Business
Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa Walalamikia Ukosefu wa Maji Kwenye Soko Hilo

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa kaunti ya Kilifi wamelalamikia ukosefu wa maji kwenye Soko hilo ambapo wafanyibiashara wengi wanalitegemea kuendeleza shughuli zao za kila siku.
Kulingana na mwenyekiti wa Soko hilo Millicent Mbodze ukosefu wa maji katika soko hilo limeathiri biashara zao kwani maji yanatumiwa kuonsha bishaa nyingi kama vile matunda, mboga na hata samaki kwa wanaouza samaki katika soko hilo.
Aidha amesema wateja wengi wanalalamikia hali mbaya ya ya soko hilo kwani kumejaa uchafu kila mahali hali inayowasababishia kuhofia afya yao.
Amesema tayari wateja wengi wanasusia maeneo hayo jambo ambalo liewasababishishia hasara kubwa kwani bidhaa nyingi huozea sokoni.
Wakati huo huo Mbodze amesema licha ya kuwasilisha swala hilo kwa kwa wahusika sawa na serikali ya kaunti ya Kilifi,bado halijatatuliwa.
Anasema imekuwa changamoto kwa wafanyabiashara kwani imekuwa shida kutumia hata sehemu za kujisaidia sokoni humo huku ikiwalazimu kutafuta bidhaa hiyo kwenye kituo kimoja cha mafuta kilichoko eneo hilo.
Huku hayo yakijiri benki ya dunia imetenga shilingi bilioni 2.58 kuimarisha mpango wa usabasazaji maji katika kaunti ya kilifi.
Mradi huo unalenga miji ya malindi , kilifi na mtwapa na utahusisha kubadilishwa kwa mabomba makuku ya maji na kuweka mabomba mapya.
Ikumbukwe Gavana wa kilifi Gedion Mung’aro alisema miradi hiyo itahakikisha kuwa kaunti hiyo iko na maji safi na yakutosha.
Business
Vijana Kaunti ya Tana River Waanzisha Biashara ya Sambusa za Samaki kuinua Uchumi

Vijana katika Kaunti ya Tana River wameanzisha biashara ya upishi wa sambusa za samaki kwa lengo la kujikwamua kiuchumi kwa kutumia rasilimali za baharini.
Wamebuni mbinu ya kipekee ya kuandaa sambusa kwa kutumia samaki wa aina mbalimbali, wakiwemo samaki papa. Mbali na sambusa, vijana hao pia wameweza kuunda bidhaa nyingine za thamani kutokana na samaki, hatua inayochochea ubunifu na kuongeza ajira miongoni mwao.
Kulingana na vijana hao, biashara hiyo inalenga kuongeza kipato chao na kufungua milango ya kuingia katika masoko mapya, ya ndani na hata ya nje ya kaunti.
Hatua hii imesukumwa na changamoto ya uhaba wa soko la samaki katika eneo hilo, hali ambayo husababisha uharibifu wa samaki kutokana na kukosa wanunuzi. Kwa hivyo, ubunifu huu umekuwa suluhisho la kiuchumi na kiteknolojia kwa vijana wa Tana River.
Business
Wafanyabiashara wa Soko la Matano Mane Waililia Serikali ya Kaunti ya Kilifi Kuwajengea Choo

Wafanyabiashara katika soko la Matano Mane, eneo la Vitengeni, Kaunti ya Kilifi, wameitaka serikali ya kaunti hiyo kuwajengea choo, wakisema ukosefu wa huduma hiyo muhimu umekuwa kero kubwa inayozorotesha shughuli za biashara.
Wakiongozwa na Phelisia Mageshi, wafanyabiashara hao wamesema kuwa hali ya sasa imesababisha baadhi yao kuhamishia biashara zao nje ya soko hilo, kutokana na mazingira yasiyofaa kwa shughuli za kila siku.
Bi Mageshi ameeleza kuwa licha ya serikali ya kaunti kufahamishwa kuhusu changamoto hiyo mara kadhaa, hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa hadi sasa, hali inayowafanya kuhisi kusahaulika.
Wameitaka serikali ya kaunti kuingilia kati kwa haraka ili kuboresha mazingira ya kufanyia biashara na kuhakikisha afya ya wananchi inalindwa.