Connect with us

News

Tahadhari Yatolewa Kuhusu Mvua Kubwa

Published

on

Idara ya utabiri wa hali ya hewa nchini imetoa tahadhari kwa wakenya kuhusu mvua kubwa itakayonyesha katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa kipindi cha siku saba.

Mkurugenzi wa idara ya hali ya hewa nchini, Dkt David Gikungu, amesema mvua hiyo itakayoambatana na ngurumo za radi inatarajiwa wakati wa alasiri na usiku, huku baadhi ya maeneo yakitarajiwa kupata mvua chache asubuhi kabla ya hali ya jua kuchomoza kwa muda mfupi.

Idara hiyo imesema viwango vya joto usiku katika maeneo haya vitashuka hadi chini ya nyuzi joto 9, hali inayoweza kuathiri watoto, wazee, na wagonjwa.

Kaunti za Siaya, Kisumu, Homa Bay, Migori, Kisii, Nyamira, Trans Nzoia, Baringo, Uasin Gishu, Elgeyo-Marakwet, Nandi, Nakuru, Narok, Kericho, Bomet, Kakamega, Vihiga, Bungoma, Busia, na Pokot Magharibi pia zimeorodhesha kati ya ya maeneo yanayotarajiwa kupokea mvua nyingi.

Hali kama hiyo inatarajiwa katika kaunti za Kitui, Makueni, Machakos, Kajiado, Taita Taveta, na sehemu za Tana River, ambako asubuhi kutakuwa na mawingu na mvua nyepesi kabla ya hali ya mvua kubwa kuanza alasiri na kuendelea hadi usiku.

Wakati mvua ikinyesha maeneo mengi ya kaunti za Mombasa, Kilifi, Lamu, Kwale, Marsabit, Mandera, Wajir, Garissa, na Isiolo yametabiriwa kupata joto nyakati za mchana hadi kufikia nyuzi joto 33.

Wataalamu wa hali ya hewa wamewahimiza wananchi kuwa waangalifu na kufuata ushauri wa serikali, hasa wale wanaoishi maeneo yenye historia ya mafuriko, maporomoko ya ardhi, na miundombinu dhaifu.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Kanisa Katoliki nchini lashinikiza maridhiano.

Published

on

By

Kanisa Katoliki nchini limeshinikiza serikali na vijana kuridhiana ili kuepuka vurugu zaidi zinazoshuhudiwa nchini.

Askofu mkuu wa kanisa katoliki Athony Muheria wa Nyeri na Phillip Anyolo wa Dayosisi ya Nairobi, waliitaka serikali kuhakikisha wanaoathirika kwenye Dhulma za maandamano wanafidiwa.

Viongozi hao wa dini walisema kunaumuhimu wa kuthamini maisha ya binadamu na kushinikiza viongozi wa siasa kuepuka kutoa semi za kuchukiza upande wowote Ule.

Matamshi ya viongozi hao yalijiri wakati vijana wa kizazi cha Gen Z, pamoja na mashirika ya kijamii wakiendelea na maandalizi ya maandamano ya kumbukumbu ya yaliyojiri juni tarehe 25 mwaka 2025, wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha.

Wakati wa maandamano hayo baadhi ya vijana waandamamanaji walipoteza maisha, wengine kuacha na majeraha na wengine kutekwa nyara na kupotezwa katika njia tatanishi

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

News

Seneta Madzayo amuonya Inspekta jenerali wa Polisi.

Published

on

By

Seneta wa kaunti ya Kilifi Stewart Madzayo amemtaka inspekta jenerali wa polisi nchini Douglas Kanja kuhakikisha maandamano ya vijana wa rika la Gen z tarehe 25 mwezi juni 2025 hayashuhudii umwagikaji damu.

Madzayo ambaye pia ni kiongozi wa wachache katika bunge la seneti alimtaka Inspekta Kanja kuhakikisha maafisa wa polisi wanawalinda waandamanaji badala ya kuwadhuru.

Akizungumza eneo la Mzambarauni-Mtwapa eneo bunge la Kilifi Kusini, Madzayo alidokeza kuwa maandamano hayo yatakuwa ya amani akikumbusha vijana hao wa Gen Z kuhakikisha wanadumisha amani wakati wa maandamano hayo.

“Tumeskia tarehe 25 kutakuwa na maandamano ya amani, nataka kumwambia inspekta jenerali Kanja, tafadhali watoto wetu watakuwa katika maandamano ya amani kwa hivyo usijaribu hata kidogo kutumia polisi vibaya kuweza kuumiza watoto wetu”, alisema Madzayo.

Kwa upande wake mbunge wa eneo hilo Ken Chonga aliwaomba viongozi wa kanisa nchini kuombea taifa kutokana na visa vya mauaji na utekeji nyara vinavyoshuhudiwa nchini.

“Tumekuwa na changamoto kubwa sana kati ya upinzani na serikali hali ya maafa ikiingia, haya yote ambayo yanaendelea sa hii yote sababu ni siasa, langu ni kusihi kwanza kanisa tunahitaji maombi yenu”, alisistiza Chonga.

Maandamano hayo ya GEN Z yanatarajiwa kufanyika tarehe 25 mwezi juni 2025 kukumbuka vijana waliopoteza maisha wakati wa maandamano ya kupinga mswada wa fedha mwezi juni mwaka 2024.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending