Connect with us

Business

Wafanyabiashara waomba kufunguliwa kwa soko la Matano Mane, Kaunti ya Kilifi

Published

on

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo bunge la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameiomba serikali ya kaunti kufungua soko la eneo hilo lililojengwa miaka 15 iliyopita lakini hadi sasa halijaanza kutumika.

Wakizungumza na Coco FM, wafanyabiashara hao wamesema kuwa wanakumbwa na changamoto nyingi, hasa wakati huu wa mvua, ambapo bidhaa zao zinaharibiwa kwa kunyeshewa kutokana na ukosefu wa sehemu ya kudumu ya kufanyia biashara.

Josphat Karisa, mmoja wa wafanyabiashara katika soko hilo, amesema kuwa wanalazimika kufanya biashara katika mazingira magumu licha ya kuwepo kwa soko lililojengwa lakini halijafunguliwa rasmi kwa matumizi.

“Tunapitia hasara kubwa wakati huu wa mvua. Bidhaa zetu zinaharibika kwa sababu hatuna mahali pa kudumu pa kufanyia biashara, ilhali kuna soko limejengwa miaka 15 iliyopita lakini halitumiki,” amesema Karisa.

Ameitaka serikali ya Kaunti ya Kilifi kuchukua hatua za haraka kuhakikisha soko hilo linafunguliwa ili wafanyabiashara waweze kuendeleza shughuli zao bila usumbufu na kujikimu kimaisha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Vijana Kaunti ya Tana River Waanzisha Biashara ya Sambusa za Samaki kuinua Uchumi

Published

on

Vijana katika Kaunti ya Tana River wameanzisha biashara ya upishi wa sambusa za samaki kwa lengo la kujikwamua kiuchumi kwa kutumia rasilimali za baharini.

Wamebuni mbinu ya kipekee ya kuandaa sambusa kwa kutumia samaki wa aina mbalimbali, wakiwemo samaki papa. Mbali na sambusa, vijana hao pia wameweza kuunda bidhaa nyingine za thamani kutokana na samaki, hatua inayochochea ubunifu na kuongeza ajira miongoni mwao.

Kulingana na vijana hao, biashara hiyo inalenga kuongeza kipato chao na kufungua milango ya kuingia katika masoko mapya, ya ndani na hata ya nje ya kaunti.

Hatua hii imesukumwa na changamoto ya uhaba wa soko la samaki katika eneo hilo, hali ambayo husababisha uharibifu wa samaki kutokana na kukosa wanunuzi. Kwa hivyo, ubunifu huu umekuwa suluhisho la kiuchumi na kiteknolojia kwa vijana wa Tana River.

Continue Reading

Business

Wafanyabiashara wa Soko la Matano Mane Waililia Serikali ya Kaunti ya Kilifi Kuwajengea Choo

Published

on

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuwajengea choo, wakisema ukosefu wa huduma hiyo muhimu umekuwa kero kubwa inayozorotesha shughuli za biashara.

Wakiongozwa na Phelisia Mageshi, wafanyabiashara hao wamesema kuwa hali ya sasa imesababisha baadhi yao kuhamishia biashara zao nje ya soko hilo, kutokana na mazingira yasiyofaa kwa shughuli za kila siku.

Bi Mageshi ameeleza kuwa licha ya serikali ya kaunti kufahamishwa kuhusu changamoto hiyo mara kadhaa, hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa hadi sasa, hali inayowafanya kuhisi kusahaulika.

Wameitaka serikali ya kaunti kuingilia kati kwa haraka ili kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na kuhakikisha afya ya wananchi inalindwa.

Continue Reading

Trending