Business
Wafanyabiashara Wakosoa KRA Kuhusu Ushuru wa Juu na Huduma Duni

Baadhi ya wafanyibiashara mjini Malindi kaunti ya Kilifi wanalalamikia kupanda kwa gharama ya maisha sawa na ushuru wa biashara wakati mamlaka ya ukusanyaji ushuru nchini, KRA ikitangaza ongezeko la ukusanyaji wa ushuru kwa asilimia 6.8 katika mwaka wa kifedha 2024/2025.
Wakiongozwa na Kenza Ondiek wafanyibiashara hao wanasema kuwa ongezeko la ushuru nchini limeathiri pakubwa ustawi wa biashara huku uboreshaji wa miundomsingi ukiwa katika viwango vya chini.
Ondiek ameiomba serikali kuhakikisha kuwa inaboresha maisha ya wananchi kupitia mapato ya ushuru hasa baada ya mamlaka ya KRA kukusanya jumla ya shilingi trilioni 2.61 katika mwaka wa kifedha 2024/2025 ikilinganishwa na trilioni 2.40 za mwaka kifedha 2023/2024.
Ondiek aidha ameiomba serikali kuwajibikia kikamilifu matumizi bora ya fedha za ushuru zinazokusanywa nchini ili kubadilisha maisha ya wananchi badala ya kuangazia njia za kuongeza kiwango cha makato ya ushuru pekee kwa wananchi.
Haya yanajiri huku mamlaka ya KRA pia ikifichua kupitisha makadirio yake ya ukusanyaji wa ushuru kutoka kwa shilingi trilioni 2.56 hadi shilingi trilioni 2.61 kwa mwaka wa kifedha 2024/2025.
Business
Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.
Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.
Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.
Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.
Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .
Business
Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.
Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.
Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.
Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.