Business
Utalii waimarika Watamu kaunti ya Kilifi

Wadau wa sekta ya utalii wadi ya Watamu kaunti ya Kilifi wameripoti kuimarika kwa sekta ya utalii eneo hilo mwaka wa 2025 ikilinganishwa na mwaka uliopita wa 2024.
Wakiongozwa na mkurugenzi wa hoteli ya Seven Island Ravi Rora, wadau hao walisema kwa sasa sekta hiyo imesajili jumla ya asilimia 25 ya watalii wanaozuru eneo hilo, huku wengine wakitarajiwa kutembelea eneo hilo siku zijazo.
Rora aidha alifichua kuwa asilimia kubwa ya hoteli za Watamu tayari zimepokea idadi kubwa ya maombi ya watalii watakaozuru eneo hilo kwa likizo ya mwezi Disemba.
Wakati huo huo mkurugenzi huyo alibainisha kuwa idadi kubwa ya watalii hao ni wa asili ya kiitaliano, Wafaransa miongoni mwa wa kutoka nchi nyingine.
Alieleza matumaini kuwa hali hiyo itaimarisha uchumi wa kaunti ya Kilifi na Kenya mzima kwa ujumla.
Taarifa ya Pauline Mwango.
Business
Mgomo wa Tuktuk Tezo waathiri biashara

Shughuli za kibiashara katika soko la Tezo kaunti ya kilifi ziliathirika jumatatu ya Julai, 21, 2025 kufuatia mgomo wa wahudumu wa tuktuk.
Kulingana na wafanyibiashara katika soko hilo, wengi wao wanategemea huduma za tuktuk kusafirisha bidhaa zao hadi katika soko hilo.
Wakizungumza na cocofm wafanyibiashara hao waliongeza kuwa wateja wengi pia hutegemea usafiri wa tuktuk kufika sokoni humo, na kufuatia mgomo huo wengi walikosa kufika hali ambayo iliwasababishia hasara kubwa.
Aidha waliitaka sekta ya tuktuk kurejesha huduma hizo ili kuwapa afueni wafanyibiashara ikizingatiwa kuwa wanategemea biashara kujikimu kimaisha.
Mgomo huo wa wahudumu wa tuktuk uliwapa wadumu wa bodaboda mjini kilifi kaunti ya kilifi fursa ya kuvuna zaidi kimapato.
Kulingana na wanaboda wa eneo la Tezo mgomo wa wahudumu wa tuktuk uliwapelekea fursa ya kuongeza nauli kutokana na idadi kubwa ya wateja.
Kutoka eneo la Tezo hadi Chumani wahudumu hao walibeba abiria mmoja kwa shilingi 200 tofauti na shilingi 100 ya hapo awali.
Wahudumu wa tuktuk waligoma kutokana na kupanda kwa bei za mafuta aina ya petroli na dizeli, hali ambayo wanasema inasawababishia harasa kubwa.
Taarifa ya Pauline Mwango
Business
Kanisa Katoliki lahimiza umuhimu wa Kilimo

Kasisi wa Kanisa Katoliki jimbo la Malindi Misheni ya Mere kaunti ya Kilifi, Blaise Kamau Andrew ametoa wito kwa wenyeji wa Pwani kuwekeza zaidi katika kilimo cha kisasa ili kupata chakula cha kutosha na kilicho bora.
Akizungumza katika eneo la Kwa Ndomo eneo bunge la Malindi, Kasisi Kamau aliesema ikiwa Wapwani watatia juhudi katika sekta ya kilimo huenda kukawa na mavuno mengi na chakula cha kutosha ili kudhibiti njaa wakati wa kiangazi.
Kasisi Kamau pia aliwashinikiza kuchimba visima vingi vya maji ili panapokosekana mvua kuwe na maji ya kutosha ya kuendeleza kilimo nyunyizi.
“Chibeni visima ili usiwe mkulima wa kungojea tu mvua ya mwenyeji Mungu.Tufanyeni bidi wengi wenu wana Ng’ombe, wengi wenu wana mbuzi uza Ng’ombe mbili, chimba kisima maji hayako mbali sana ili mvua ikikatika bado mnaendeleza kilimo nyunyizi’’, alisema Kasisi Kamau.
Ni kauli ambayo imeungwa mkono na msimamizi wa kitengo cha chakula na Kilimo katika benki ya Equity tawi la Nairobi, George Macharia ambaye alisema ili kuimarisha uchumi wa Kenya ni lazima Wapwani na wakenya kwa jumla wakumbatie kilimo cha kisasa kupitia mfumo wa teknolojia.
“Ili tuweze kupanua uchumi ni lazima tuwekeze katika kilimo na tuhakikishe tunatumia kilimo cha kisasa cha kiteknolojia’’, Macharia aliwasihi Wakulima.
Taarifa ya Janet Mumbi