Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa Walalamikia Ukosefu wa Maji Kwenye Soko Hilo

Published

on

Wafanyabiashara wa Soko la Mtwapa kaunti ya Kilifi wamelalamikia ukosefu wa maji kwenye Soko hilo ambapo wafanyibiashara wengi wanalitegemea kuendeleza shughuli zao za kila siku.

Kulingana na mwenyekiti wa Soko hilo Millicent Mbodze ukosefu wa maji katika soko hilo limeathiri biashara zao kwani maji yanatumiwa kuonsha bishaa nyingi kama vile matunda, mboga na hata samaki kwa wanaouza samaki katika soko hilo.

Aidha amesema wateja wengi wanalalamikia hali mbaya ya ya soko hilo kwani kumejaa uchafu kila mahali hali inayowasababishia kuhofia afya yao.

Amesema tayari wateja wengi wanasusia maeneo hayo jambo ambalo liewasababishishia hasara kubwa kwani bidhaa nyingi huozea sokoni.

Wakati huo huo Mbodze amesema licha ya kuwasilisha swala hilo kwa kwa wahusika sawa na serikali ya kaunti ya Kilifi,bado halijatatuliwa.

Anasema imekuwa changamoto kwa wafanyabiashara kwani imekuwa shida kutumia hata sehemu za kujisaidia sokoni humo huku ikiwalazimu kutafuta bidhaa hiyo kwenye kituo kimoja cha mafuta kilichoko eneo hilo.

Huku hayo yakijiri benki ya dunia imetenga shilingi bilioni 2.58 kuimarisha mpango wa usabasazaji maji katika kaunti ya kilifi.

Mradi huo unalenga miji ya malindi , kilifi na mtwapa na utahusisha kubadilishwa kwa mabomba makuku ya maji na kuweka mabomba mapya.

Ikumbukwe Gavana wa kilifi Gedion Mung’aro alisema miradi hiyo itahakikisha kuwa kaunti hiyo iko na maji safi na yakutosha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Published

on

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.

Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.

Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.

Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.

Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .

Continue Reading

Business

Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Published

on

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.

Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.

Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.

Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.

Continue Reading

Trending