Connect with us

Sports

Ureno Mabingwa Uefa Nations Ligi

Published

on

Timu ya taifa la Ureno ndiyo mabingwa taji la Uefa Nations Ligi baaday ya kucharaza majirani wao Uhispania magoli 5-3 kupitia matuta au Penalti ukipenda

Hii baada ya timu zote kutoshana nguvu magoli 2-2 muda wa kawaida na ule ziada mechi iliopigwa ugani Allianz Arena.

Kiungo anayeiwindwa na Arsenal Martin Zubimendi aliwaweka uongozini The La Furia Rojas kwa faida ya Uhispania kunako dakika ya 21 kabila ya beki matata wa kushoto Nuno Mendes kuishazishia Ureno kunako dakika 26 kipindi cha kwanza.

Mshambulizi wa Real Sociadad Mikel Oyarzabal alirejesha tena mabingwa hao watetezi uongozini kunako dakika ya 45 kabila mshmabulizi nguli na mwamba wa miaka mingi Christiano Ronaldo kusawazishia Ureno dakika 61 kipindi cha pili.

Katika mechi ya kutafuta nafasi ya tatu Ufaransa walinyuka Ujerumani magoli 2-0.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending