Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa Walalamikia Ukosefu wa Maji Kwenye Soko Hilo

Published

on

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa kaunti ya Kilifi wamelalamikia ukosefu wa maji kwenye Soko hilo ambapo wafanyibiashara wengi wanalitegemea kuendeleza shughuli zao za kila siku.

Kulingana na mwenyekiti wa Soko hilo Millicent Mbodze ukosefu wa maji katika soko hilo limeathiri biashara zao kwani maji yanatumiwa kuonsha bishaa nyingi kama vile matunda, mboga na hata samaki kwa wanaouza samaki katika soko hilo.

Aidha amesema wateja wengi wanalalamikia hali mbaya ya ya soko hilo kwani kumejaa uchafu kila mahali hali inayowasababishia kuhofia afya yao.

Amesema tayari wateja wengi wanasusia maeneo hayo jambo ambalo liewasababishishia hasara kubwa kwani bidhaa nyingi huozea sokoni.

Wakati huo huo Mbodze amesema licha ya kuwasilisha swala hilo kwa kwa wahusika sawa na serikali ya kaunti ya Kilifi,bado halijatatuliwa.

Anasema imekuwa changamoto kwa wafanyabiashara kwani imekuwa shida kutumia hata sehemu za kujisaidia sokoni humo huku ikiwalazimu kutafuta bidhaa hiyo kwenye kituo kimoja cha mafuta kilichoko eneo hilo.

Huku hayo yakijiri benki ya dunia imetenga shilingi bilioni 2.58 kuimarisha mpango wa usabasazaji maji katika kaunti ya kilifi.

Mradi huo unalenga miji ya malindi , kilifi na mtwapa na utahusisha kubadilishwa kwa mabomba makuku ya maji na kuweka mabomba mapya.

Ikumbukwe Gavana wa kilifi Gedion Mung’aro alisema miradi hiyo itahakikisha kuwa kaunti hiyo iko na maji safi na yakutosha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Kaunti ya Kilifi yaendeleza mikakati ya kuimarisha sekta ya uvuvi

Published

on

By

Mkurugenzi wa masuala ya uvuvi kaunti ya Kilifi Mwangi Gachuru amesema serikali ya kaunti ya Kilifi inaendeleza mikakati katika kuimarisha sekta ya uvuvi kwenye kaunti hii ya Kilifi.

Gachuru alisema wanashirikiana na wasimamizi wa fuo za bahari katika kaunti ya Kilifi katika kuhakikisha wavuvi wananufaika kupitia raslimali za baharini.

Aidha, Gachuru aliwahimiza wavuvi na wenyeji wa kaunti ya Kilifi kushirikiana ipasavyo kuhakikisha raslimali hizo zinawafaidi ipasavyo.

“Ni kupitia ushirikiano pekee ndipo mtaweza kuendeleza uvuvi wenu vizuri’’, alisema Gachuru

Akizungumzia mzozo baina ya wavuvi, Gachuru aliwataka kuzingatia sheria zilizopo kwa mujibu wa sheria za uvuvi ili kupatikane mwafaka na sio kuchukua sheria mkononi na kuahidi kuwa watawakabili kisheria wale ambao wanatumia nyavu ambazo zilipigwa marufuku kutumika baharini kuvua samaki.

“Panapotokea ugomvi miongoni mwenu, zingatieni sheria na sio kuchukua sheria mkononi’’ Aliongeza Gichuru.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Business

Wafanyibiashara wa Shanga wavuna kutokana na watalii Mombasa

Published

on

By

Wafanyibiashara kaunti ya Mombasa wanaendelea kuvuna zaidi kutokana na watalii wa ndani na nje waliozuru kaunti hiyo kufuatia maonyesho ya kimataifa ya Kilimo ambayo yalikamilika siku ya Jumapili.

Kulingana na wafanyibiashara wa kuuza shanga eneo la Lights kaunti ya Mombasa walisema idadi ya watalii ambao walitembelea eneo hilo imefanya biashara kuimarika.

Wakizungumza na CocoFm, walisema bei za Shanga zilipanda kutoka shilingi mia tatu hadi mia tano kwa shanga ndogo huku shanga kubwa zikiuzwa kwa shilingi elfu moja

Hata hivyo waliitaka serikali ya kaunti ya Mombasa kuimarisha usalama katika maeneo mengi ya kaunti hiyo ili kuwavutia watalii zaidi.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending