Connect with us

Business

Wafanyabiashara Kilifi Walalamikia Ubomozi wa Vibanda Kupisha Ujenzi wa Barabara

Published

on

Wafanyabiashara katika eneo la Misufini kuelekea Kwa Mwango, mjini Kilifi, wameelezea hofu yao kuhusu hatma ya biashara zao kufuatia tangazo la serikali ya kaunti ya Kilifi la kubomoa vibanda katika eneo hilo ili kupisha ujenzi wa barabara mpya.

Wakiongozwa na Isaac Thomas, mfanyabiashara wa bidhaa za rehani, wamesema kuwa mpango huo wa ubomoaji utasababisha hasara kubwa kwao, hasa kupoteza wateja wa kudumu, jambo ambalo linaweza kusambaratisha kabisa biashara zao.

“Biashara hii ndiyo tegemeo langu pekee. Nikiondolewa hapa bila mpango mbadala, nitapoteza wateja wangu na maisha yatakuwa magumu,” alisema Thomas.

Wameiomba serikali ya kaunti kuwapatia eneo mbadala la kufanyia biashara kabla ya kutekeleza zoezi hilo la ubomoaji, wakisisitiza kuwa wengi wao hutegemea biashara hizo kwa riziki ya kila siku.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa serikali ya kaunti, barabara inayopangwa kujengwa kutoka Misufini hadi Kibaoni inapita katika kiwanja kinachomilikiwa na Chuo Kikuu cha Pwani, hali inayowalazimu kuondoa miundo mbinu isiyo rasmi ili kuwezesha ujenzi huo.

Wafanyabiashara sasa wanasubiri kauli ya mwisho kutoka kwa mamlaka husika kuhusu mustakabali wao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Wafanyabiashara Wadogo Kilifi Wakandamizwa na Nauli Ghali

Published

on

Wafanyibiashara wanaotegemea huduma za tuktuk mjini kilifi kaunti ya kilifi wanalalamikia kukadiria hasara kutokana na hatua ya wahudu hao kupandisha nauli.

Wafanyibaisahara hao ambao ni wa kuhamahama wanasema kuwa hatua ya wahudumu wa tuktuk kuongeza bei ya nauli inawakagandamiza kwani hakuna pesa na kuongeza nauli inafanya maisha kuwa magumu.

Kulingana na wafanyibiashara hao imekuwa vigumu kwa wao kusafiri kutoka soko moja hadi nyingine kuendeleza biashara zao hali ambayo imeathiri maisha yao.

Wametolea wito wahudumu hao kuangizia upya swala hilo ili kuwasaidia wafanyibishara hao kuendeleza shughuli zao kwa urahisi.

Wakati huo huo wameitaka serikali na mamlaka ya udhibiti wa kawi kupunguza bei za mafuta .

Continue Reading

Business

Idara ya Vijana Malindi na Magarini Yatishia Hatua Dhidi ya Walioshindwa Kulipa Mikopo

Published

on

Idara ya vijana eneo bunge la Malindi na Magarini kaunti ya Kilifi inayataka makundi ya vijana, wanawake na walemavu yaliyopata mikopo ya hazina ya uwezo kulipa fedha za mikopo hiyo mara moja ili kuwezesha makundi zaidi kunufaika na hazina hiyo.

Kulingana na afisa msimamizi wa idara hiyo Juma Mtana Mwahunga, asilimia kubwa ya makundi yaliyokopa fedha hizo hayajarudisha hivyo kutatiza utekelezaji wa mpango wa hazina ya uwezo eneo hilo.

Mwahunga amekariri kuwa huenda makundi yaliyochukua mikopo hiyo hayakuzitumia fedha hizo kwa njia mwafaka hivyo kushindwa kulipa mikopo yao kwa wakati unaofaa ili kufanikisha mpango huo.

Afisaa huyo aidha amefichua kuwa jumla ya shilingi milioni 10 za hazina hiyo zilitolewa kupitia mikopo kwa makundi hayo huku milioni 3 pekee zikirudishwa kufikia sasa.

Continue Reading

Trending