News
Wahudumu wa boda boda Mariakani-Kilifi walalamikia utovu wa usalama.

Wahudumu wa boda boda huko Mariakani eneo bunge la Kaloleni kaunti ya Kilifi wanatilia shaka ongezeko la watu wanaojifanya wanabodaboda ilihali watekeleza visa vya uhalifu eneo hilo.
Mwenyekiti wa wahudumu hao Gitome Mwasia alisema kwa sasa wameanza mchakato wa kuwasajili wahudumu wote wa bodaboda katika kila kituo eneo hilo.
Mwasia aliongeza kuwa hatua hiyo itarahisisha wao kuwatambua wahudumu halali wa eneo hilo.
Wakati huo huo mwenyekiti huyo alisisitiza haja ya kila mwanabodaboda eneo hilo kujisajili akisema hatua hiyo itawasaidia kutambua wahalifu wanaotumia kigezo cha wanabodaboda kutekeleza visa vya ujambazi.
Vile vile aliwashauri wahudumu hao kuwa makini wanapobeba abiria huku akiwashinikiza wakazi wa eneo hilo kutowaficha wahalifu bali watoe habari muhimu kwa vitengo husika.
Taarifa ya mwanahabari wetu.
News
Washukiwa wa wizi eneo la Mtwapa-Kilifi kufahamu hatma yao.

Washukiwa 7, waliokamatwa katika eneo la Mtwapa kaunti Kilifi, kwa tuhuma za wizi kwenye magari watafahamu hatma yao sikuya Ijumaa 13 mwezi huu iwapo wataachiliwa kwa dhaman au la.
Washukiwa hao Edwin Kyalo Mulandi, Nicholus Mungaro Kitumbo, maarufu Papa, Erick Kabue Maranga maarufu Wachira, Ali Said Nassir, Fred Mungoma Mwanjira, Fredrick Kalungo Konde na Akasha Hassan Akasha walifikishwa katika mahakam ya Shanzu kaunti ya Mombasa ambako walikanusha mashtaka dhidi yao.
Aidha, upande wa mashtaka uliwasilisha ombi la kutaka saba hao kunyimwa dhama ikizingatiwa ni miongoni mwa wahalifu sugu ambao wamekuwa wakitafutwa na asasi za usalama, baadhi yao wakiwa na rekodi za kesi mahakamani.
Saba hao walikamatwa baada ya kuhusishwa na visa vya wizi viliyoripotiwa katika vituo mbalimbali vya polisi ikiwemo Mtwapa kaunti ya Kilifi, Changamwe, Nyali, Tononoka, Makupa na Central, kaunti ya Mombasa, kituo cha Embakasi jijini Nairobi na Dar es Salaam nchini Tanzania.
Wakati wa kukamatwa 7 hao, polisi pia walifanikiwa kunasa magari 8 na bidhaa mbalimbali zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 7.
Taarifa ya Mwanahabari wetu.
News
Jaji mkuu mstaafu David Maraga akosoa utawala wa Rais William Ruto.

Jaji Mkuu mstaafu David Maraga ametoa wito wa kusitishwa mara moja kwa utawala wa rais William Ruto kufuatia kifo cha mwanablogu Albert Omondi Ojwang anayedaiwa kufariki akiwa mikononi mwa maafisa wa polisi.
Katika taarifa yenye maneno makali iliyotolewa Maraga, alinukuu ripoti ya upasuaji wa maiti ya mwanapatholojia wa serikali, ambayo anasema inathibitisha kuwa Ojwang alitendewa ukatili, kunyongwa, kuteswa na kuuawa na maafisa wa polisi.
Maraga ambaye anawania wadhfa wa urais kwenye uchaguzi mkuu ujao mwaka 2027, alikumbusha maandamano ya vijana wa kizazi cha Gen Z, ambapo zaidi ya vijana 100 walipoteza maisha kutokana na ukatili wa maafisa wa polisi.
Vile vile alilaani utawala wa rais Ruto kwa kuunga mkono mauaji ya kiholela, akitaja kifo cha Ojwang’ kama tukio la mwisho.
Maragapia alishtumu serikali kwa kufumbia macho madai ya ugaidi unaofadhiliwa na serikali.
Wakati huo huo Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga aliagiza hatua za haraka kuchukuliwa dhidi ya maafisa wa polisi waliohusika na mauaji ya kijana huyo huku akisistiza uwajibikaji.
Taarifa ya Joseph Jira