Sports
United Wamewasilisha Ofa Kumsajili Mbeumo

Kilabu ya Manchester United imewasilisha ofa ya pauni milioni 55 kwa kilabu ya Brenford kuhusiana na uhamisho wa winga matata Bryan Mbeumo raia wa Cameroon.
Hata hivyo ofa hiyo inatarajiwa kukataliwa na Brenford ambao wanataka pauni milioni 60 kumwachilia mchezaji huyo ambaye aliwasaidia pakubwa msimu ambao umekamilika.
Mchezaji huyo mwneye umri wa miaka 26 ameambia United anataka mshahara wa kitita cha pauni laki 250,000 kila wiki ili aweze kutua OLd Trafford licha ya kulipwa pauni Elfu 50 kila wiki na Brenford.
Mbeumo alifunga magoli 20 msimu ambao umekamilika na kuchangia mengine 9 na kusaidia The Bees kumaliza ya 10 ligi ya Epl na licha ya kumezewa mate na vilabu vya Arsenal,Newcastle United amesema chaguo lake la kwanza na kutua Old Trafford msimu ujao.
Iwapo United watapata sahihi yake basi atakua sajili wa pili kwa kocha Ruben Amorim baada ya kupata mshambulizi Matheus Cunha.
Sports
Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Sports
Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo
