Sports
United Wamewasilisha Ofa Kumsajili Mbeumo

Kilabu ya Manchester United imewasilisha ofa ya pauni milioni 55 kwa kilabu ya Brenford kuhusiana na uhamisho wa winga matata Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Hata hivyo ofa hiyo inatarajiwa kukataliwa na Brenford ambao wanataka pauni milioni 60 kumwachilia mchezaji huyo ambaye aliwasaidia pakubwa msimu ambao umekamilika.
Mchezaji huyo mwneye umri wa miaka 26 ameambia United anataka mshahara wa kitita cha pauni laki 250,000 kila wiki ili aweze kutua OLd Trafford licha ya kulipwa pauni Elfu 50 kila wiki na Brenford.
Mbeumo alifunga magoli 20 msimu ambao umekamilika na kuchangia mengine 9 na kusaidia The Bees kumaliza ya 10 ligi ya Epl na licha ya kumezewa mate na vilabu vya Arsenal,Newcastle United amesema chaguo lake la kwanza na kutua Old Trafford msimu ujao.
Iwapo United watapata sahihi yake basi atakua sajili wa pili kwa kocha Ruben Amorim baada ya kupata mshambulizi Matheus Cunha.
Sports
Harambee Stars Kuvaana Na Chad Mechi Ya Kirafiki.

Timu ya Taifa Harambee Stars chini ya kocha Benni Mccarthy kushuka dimbani majira saa kumi jioni Ugani Stade de Marrakech Morocco ikiwa ni mechi ya kirafiki.
Kwa mujibu wa mwalimu wa Stars Mccarthy mechi hizi ni muhimu kujenga kikosi kwa majukumu ya siku za usoni lakini pia kwa taji la Chan sawa na Afcon mwaka 2027.
“Ni muda mzuri mimi kufahamu vijana wangu na kuanza kuanda timu yenye ubora kwa minajili ya siku za usoni na wachezaji wa nyumabani watasaidia sana CHAN mwezi Agosti.”
Baada ya mechi hiyo Stars watacheza mechi nyingine na taifa hilo Juni 10.
Rais wa Fkf Hussein Mohammed amekariri kikosi hicho kitaelekea Uarabuni kwa maozezi kabambe kabila ya Chan humu nchini.
Sports
Kenya Pipeline Yaanza Kwa Kishindo Fainali Ya Voliboli

Kilabu ya Kenya Pipeline ilianza kwa kishindo fainali ya taji la akina dada mchezo wa voliboli mashidano yanayondelea uwanjani Kasarani Indoor Arena jijini Nairobi.
Hii ni baada ya vipusa hao chini ya kocha Godfrey Omondi kuwatandika wenzao DCI seti 3-0 mechi ya ufunguzi uwanja huo ukifurika hadi pomoni.
Kikosi hicho kilishinda mechi hiyo kwa seti 25-19,25-20,25-14 na kuibuka na ushindi huo mnono kabila ya mechi ya pili jumamosi.
Nahodha wa KPC Gladys Ereng amesema kwamba mechi haikua rahisi kwani DCI walikua vizuri ila walipambana kwa ushindi huo.
“DCI ni timu nzuri walicheza vizuri kipindi cha kwanza kwani tulianza kwa utepetevu ila tukazungumza na kujikusanya vyema na kupata ushindi huo muhimu kwetu.”
Kwa Upende wake kocha wa DCI Patrick Sang amedokeza kwamba hakucheza kwa umakinifu waliotarajia;”Hatukucheza kwa mipangilio yetu mazungumzo pamoja na utulivu haikuwepo lakini ndio hali ya mchezo nipongeze wenzetu.”
Kilabu ya General Service Unit (GSU) upande wa wanaume ilianza vema kusaka taji la upande wa Wanaume baada ya kushinda mechi ya mkondo kwanza sati 3-0 katika uwanja huo huo.
Hii ni baada ya kuwatandika Kenya Ports Authority (KPA) seti 3-0 za 25-15,25-22,30-28