Connect with us

Entertainment

#UlijanjarukaVipi! Safari ya Mpishi Nguli, Don Moses: Kutoka Kukosa Karo Hadi Kuwa Head Chef

Published

on

Katika dunia ya leo ambapo changamoto za kiuchumi zimewaacha vijana wengi wakihangaika, simulizi ya Don Moses ni mwanga wa matumaini kwa wengi.

Akiwa mgeni katika kipindi cha Janjaruka 254, kinachorushwa kila siku ya wiki kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa, Moses alisimulia safari yake ya ajabu kutoka kwa kijana aliyezuiwa na karo ya shule hadi kuwa mpishi mashuhuri hadi kuwa Head Chef aliyesimamia wapishi waliosomea fani hiyo chuoni.

Baada ya kuhitimu kidato cha nne, Moses alikuwa ameweka ndoto ya kujiunga na chuo lakini maisha yalikuwa na mpango tofauti. Mama yake alipata ajali mbaya, hali iliyolazimu familia kuhamishia raslimali kwenye matibabu badala ya karo yake ya chuo.

“Nilijua wazi kuwa singeweza kulazimisha familia ichague kati ya maisha ya mama na elimu yangu. Ilibidi nitafute njia mbadala,” anasema Moses.

Jiko la YouTube: Darasa la Ukombozi

Akiwa hana karo, lakini akiwa na shauku, Moses alianza kujifunza sanaa ya upishi kupitia video za YouTube. Binamu yake, Moses Gambo, ndiye aliyemfungulia mlango wa maarifa kwa kumtambulisha kwenye tutorials mbalimbali mtandaoni.

Ni ujuzi huo wa mtandaoni uliomfungulia milango ya ajira katika hoteli za kifahari, ambapo aliweza kupanda ngazi hadi kuwa mpishi mkuu (Head Chef) — akiongoza wapishi waliopitia vyuo vya kitaaluma. Ni mafanikio ambayo wengi hawakuyatarajia kutoka kwa kijana ambaye hakuingia darasa la kawaida, bali alikaa mbele ya skrini.

“Najua kwenye upishi kuna kupika mashendea ama kupika chakula kibaya ila sijawahi kufeli. Siku zote mimi ni makini na ratio ya viungo. Ndiyo silaha yangu,” anasema kwa kujiamini.

Mwaka wa Mageuzi: 2020

Kama ilivyokuwa kwa wengi, mwaka wa janga la COVID-19 – 2020 – ndiyo ulikuwa mwaka wa mabadiliko makubwa kwa Moses. Akiwa na muda mwingi na motisha mpya, alianza kupika kibiashara, akihudumia watu waliokuwa majumbani.

“Kabula ya hapo, nilikuwa napika kwa kujifurahisha tu. Lakini corona ilinifungua macho. Nikaanza kuona kuwa mapishi ni biashara yenye nguvu,” anasema Moses.

Karo Iliyogeuka Mtaji

Kipindi fulani baadaye, Moses alipata nafasi ya kujiunga na chuo hatimaye. Lakini kwa mshangao wa wengi, alikataa ofa hiyo kwa hiari na kuomba fedha hizo zitumike kupanua biashara yake ya upishi.

“Nitamudu gharama ya chuo siku moja. Kwa sasa, najenga misingi. Muda wa kusoma utafika,” anasema.

💡 Ushauri kwa Vijana: Anza na Kile Kilicho Mkono Wako

Don Moses sasa ni sauti ya matumaini kwa vijana wengi wanaohisi kuwa elimu ya juu au mtaji mkubwa ndio tiketi pekee ya mafanikio. Anasisitiza umuhimu wa kuanza na huduma, si lazima mtaji.

“Kama huna kazi wala mtaji, toa huduma kwanza. Ukiwa na bidii na ubunifu, malipo yatafuata,” anashauri.

Leo hii, sehemu kubwa ya mapato ya Moses huingia moja kwa moja kwenye ununuzi wa vifaa bora vya upishi, huku akiendeleza ndoto yake ya kuwa mmoja wa wapishi wakubwa zaidi nchini Kenya.

Continue Reading
1 Comment

1 Comment

  1. Austine oscar

    June 6, 2025 at 10:12 pm

    Tumeona kazi zako Boss kupitia mm mkufunzi wako heko na kupa cha zaidi nakuombea heri na mafanikio mema na uishi maisha marefu ju isingekuwa ww singekuwa mahali nilipo nashkuru Mungu Sana kwa umbali umenitoa ningetamani pia mm nifike mahali upo na Niko na Imani kubwa Sana hata ww mwenyewe walijuwa hilo ila IPO siku 🧨🙏

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Paula Kajala Afunguka Sababu ya Kumtema Rayvanny

Published

on

Mwanamitindo na mtangazaji maarufu kutoka Tanzania, Paula Kajala, hatimaye amevunja ukimya na kueleza sababu za kuachana na msanii nyota Rayvanny.

Katika mahojiano ya wazi, Paula alifichua kuwa uhusiano huo haukuweza kudumu kwa sababu ya kile alichokitaja kama kukosa uthabiti na kutoheshimu hisia za wanawake kwa upande wa msanii huyo.

Paula alisema kuwa safari yake ya mapenzi na Rayvanny ilikuwa ngumu na ya kukatisha tamaa.

“Hajali hisia za mtu yeyote. Alikuwa na Fahima, akaja kwangu, baadaye akaonekana na Feza, na sasa amerudi tena kwa Fahima. Hivyo basi, msishangae kesho mkimuona na mwanamke mwingine. Kwake yeye ni kiki na kubaki trending tu,” Paula alieleza.

Kulingana naye, mabadiliko ya mara kwa mara ya msanii huyo kati ya wanawake mbalimbali yalifanya iwe vigumu kujenga mustakabali thabiti wa pamoja.

Paula alitumia nafasi hiyo kuonya wanawake wanaotamani kuwa na uhusiano na watu mashuhuri kama Rayvanny kuchukua tahadhari.

“Wanawake wanapaswa kuchunguza tabia ya mwanaume kabla ya kuingia kwenye uhusiano. Kwa Rayvanny, mara nyingi huwa ana wanawake kadhaa kwa wakati mmoja,” aliongeza.

Kauli za Paula zilisambaa kwa kasi mitandaoni, zikizua mjadala mpana kuhusu changamoto za kuwa na uhusiano na wasanii wakubwa.

Wengi walihoji kama maisha ya umaarufu yanaweza kuendana na mahusiano ya kudumu, huku wengine wakiona kuwa tabia ya Rayvanny ni taswira ya changamoto zinazowakabili wanawake wengi wanaojaribu kujenga familia na wanaume maarufu.

What do youy think?

Continue Reading

Entertainment

Good Morning to All Dianas, Aandika Diana Yegon Baada ya Kauli ya Pastor Ezekiel

Published

on

Mwanahabari na mke wa Presenter Kai, Diana Yegon, ameibua gumzo mtandaoni baada ya kuandika ujumbe wa ucheshi uliolenga wanawake wote wanaoitwa Diana.

Kupitia ukurasa wake wa Facebook, Diana aliandika:

“Good morning to all ladies called Diana. Naskia sifa zetu nzuri nzuri sana. 😁”

Kauli hii imetafsiriwa na mashabiki wake kama jibu la kifahari na la utani kwa maneno ya Pastor Ezekiel, ambaye siku za hivi karibuni alizua mjadala mkubwa baada ya kudai kwamba wanawake wenye jina Diana ni wenye tabia zinazoweza kuvuruga ndoa.

Katika mahubiri yake, Pastor Ezekiel alisikika akisema:

“Ukioa mwanamke anaitwa Diana uishi na yeye, jua yeye ndiye ataku-control kama robot, ndiyo hiyo ndoa idumu… Yeye ndiye atakuwa husband, lakini wewe ukiwa mume, Diana hawezi dumu kwa ndoa… Pia jua ukioa Diana, lazima utashare na watu, sababu jina Diana imebeba mapepo… Hiyo ni ukweli mtupu!!!”

Kauli hii ilisambaa kwa kasi mitandaoni, huku ikiwasha mjadala mpana kuhusu imani, mitazamo ya kijamii na namna majina yanavyohusishwa na tabia za watu.

Badala ya kuingia kwenye malumbano, Diana aliamua kutumia uchemfu na ucheshi kujiweka mbali na mitazamo hiyo. Ujumbe wake wa “Good morning…” ulionekana kama njia ya: Kujipa nguvu na kuonyesha kujiamini kama mwanamke, Kuwatia moyo wanawake wote wanaoitwa Diana ambao huenda walihisi kushutumiwa na kauli ya mhubiri huyo, Kupunguza ukali wa mjadala kwa kutumia mzaha na mtindo wake wa kawaida wa kuchekesha mashabiki.

Mara baada ya posti hiyo, sehemu ya maoni ilijaa vicheko, pongezi na mijadala mikali. Wengi walimpongeza Diana kwa kuchukua hatua ya kugeuza maneno ya ukosoaji kuwa kicheko, wakisema kuwa huo ndio mfano wa kujua thamani yako bila kuyumbishwa na mitazamo ya nje.

Wengine walihoji uhalali wa kauli za kiroho zinazohusisha majina na tabia, wakisisitiza kuwa utu wa mtu hautokani na jina lake bali na malezi, maamuzi na imani.

Mjadala huu unaakisi hali halisi ya jamii ya sasa, ambapo mitazamo ya kidini, mila na maoni binafsi mara nyingi huibua tafsiri tofauti.
Kwa upande mmoja, kuna wale wanaoamini kabisa nguvu za majina, na kwa upande mwingine, kuna kizazi kipya kinachoona jina si kigezo cha utu wa mtu.

Kwa Diana Marua, kauli yake imezidi kuimarisha taswira yake kama msanii na mwanamke jasiri ambaye hajivunji moyo na maneno ya kukatisha tamaa.

Continue Reading

Trending