Connect with us

Sports

United Wamewasilisha Ofa Kumsajili Mbeumo

Published

on

Kilabu ya Manchester United imewasilisha ofa ya pauni milioni 55 kwa kilabu ya Brenford kuhusiana na uhamisho wa winga matata Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.

Hata hivyo ofa hiyo inatarajiwa kukataliwa na Brenford ambao wanataka pauni milioni 60 kumwachilia mchezaji huyo ambaye aliwasaidia pakubwa msimu ambao umekamilika.

Mchezaji huyo mwneye umri wa miaka 26 ameambia United anataka mshahara wa kitita cha pauni laki 250,000 kila wiki ili aweze kutua OLd Trafford licha ya kulipwa pauni Elfu 50 kila wiki na Brenford.

Mbeumo alifunga magoli 20 msimu ambao umekamilika na kuchangia mengine 9 na kusaidia The Bees kumaliza ya 10 ligi ya Epl na licha ya kumezewa mate na vilabu vya Arsenal,Newcastle United amesema chaguo lake la kwanza na kutua Old Trafford msimu ujao.

Iwapo United watapata sahihi yake basi atakua sajili wa pili kwa kocha Ruben Amorim baada ya kupata mshambulizi Matheus Cunha.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending