Connect with us

Business

Wafanyabiashara wa Maembe Mariakani Walia na Hasara Kufuatia Mvua

Published

on

Wafanyibiashara wa kuuza maembe katika eneo la mariakani kaunti ya kiliifi wanasema kuwa msimu huu wa mvua biashara iko chini ikilinganishwa na msimu wa kiangazi.

Kulingana na Amina Menza licha ya kuwa maembe ni mengi idadi ya wateja imepungua kutokana na baridi hali ambayo inasababisha maembe kuharibika.

Akizungumza na cocofm Menza amesema mara kwa mara wamekuwa wakikadiria hasara hasa maembe yakinyeshewa huharibika.

Aidha wameitaka serikali kujenga viwanda vya maembe hasa eneo la pwani ili kuwasaidia kuuza maembe na kuikimu kimaisha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wavuvi Old Ferry Wageukia Biashara ya Mahindi Kutokana na Uhaba wa Samaki

Published

on

Baadhi ya wavuvi kutoka eneo la old ferry kaunti ya kilifi wamegeukia biashara ya kuchoma mahindi machanga kutokana na kutoweza kuingia baharini.

Wavuvi hao wamesema kuwa msimu huu wa kusi hakuna samaki hali ambayo imefanya kuingilia biashara ya kuchoma mahindi ili kujiendeleza kimaisha.

Kulingana na wavuvi kutokana na uhaba wa vifaa vya kisasa hawawezi kuingia katika maji marefu ili kuvua samaki.

Hata hivyo wameitaka serikali kuwawezesha na vifaa vya kisasa ili waweze kuvua katika maji marefu.

Continue Reading

Business

Wanawake Pwani Wataka Ushirikishwaji Zaidi Katika Uchumi wa Majini

Published

on

Wanawake kutoka maeneo ya Pwani wanaitaka serikali kuu na zile za kaunti kuhakikisha wanashirikishwa kikamilifu katika sekta ya uchumi wa majini ili kujiendeleza kimaisha.

Wakiongozwa na Mercy Mghanga, wanawake hao wamesema licha ya wanawake wengi kujihusisha na uvuvi na shughuli nyingine za baharini, bado wanakosa vifaa na msaada wa kukuza biashara zao.

Kwa upande wake Linda Shuma wa shirika la Women and Girls Empowerment CBO, amesema kuna haja ya wanawake kushiriki katika michezo ya majini, utalii na usafiri wa baharini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi.

Continue Reading

Trending