Entertainment
Ullulations! Sister Shanniez Afunga Ndoa Mtwapa
Drumrolls tafadhali! 🔔🎉 Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, hatimaye ametoka soko rasmi! Harusi ya kifahari ya kimyakimya, katikati ya jiji la Mtwapa, imegeuza Jumamosi kuwa sinema ya mapenzi ya Pwani. Wageni wachache lakini mashuhuri, vibes za Coco, na miondoko ya kimahaba—ni kama movie, lakini real life! 💍✨”

Mtangazaji mahiri wa Coco FM, Sister Shanniez, ameanza ukurasa mpya wa maisha kwa kufunga ndoa katika harusi ya kifahari lakini ya faragha, iliyofanyika Jumamosi Mei 31, katikati mwa jiji la Mtwapa, kaunti ya Kilifi.
Harusi hiyo, iliyosheheni uzuri wa Pwani na mvuto wa mazingira ya kimahaba, ilifanyika kwa mwaliko maalum kwa watu wa karibu tu.
Miongoni mwa waliohudhuria walikuwa ni jamaa wa familia, marafiki wa karibu pamoja na baadhi ya wafanyakazi wenzake kutoka Coco FM, waliokuja kushuhudia tukio hilo la kihistoria kwa ukaribu na heshima .
Watangazaji waliokuwa miongoni mwa wageni maalum ni Hamisi Kombe, Mamaa Madikodiko, Teddy Mwanamgambo, Hon Baba Yaga, Kassim Mbui, Binti Umazi, Sifa na Patrick. Uwepo wao katika sherehe hiyo ulidhihirisha mshikamano na urafiki wa kweli uliopo ndani ya familia ya redio hiyo.
Sister Shanniez, anayefahamika kwa sauti yake yenye mvuto na ucheshi wa kipekee hewani kupitia kipindi cha Coco Drive kinachorushwa kila Jumatatu hadi Ijumaa, ameendelea kuwa mfano wa mwanamke jasiri na mwenye msimamo maishani. Mbali na umahiri wake kitaaluma, harusi yake imefungua ukurasa mpya unaodhihirisha utu uzima na maamuzi ya busara katika maisha binafsi.
Kinachovutia zaidi ni kuwa maandalizi na taarifa kuhusu harusi hiyo yalisalia kuwa siri kubwa hadi siku yenyewe ya tukio. Ukimya huo wa kimakusudi ulitoa nafasi ya sherehe hiyo kufanyika kwa utulivu, upendo na heshima ya kipekee, bila minong’ono wala mkorogo wa hadhara.
Ingawa bado hakujatolewa taarifa rasmi kutoka kwake kuhusu tukio hilo, waliokuwepo wameelezea harusi hiyo kama yenye haiba, hisia, na ladha ya mapenzi ya kweli. Tangu kuwasili kwa bibi harusi hadi kwenye mankuli, kila hatua ilikuwa ya kipekee na ya kupendeza.
Ni wazi na dhahiri kuwa sura mpya ya maisha yake ya ndoa inaleta mvuto mpya katika safari yake ya maisha ya ndani na nje ya taaluma yake.
Hapa COCO FM tunasema kila lenye Kheri dada Shanniez na Mwenyezi Mungu akujalie mema kwenye ukurasa huu mpya wa maisha ya ndoa, Amen🙏🏼
Entertainment
Chris Brown Akanusha Shtaka la Kumshambulia Producer kwa Chupa

Msanii nyota wa Marekani, Chris Brown, amekana mashtaka mawili mahakamani yanayohusiana na madai ya shambulio kwa kutumia chupa katika kilabu cha usiku jijini London miaka miwili iliyopita.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 anatuhumiwa kumsababishia mtayarishaji wa muziki majeraha ya mwili katika tukio ambalo waendesha mashtaka wamelieleza kuwa “halikuwa na uchochezi wowote”.
Pia anakabiliwa na shtaka la kumiliki silaha hatari — ambayo ni chupa ya kileo.
Mashtaka haya mawili yaliongezwa mwezi uliopita kwenye shtaka la awali, kubwa zaidi, la kujaribu kumsababishia mtu majeraha mabaya ya mwili (GBH), ambalo tayari Bwana Brown alilishatupilia mbali kwa kujitetea kuwa si kweli.
Chris Brown anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kesi hiyo mwezi Oktoba mwaka 2026.
Waendesha mashtaka wamesema kuwa mhanga wa tukio hilo, Abraham Diaw, alikuwa amesimama kwenye baa ya kilabu cha usiku kilichopo eneo la Soho mnamo tarehe 19 Februari 2023, wakati Chris Brown alimpiga kwa chupa mara kadhaa.
Mwimbaji huyo alikamatwa mwezi Mei katika hoteli ya nyota tano iliyopo Salford, Greater Manchester, baada ya kurejea Uingereza kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya muziki barani Ulaya.
Alizuiliwa korokoroni kwa takriban wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa dhamana baada ya kukubali kulipa ada ya dhamana ya pauni milioni tano (£5m) kwa mahakama.
Ada ya dhamana ni kiasi cha fedha kinachowekwa kama dhamana ya kifedha kuhakikisha mtuhumiwa atarudi mahakamani kwa kesi yake. Brown anaweza kupoteza fedha hizo endapo atakiuka masharti ya dhamana, ambayo yaliendelezwa katika kikao cha mahakama siku ya Ijumaa.
Kwa mujibu wa masharti hayo, Chris Brown anatakiwa kuishi katika anwani iliyopo Uingereza akisubiri kesi hiyo, na aliamriwa kukabidhi pasipoti yake kwa polisi.
Hata hivyo, ameruhusiwa kuendelea na ratiba ya ziara yake ya kimataifa ya Breezy Bowl XX kwa masharti kwamba atakabidhi pasipoti kila anapomaliza safari, na kuirudishiwa anapohitaji kusafiri kwa ajili ya maonesho.
Katika wiki za hivi karibuni, Brown amekuwa akitumbuiza kwenye viwanja na kumbi mbalimbali za burudani kote Uingereza na Ulaya, na kumaliza burudani mjini Paris mwishoni mwa wiki iliyopita. Sehemu ya ziara hiyo inayofanyika Marekani Kaskazini inatarajiwa kuanza baadaye mwezi huu na kufikia tamati tarehe 18 Oktoba.
Kikao kingine cha mahakama kimepangwa kufanyika tarehe 24 Oktoba.
Chris Brown ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa zaidi wa R&B nchini Marekani, akiwa mshindi wa tuzo mbili za Grammy na nyimbo 19 zilizofika katika nafasi 10 za juu kwenye chati za Uingereza, zikiwemo Turn Up The Music, Freaky Friday, With You na Don’t Wake Me Up.
Mshitakiwa mwenza, Omololu Akinlolu, raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 anayefahamika kisanii kama HoodyBaby, naye pia alikana shtaka la kumsababishia mtu majeraha ya mwili. Awali, alikana pia shtaka la kujaribu kusababisha majeraha mabaya ya mwili.
Chanzo: BBC
Entertainment
Justin Bierber Arejea na Album Mpya ‘SWAGG’

Msanii nyota wa muziki wa kimataifa, Justin Bieber, hatimaye ameachia rasmi albamu yake mpya na ya saba kwa jina “Swag”, ikiwa ni albamu yake ya kwanza tangu mwaka 2021 alipotoa Justice. Albamu hii imetoka leo na tayari imeanza kutikisa majukwaa mbalimbali ya muziki duniani.
Swag imejumuisha mastaa kadhaa akiwemo Gunna, Sexyy Red, Cash Cobain, pamoja na wasanii wengine wa kizazi kipya.
Albamu hiyo ina jumla ya nyimbo 20 na tayari baadhi ya vibao kama “Go Baby”, “Soulful” na Butterflies “zimeanza kupokelewa vizuri kwenye mitandao ya Spotify, Apple Music na YouTube.
Hii ni mara ya kwanza kwa Bieber kuachia albamu tangu alipopata matatizo ya kiafya mwaka 2022 yaliyosababisha asitishe ziara yake ya kimataifa ya Justice World Tour ambayo ilikuwa iendelee hadi mwaka 2023.
Ziara hiyo ilisitishwa mnamo Septemba 2022 baada ya Bieber kupatwa na maradhi ya Ramsay Hunt Syndrome, ugonjwa uliomsababishia kupooza upande mmoja wa uso.
Kwa kipindi cha miaka minne bila kazi mpya, mashabiki wa Justin Bieber duniani wamekuwa wakimsubiria kwa hamu ujio wa kazi mpya kutoka kwake. Kupitia Swag, msanii huyo ameonyesha kurejea kwa nguvu na ubunifu wa hali ya juu, huku akiwa katika hali nzuri kiafya na kisaikolojia.
Taarifa na Francos Mzungu
Asha kassim
May 31, 2025 at 9:02 pm
Congratulations my fave Mungu akujalie kheri njema katika ndoa Yako as your biggest fan am proud of you dear we love you so much 💕💕💕💖💖🫂🫂🫶🫶🫶
Aisha
June 1, 2025 at 7:39 pm
Pongezi dada sister shanniz.
Karibu ndani yake tukaendeshe