Connect with us

Sports

Stars Kambini Kwa Maandalizi Ya CHAN

Published

on

Timu ya Taifa ya soka Harambee Stars kimeingia kambini tayari kwa maandalizi ya Chan mwezi ujao katika mataifa ya Kenya,Uganda na Tanzania.

Vijana wa Nyumbani wamekaribishwa kambini na Waziri wa michezo Salim Mvurya na katibu mkuu Elija Mwangi na,rais wa Shirikisho la soka FKF Hussein Mohammed.

Stars itaendeleza mazoezi ugani Ulinzi Sports Complex chini ya kocha mkuu Benni MacCarthy ambaye amesema kwamba wako katika hali shwari,alipoulizwa kuhusu wachezaji wengine kukosana kikosini mwalimu huyo amedai kwamba hawezi akafurahisha kila mmoja wakati wa Uteuzi.

“Huwezi kumpendeza kila mtu,Sijakuja kufurahisha kila mtu ila malengo yake ni kuteua kikosi bora kwa ajili ya Taifa,Ni mimi ndiye kocha na nimetazama hawa wachezaji kwa hivyo lengo ni kunoa stars kuleta matokeo chanya timuni.”

Stars watakua kambini kabila ya kuelekea Tanzania kwa taji la CECAFA mataifa manne ;Kenya, Uganda,Tanzania na Sudan Kusini.

 

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Published

on

By

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Continue Reading

Sports

Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.
Continue Reading

Trending