Connect with us

Sports

Stars Yaanza Vema Chan Kwa Ushindi Goli 1-0 Dhidi Ya DR.Congo

Published

on

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Timu Ya Taifa Ya DR Congo Yawasili Nchini Kwa Mechi Ya Ufunguzi Dhidi Ya Harambee Stars

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DR Congo) imewasili nchini mapema leo kwa ajili ya mechi ya ufunguzi dhidi ya Harambee Stars itakayochezwa siku ya Jumapili.

Kikosi hicho, kilicho na wachezaji 25 pamoja na benchi la kiufundi, kiliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) na kupokelewa rasmi kabla ya kuelekea hotelini jijini Nairobi.

DR Congo, maarufu kama The Leopards, ni mabingwa mara mbili wa kombe hilo na wanatarajiwa kufanya mazoezi yao ya kwanza jioni ya leo katika Uwanja wa Kasarani.

Vijana hao wako katika Kundi A pamoja na wenyeji Kenya, pamoja na AngolaMorocco, na Zambia.

Continue Reading

Sports

Waziri Wa Michezo Salim Mvurya Asema Kenya Iko Tayari Kwa CHAN

Published

on

By

SIKU 3 ZIMESALIA KUNGOA NANGA KOMBE LA CHAN:
Waziri wa Michezo, Salim Mvurya, pamoja na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya CHAN, Nicholas Musonye, wamefanya ukaguzi wa mwisho leo katika viwanja vya Kasarani na Nyayo kabla ya mechi ya ufunguzi kati ya Harambee Stars na DR Congo itakayochezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Kasarani.

Waziri Mvurya, akizungumza katika Uwanja wa Nyayo, amesema kuwa fursa hiyo ni ya kipekee kwa taifa na sekta ya michezo kwa ujumla, huku maandalizi ya kuelekea AFCON 2027 yakiendelea.

Aidha, Mvurya amewataka mashabiki kujitokeza kwa wingi kushangilia timu ya taifa, Harambee Stars, katika mechi ya Jumapili na michezo yote ya michuano hiyo.

Harambee Stars itacheza mechi zake zote katika Uwanja wa Kasarani. Timu hiyo imo katika Kundi A pamoja na Angola, Morocco, Zambia, na DR Congo.

Continue Reading

Trending