Connect with us

Business

Wadau wa sekta ya uvuvi walalamikia unyakuzi wa ardhi

Published

on

Kamati ya bunge la kitaifa kuhusu uchumi wa bahari na masuala ya ubaharia imewataka wawekezaji wote waliovamia ardhi zilizotengewa

Kauli hii ilijiri baada ya wavuvi na wasimamizi wa fuo za bahari kuelekeza lalama zao kwa kamati hiyo wakidai kuhangaishwa kila mara na baadhi ya mabwenyenye wanaodaiwa kushirikiana na baadhi ya maafisa wa serikali.

Walidai kwamba unyakuzi huo umekuwa donda sugu na uliadhiri pakubwa shughuli za uvuvi huku wakiitaka serikali ya kitaifa kuingilia kati na kuhakikisha ardhi hizo zinarudhishwa mikononi mwa jamii za wavuvi haraka iwezekanavyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati hiyo na ambaye pia ni mbunge wa Marakwet Mashariki David Kangogo Bowen alisema ujenzi wa kibinafsi katika maeneo ya mita 60 kutoka ukingo wa bahari ni ukiukaji wa sheria kwani maeneo hayo yametengwa mahususi kwa matumizi ya wavuvi.

“Wale wamejenga mita 60 kando ya bahari waondolewa ndio hawa wavuvi wapewe nafasi ya kufanya biashara yao vizuri na pia wapate sehemu ya kuegeza maboti yao”. … alisisitiza David Bowen.

Kauli yake iliungwa mkono na mbunge wa Matunga Kassim Sawa Tandaza aliyesema agizo hilo ni sharti litekelezwa mara moja na yeyote atakayekiuka agizo hilo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

KPA kushirikiana na kaunti ya Siaya kibiashara

Published

on

By

Halmashauri ya bandari Kenya (KPA) pamoja na serikali ya kaunti ya Siaya zimeahidi kushirikiana kwa karibu kuimarisha miundomsingi ya usafiri na biashara katika ukanda wa Ziwa Victoria.

Katika kikao cha viongozi wa pande zote mbili kilichofanyika jijini Mombasa, viongozi hao walijadili miradi ya miundomsingi ya baharini inayolenga kufungua fursa mpya za uwekezaji na mageuzi ya kiuchumi kwa wakazi wa maeneo ya Ziwa Victoria.

Mkurugenzi mkuu wa KPA nahodha William Ruto alithibitisha kuwa usanifu wa kivuko cha Usenge utakamilika ndani ya wiki mbili, huku ikiahidi kushirikiana na Kenya Shipyards Limited kuhakikisha ujenzi wake unakamilika kwa wakati.

Aidha, Ruto alieeleza utayari wa mamlaka hiyo kushirikiana na serikali ya kaunti ya Siaya kuhakikisha miradi hiyo inaendana na vipaumbele vya eneo hilo.

Ruto aliongeza kuwa miradi hiyo inalenga kuchochea uwekezaji, kuongeza nafasi za ajira na kuleta mabadiliko ya kiuchumi katika ukanda wa ziwa.

Kwa upande wake, gavana wa kaunti ya Siaya James Orengo alieleza kuridhishwa na ushirikiano huo, akimpongeza nahodha Ruto kwa uongozi wake wa vitendo akisema kuwa miradi hiyo inaleta matumaini mapya kwa wakazi wa Siaya na ukanda mzima wa Ziwa Victoria.

Taarifa ya Mwanahabari wetu

Continue Reading

Business

Maonyesho ya Kilimo Mombasa 2025 kuangazia uhifadhi wa mazingira

Published

on

By

Washirika kutoka mataifa saba duniani wanatarajiwa kushiriki katika maonyesho ya kimataifa ya kilimo ya mwaka 2025 yanayofanyika eneo la Mkomani kaunti ya Mombasa.

Mwenyekiti wa maonyesho hayo Henry Nyaga, alidokeza kuwa maonyesho hayo yamevutia washirika kutoka mataifa ya afrika mashariki, vile vile mataifa ya India, China, Botswana, Zambia na DR.Congo.

Akizungumza na Coco Fm katika uwanja wa maonyesho hayo, Nyaga alisema maonyesho ya mwaka huu wa 2025 yanaangazia kilimo biashara akisistiza umuhimu wa vijana kushiriki katika hafla hiyo iliyoambatanishwa na matumizi ya teknolojia na mabadiliko ya tabia nchi kwa kuhifadhi mzaingira.

“Kuna wale kutoka mataifa saba ambao tayari wameonyesha watakuwa nasi, tayari amewasili yule ambaye anatoka nchi ya Botswana, tunazingatia mambo haya ya tabia nchi ambayo yamefanya ulimwengu umekuwa tofauti sasa, kwa hivyo tunatarajia washiriki wote watatuonyesha jinsi gani tunaweza kukabiliana na hali hii ya mabadiliko ya tabia nchi, na ningependa haswa vijana muweze kufika hapa katika maonyesho kwa sababu kuna mengi ya kiteknolojia ambayo yanaweza kuwasaidia”,alisema Nyaga.

Kwa upande wake mwenyekiti wa maonyesho ya kilimo nchini Edith Onzare pamoja na mwanachama wa baraza la maonyesho ya Kilimo Mombasa- Anisa Abdhalla waliwasihi wananchi kutumia fursa hiyo kujifunza mengi kuhusu kilimo endelevu na namna ya kujiendeleza kuhusu ufugaji wa kisasa.

“Njooni kwa wingi tutajifunze mengi ya kilimo, kuna mifugo ya aina mbali mbali kuna kilimo na teknolojia hasa kwa vijana wetu, magen z kuna kazi nyingi ambazo ukija hapa kwenye maonyesho utajifunza mambo mengi ya kiteknolojia na taaluma mbali mbali ambazo utaweza kupata usaidizi”,walisema viongozi hao.

Baadhi ya washirika katika maonyesho hayo walishinikiza wakenya kukumbatia kilimo cha kisasa katika kuboresha mapato vile vile kulinda mazingira.

Wakiongozwa Benson Muchiri, waliwahimiza wakulima kujitenga na mbinu za jadi za kupalilia mashamba, akisema zimekuwa zikichangia mazao duni.

Muchiri ambaye amekuwa akitumia chupa na mabomba ya maji yaliyorushwa kuandaa sehemu za kuotesha mbegu kabla ya upanzi, amesema mbinu hiyo inasaidia kuokoa matumizi ya ardhi ipasavyo, sawa na kuhifadhi mazingira.

“Ninataka kuonyesha wakulima jinsi ya kufanya kilimo cha mjini, sio lazima uwe na kipande kikubwa cha ardhi ndio ufanye ukulima hasa kilimo cha mboga, ukiangalia vile vitu tulivyotumia hapa ni vile ambavyo ni kero, ukiangalia tuna chupa za plastiki ambazo tumezitumia, kile ambacho kinachafua mazingira hicho ndio tunahimiza mkulima badala ya hicho kitu kipotee wacha kiwe faida kwako”,alisema Muchiri.

Zaidi ya washirika 200 wanahudhuria maonyesho hayo ambayo yanaanza rasmi Jumatano 3 Septemba 2025, na kukamilika Jumapili 7 Septemba 2025.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending