ni vipi hazina hizi zinawahusu”, aliongeza Alubbe.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

News

Chahale, aishutumu serikali kutokana na dhulma za kijinsia

Published

on

By

Mkurugenzi mkuu wa Shirika la kutetezi haki za kibinadamu la International Justice Mission, IJM, Vincent Chahale ameishutumu serikali kwa kuzembea katika kukabiliana na dhulma dhidi ya wasichana na wanawake nchini.

Chahale alisema kwamba wasichana wadogo wamekuwa wakidhulumiwa kingono na wengi wao huishia kukosa haki.

Alirejelea kisa ambapo msichana wa umri wa miaka 17 kwa jina Farida Julius Changawa aliyeuawa kinyama kwa kudungwa kesu eneo la Msumarini kaunti ya Kilifi ambali alisema ni sharti serikali iwe ange katika kuhakikisha kwamba wasichana wanalindwa dhidi ya dhulma katika jamii.

“Kuna pengo katika jamii yetu ambapo wasichana wadogo wanaendelea kudhulumiwa bila kupata haki. Kesi kama ya Farida ni kesi ya kusikitisha sana na tutaifuatilia hadi pale familia yake itakapopata haki” alisema Chahale.

Akiunga mkono kauli hiyo, Aggrey Juma meneja msimamizi wa Shirika la international Justice Mission alisema serikali inapaswa kutilia mkazo suala la dhulma dhidi ya Wanawake akieleza kusikitishwa na mauaji ya kinyama aliyotekelezewa marehemu Farida Julius.

Wawili hawa waliyasema haya wakati wa mazishi ya mwendazake Farida yaliyofanyika eneo la Mavueni siku Jumamosi ya tarehe ya 21 mwezi Juni 2025.

Farida alipitia dhulma ya kubakwa akiwa na umri wa miaka 13 kudhulimiwa tena miaka minne baadaye ambapo aliishia kuuawa kwa kudungwa kisu hivi majuzi.

Marehemu aliacha mtoto mmoja wa kiume mwenye umri wa miezi 9.

Taarifa ya Hamis Kombe

Continue Reading

Trending