Sports
Uhispania Yaikomoa Ufaransa Uefa Nations Ligi.

UEFA NATIONS LEAGUE
Mabingwa watetezi wa taji la Uefa Nations Ligi Uhispania wameingia kwenye fainali ya taji hilo kwa kishindo Jumapili hii baada ya kunyuka Ufaransa magoli 5-4 hapo jana ugani Allianz Arena.
Winga matata wa Athletico Bilbao Nico Williams aliweka uongozini Uhispania dakika ya 22 kabila ya mshambulizi wa Arsenal Mikel Merino kuweka la pili dakika ya 25 kipindi cha kwanza.
La Furia Roja aliendeleza walipoachia kipindi cha kwanza katika kipindi cha pili huku winga wa Barcelona Lamine Yamal akiweka chuma ya tatu dakika ya 54,na lingine dakika ya 67 kabila ya Pedri kuweka la nne dakika ya 55 na kufanya mambo kuwa magoli 5-0
Hata hivyo Ufaransa walirejea kwa kishindo wakijipatia magoli kupitia Kyllian Mbappe dakika ya 59 naye Ryan Cherki dakika ya 79 Randal Kolo Muani dakika ya 93 uhispania pia wakijifunga kupitia beki Vivian.
Fainali ya Uefa Nations ligi ni kati ya Uhispania na Ureno jumapili saa nne usiku.
Sports
Harambee Stars Kuvaana Na Chad Mechi Ya Kirafiki.

Timu ya Taifa Harambee Stars chini ya kocha Benni Mccarthy kushuka dimbani majira saa kumi jioni Ugani Stade de Marrakech Morocco ikiwa ni mechi ya kirafiki.
Kwa mujibu wa mwalimu wa Stars Mccarthy mechi hizi ni muhimu kujenga kikosi kwa majukumu ya siku za usoni lakini pia kwa taji la Chan sawa na Afcon mwaka 2027.
“Ni muda mzuri mimi kufahamu vijana wangu na kuanza kuanda timu yenye ubora kwa minajili ya siku za usoni na wachezaji wa nyumabani watasaidia sana CHAN mwezi Agosti.”
Baada ya mechi hiyo Stars watacheza mechi nyingine na taifa hilo Juni 10.
Rais wa Fkf Hussein Mohammed amekariri kikosi hicho kitaelekea Uarabuni kwa maozezi kabambe kabila ya Chan humu nchini.
Sports
Kenya Pipeline Yaanza Kwa Kishindo Fainali Ya Voliboli

Kilabu ya Kenya Pipeline ilianza kwa kishindo fainali ya taji la akina dada mchezo wa voliboli mashidano yanayondelea uwanjani Kasarani Indoor Arena jijini Nairobi.
Hii ni baada ya vipusa hao chini ya kocha Godfrey Omondi kuwatandika wenzao DCI seti 3-0 mechi ya ufunguzi uwanja huo ukifurika hadi pomoni.
Kikosi hicho kilishinda mechi hiyo kwa seti 25-19,25-20,25-14 na kuibuka na ushindi huo mnono kabila ya mechi ya pili jumamosi.
Nahodha wa KPC Gladys Ereng amesema kwamba mechi haikua rahisi kwani DCI walikua vizuri ila walipambana kwa ushindi huo.
“DCI ni timu nzuri walicheza vizuri kipindi cha kwanza kwani tulianza kwa utepetevu ila tukazungumza na kujikusanya vyema na kupata ushindi huo muhimu kwetu.”
Kwa Upende wake kocha wa DCI Patrick Sang amedokeza kwamba hakucheza kwa umakinifu waliotarajia;”Hatukucheza kwa mipangilio yetu mazungumzo pamoja na utulivu haikuwepo lakini ndio hali ya mchezo nipongeze wenzetu.”
Kilabu ya General Service Unit (GSU) upande wa wanaume ilianza vema kusaka taji la upande wa Wanaume baada ya kushinda mechi ya mkondo kwanza sati 3-0 katika uwanja huo huo.
Hii ni baada ya kuwatandika Kenya Ports Authority (KPA) seti 3-0 za 25-15,25-22,30-28