Connect with us

Business

Wafanyabiashara waomba kufunguliwa kwa soko la Matano Mane, Kaunti ya Kilifi

Published

on

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo bunge la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameiomba serikali ya kaunti kufungua soko la eneo hilo lililojengwa miaka 15 iliyopita lakini hadi sasa halijaanza kutumika.

Wakizungumza na Coco FM, wafanyabiashara hao wamesema kuwa wanakumbwa na changamoto nyingi, hasa wakati huu wa mvua, ambapo bidhaa zao zinaharibiwa kwa kunyeshewa kutokana na ukosefu wa sehemu ya kudumu ya kufanyia biashara.

Josphat Karisa, mmoja wa wafanyabiashara katika soko hilo, amesema kuwa wanalazimika kufanya biashara katika mazingira magumu licha ya kuwepo kwa soko lililojengwa lakini halijafunguliwa rasmi kwa matumizi.

“Tunapitia hasara kubwa wakati huu wa mvua. Bidhaa zetu zinaharibika kwa sababu hatuna mahali pa kudumu pa kufanyia biashara, ilhali kuna soko limejengwa miaka 15 iliyopita lakini halitumiki,” amesema Karisa.

Ameitaka serikali ya Kaunti ya Kilifi kuchukua hatua za haraka kuhakikisha soko hilo linafunguliwa ili wafanyabiashara waweze kuendeleza shughuli zao bila usumbufu na kujikimu kimaisha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Published

on

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.

Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.

Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.

Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.

Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .

Continue Reading

Business

Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Published

on

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.

Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.

Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.

Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.

Continue Reading

Trending