Connect with us

Entertainment

Ullulations! Sister Shanniez Afunga Ndoa Mtwapa

Drumrolls tafadhali! 🔔🎉 Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, hatimaye ametoka soko rasmi! Harusi ya kifahari ya kimyakimya, katikati ya jiji la Mtwapa, imegeuza Jumamosi kuwa sinema ya mapenzi ya Pwani. Wageni wachache lakini mashuhuri, vibes za Coco, na miondoko ya kimahaba—ni kama movie, lakini real life! 💍✨”

Published

on

Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, ameanza ukurasa mpya wa maisha kwa kufunga ndoa katika harusi ya kifahari lakini ya faragha, iliyofanyika Jumamosi Mei 31, katikati mwa jiji la Mtwapa, kaunti ya Kilifi.

Harusi hiyo, iliyosheheni uzuri wa Pwani na mvuto wa mazingira ya kimahaba, ilifanyika kwa mwaliko maalum kwa watu wa karibu tu.

Miongoni mwa waliohudhuria walikuwa ni jamaa wa familia, marafiki wa karibu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake kutoka Coco FM, waliokuja kushuhudia tukio hilo la kihistoria kwa ukaribu na heshima .

Watangazaji waliokuwa miongoni mwa wageni maalum ni Hamisi Kombe, Mamaa Madikodiko, Teddy Mwanamgambo, Hon Baba Yaga, Kassim Mbui, Binti Umazi, Sifa na Patrick. Uwepo wao katika sherehe hiyo ulidhihirisha mshikamano na urafiki wa kweli uliopo ndani ya familia ya redio hiyo.

Sister Shanniez, anayefahamika kwa sauti yake yenye mvuto na ucheshi wa kipekee hewani kupitia kipindi cha Coco Drive kinachorushwa kila Jumatatu hadi Ijumaa, ameendelea kuwa mfano wa mwanamke jasiri na mwenye msimamo maishani. Mbali na umahiri wake kitaaluma, harusi yake imefungua ukurasa mpya unaodhihirisha utu uzima na maamuzi ya busara katika maisha binafsi.

Kinachovutia zaidi ni kuwa maandalizi na taarifa kuhusu harusi hiyo yalisalia kuwa siri kubwa hadi siku yenyewe ya tukio. Ukimya huo wa kimakusudi ulitoa nafasi ya sherehe hiyo kufanyika kwa utulivu, upendo na heshima ya kipekee, bila minong’ono wala mkorogo wa hadhara.

Ingawa bado hakujatolewa taarifa rasmi kutoka kwake kuhusu tukio hilo, waliokuwepo wameelezea harusi hiyo kama yenye haiba, hisia, na ladha ya mapenzi ya kweli. Tangu kuwasili kwa bibi harusi hadi kwenye mankuli, kila hatua ilikuwa ya kipekee na ya kupendeza.

Ni wazi na dhahiri kuwa sura mpya ya maisha yake ya ndoa inaleta mvuto mpya katika safari yake ya maisha ya ndani na nje ya taaluma yake.

Hapa COCO FM tunasema kila lenye Kheri dada Shanniez na Mwenyezi Mungu akujalie mema kwenye ukurasa huu mpya wa maisha ya ndoa, Amen🙏🏼

Continue Reading
2 Comments

2 Comments

  1. Asha kassim

    May 31, 2025 at 9:02 pm

    Congratulations my fave Mungu akujalie kheri njema katika ndoa Yako as your biggest fan am proud of you dear we love you so much đź’•đź’•đź’•đź’–đź’–đź«‚đź«‚đź«¶đź«¶đź«¶

  2. Aisha

    June 1, 2025 at 7:39 pm

    Pongezi dada sister shanniz.
    Karibu ndani yake tukaendeshe

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Mboga Imejileta; Arrow Bwoy Aitisha Pigano Dhidi ya Shakib

Published

on

Msanii maarufu wa Kenya, Arrow Bwoy, amezua gumzo mtandaoni baada ya kumualika wazi wazi mfanyabiashara kutoka Uganda, Shakib Cham, kwenye pambano la ndondi.

Hii imekuja baada ya kipigo cha hadharani ambacho Shakib alipokea kutoka kwa msanii mwenzake wa Uganda, Rickman, hali iliyoacha mashabiki wengi wakisema: “Sasa ata Arrow Bwoy anaweza!”

Kupitia video inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii, Arrow Bwoy, anayefahamika kwa vibao kama Digi Digi, hakuonyesha woga wowote. Kwa ucheshi, alisema amekuwa akisubiri nafasi kama hii kwa muda mrefu.

“Mboga imejileta,” alisema kwa kujiamini, akimaanisha kuwa Shakib amejileta mwenyewe kwenye kipigo.

“Chakula kiko tayari. Niko tayari kwa pambano hili.”

Arrow Bwoy pia hakusita kumtaja mke wa Shakib, Zari Hassan, akimtaka akae mbali na ulingo siku ya pambano hilo kwa usalama wake binafsi.

“Zari, usijisumbue kuja. Hii si sehemu ya wanawake. Usije ukazimia tukapata janga la pili,” alisema kwa kejeli.

Hata hivyo, wakosoaji wake walikumbusha jamii kuhusu video za awali zinazoonyesha Arrow Bwoy akichapwa na polisi wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha. Swali likabaki: Je, kweli ana uwezo wa kumpiga Shakib au ni porojo za mitandaoni?

Kwa jina la Zari kuingizwa kwenye sakata hili, mvutano umeongezeka na mashabiki kote Afrika Mashariki wanasubiri kuona kama Shakib atakubali changamoto hii ya kihistoria.

“Zari, kama unasikia, mtume tu kijana wako aje achukue kichapo — kichapo cha kimataifa,” Arrow Bwoy alimalizia kwa msisitizo.

Kwa sasa, macho yote yako kwa Shakib. Je, atakubali changamoto hii na kuweka historia mpya ya burudani Afrika Mashariki?

Continue Reading

Entertainment

#CHAN2024: Savara, Zuchu na Eddy Kenzo Kutumbuiza Fainali ya CHAN 2024 Nairobi

Published

on

Mashindano ya CHAN 2024 yakielekea ukingoni, mashabiki wanatarajiwa kupata burudani ya aina yake kutoka kwa baadhi ya nyota wakubwa wa muziki Afrika Mashariki.

Kenya, Uganda na Tanzania zitawakilishwa vilivyo kupitia majina makubwa matatu: Savara wa Kenya (mwanachama wa zamani wa kundi maarufu Sauti Sol), Eddy Kenzo wa Uganda, na Zuchu kutoka Tanzania, anayejulikana kwa jina halisi Zuhura Othman.

Onyesho hili la kufunga pazia litafanyika sambamba na mechi ya fainali Jumamosi, likitarajiwa kuhamasisha na kuburudisha maelfu ya mashabiki watakaofurika uwanja wa Kasarani. Shoo hiyo inalenga kumaliza mashindano haya ya kihistoria kwa upekee na kiwango cha juu cha burudani.

Mbali na kusubiriwa kwa hamu jukwaani, Savara pia amekuwa na mchango mkubwa nyuma ya pazia. Yeye ndiye mtunzi na mtayarishaji wa wimbo rasmi wa CHAN 2024 unaoitwa “Pamoja”.

Wimbo huo unashirikisha nyota kutoka kanda hii: Elijah Kitaka wa Uganda na Phina wa Tanzania. Uliimbwa kwa mara ya kwanza katika sherehe za ufunguzi na uliweka ladha na hamasa ya mashindano haya.

Ingawa wenyeji wa mashindano haya—Kenya, Uganda na Tanzania—waliishia katika hatua ya robo fainali, fainali za mwaka huu zinaahidi kuwa kilele cha msisimko.

Burudani kutoka kwa Zuchu, Savara na Eddy Kenzo itakuwa chachu ya kuhitimisha mashindano yaliyojaa matukio na hisia.

Kwa upande mwingine, kumekuwa na malumbano mitandaoni kati ya mashabiki wa Kenya na Tanzania, hususan baada ya timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, kudondoshwa nje ya michuano hiyo katika robo fainali.

Mashabiki wa Tanzania hawakusita kuchokoza wenzao kwa kejeli, jambo lililoongeza ladha ya ushindani wa nje ya uwanja.

Continue Reading

Trending