Connect with us

Sports

Ureno Mabingwa Uefa Nations Ligi

Published

on

Timu ya taifa la Ureno ndiyo mabingwa taji la Uefa Nations Ligi baaday ya kucharaza majirani wao Uhispania magoli 5-3 kupitia matuta au Penalti ukipenda

Hii baada ya timu zote kutoshana nguvu magoli 2-2 muda wa kawaida na ule ziada mechi iliopigwa ugani Allianz Arena.

Kiungo anayeiwindwa na Arsenal Martin Zubimendi aliwaweka uongozini The La Furia Rojas kwa faida ya Uhispania kunako dakika ya 21 kabila ya beki matata wa kushoto Nuno Mendes kuishazishia Ureno kunako dakika 26 kipindi cha kwanza.

Mshambulizi wa Real Sociadad Mikel Oyarzabal alirejesha tena mabingwa hao watetezi uongozini kunako dakika ya 45 kabila mshmabulizi nguli na mwamba wa miaka mingi Christiano Ronaldo kusawazishia Ureno dakika 61 kipindi cha pili.

Katika mechi ya kutafuta nafasi ya tatu Ufaransa walinyuka Ujerumani magoli 2-0.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Liverpool Kuwasilisha Ofa Mpya Kusajili Wirtz

Published

on

By

Mabingwa wapya wa ligi ya Epl liverpool inatarajiwa kuwasilisha ofa nyingine kusaka hudumza kiungo matata wa Ujerumani Florian Wirtz.

Hii ni Baada ya kilabu ya Bayer Leverkusen kukataa ofa ya pauni milioni 113 kutoka kwa usajli wa mchezaji huyo ambaye ameweka wazi yuko tayari kujiunga na The Reds msimu ujao.

Leverkusen imeshikilia kuwa inahitaji kitita cha pauni milioni 126 kumwachilia nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 ambaye pia anamezewa mate na Real Madrid ya Uhispania na Manchester City wa Uingereza.

Inaaminika mchezaji huyo ndiye atakua sajili wa kwanza kwa kocha mkuu Arne Slot msimu huu wakiwa tayari kuwachiliwa nyota wake akiwemo mshmabulizi Darwin Nunez,Federico Chiesa,Harvey Elliot na Kostas Tsimiskas ambao wote wataondoka ugani Anfield.

Continue Reading

Sports

Kocha Wa Starlets Odemba ajiuzulu

Published

on

By

Mkufunzi wa timu ya taifa soka akina dada Harambee Starlets Beldine Odemba ametangaza kujizulu wadhifa wake kama kocha mkuu wa kikosi hicho baada ya kichapo cha magoli 5-1 na Morocco mechi ya kirafiki.

Kwa mujibu wa mwalimu huyo kilichomfanya kuondoka katika kambi ya timu hiyo ni kukosa ungwaji mkono katika kazi yake ya kunoa starlets akiondoka siku chache tuu kabla ya kungoa nanga kwa taji Cecafa nchini Tanzania Juni 12.

Mkufunzi huyo ambaye ameshinda ligi ya akina dada na kilabu ya Kenya Bullets amedokeza kwamba ni swala ambalo ameliwazia kwa muda na kwa sasa anaelekeza nguvu zote kwa kikosi hicho taji la Cecafa baina ya vilabu.

Ripoti zinaarifu kwamba kocha wa Kibera Soccer Women David Vijago atatangazwa kocha mpya wa Starlets akisaidiana na Alex Alumira ambaye amewahi kuwa kocha wa timu hiyo.

Continue Reading

Trending