National News
Viongozi wa ODM Wakashifu Wanaosherehekea Kuanguka Kwa Raila AUC

Viongozi wa Chama cha ODM wamewakashfu baadhi ya wakenya wanaosherehekea kushindwa kwa aliyekuwa mgombea wa Kenya katika wadhfa wa uwenyekiti wa Tume ya umoja wa Afrika AUC Raila Odinga wiki iliyopita.
Wakiongozwa na Mwenyekiti wa chama hicho nchini, Gladys Wanga, ambaye pia ni Gavana wa kaunti ya Homabay wamesema japo hawakutarajia kwamba Odinga angeshindwa katika kinyang’anyiro hicho lakini walikubali matokeo.
Wakizungumza eneo bunge la Likoni katika kaunti ya Mombasa wakati wa kongamano la wajumbe wa chama cha ODM, Wanga amempongeza Rais William Ruto kwa kusimama na Odinga katika uchaguzi huo, akiwakosoa wale waliosherehekea kushindwa kwa Odinga na kuwataja kama wakenya wasio na uzalendo.
Kauli yake imeungwa mkono na Naibu Kinara wa Chama hicho nchini Abdulswamad Sharrif Nassir ambaye pia ni Gavana wa kaunti ya Mombasa akiwakosoa wale wanaodai kwamba serikali ya Kenya Kwanza ilimsaliti Odinga.
National News
Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).
Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa
Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.
Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.
Taarifa Ya Elizabeth Mwende
National News
Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.
Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.
Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.
Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.
Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.
Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.
Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.
Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.
Taarifa ya Joseph Jira