Connect with us

Sports

Starlets Watambaa Dhidi Ya Crested Cranes Ya Uganda

Published

on

Timu ya Taifa ya soka akina dada Harambee Starlets imeendeleza ilipoachia mechi ya pili taji la CECAFA ukanda wa Afrika Mashariki baada ya kunyuka Crested Cranes ya Uganda kipigo cha magoli 4-0 mechi ya pili Ugani Azam Sports Complex mjini Dar es salaam Tanzania.

Kiungo wa kilabu ya Kenya Police Bullets Diana Wacera aliwaweka uongozini vipusa wa nyumbani kunako dakika ya 19,Huku nyae beki wa kimataifa Dorcas Shikhobe akiweka kambani goli la pili kunako dakika ya 27,mshambulizi wa kimataifa Violet Wanyonyi Nanjala akifunga goli la tatu dakika ya 29 naye kiungo wa kilabu ya Vihiga Queens Martha Amunyolet akifunga goli la nne na la mwisho dakika ya 81 kipindi cha pili.

Huu ukiwa ni ushindi wa pili kwa timu hiyo chini ya kocha Beldine Odemba katika mechi ya kwanza walishinda Burundi magoli 3-0 siku ya Jumapili.

Katika mechi nyingine Twiga Stars ya tanzania walirindima Burundi magoli 6-0 katika uga uo huo.Kituo kinachofuata kwa Starlets ni dhidi ya Sudan Kusini Alhamisi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Kilabu Ya Kenya Police Mabingwa Ligi Kuu FKF PL

Published

on

By

Timu ya Kenya Police FC imetawazwa mabingwa wa Ligi Kuu ya FKF kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwake, katika mechi ya mwisho dhidi ya Gor Mahia iliyopigwa kwenye Uwanja wa Ulinzi Sports Complex, .

Mabingwa hao wapya walionesha ari ya kupigania hadi dakika ya mwisho, wakitoka nyuma na kupata sare ya 1–1 dhidi ya Gor Mahia waliokuwa nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.
katika matokeo mengine jana:

AFC Leopards  0-0 KCB,BANDARI 1-1 POSTA,KAKAMEGA HOMEBOYZ 0-0 TUSKER,KSHARKS 4-1 MARA SUGAR,SHABANA 1-1 ULINZI STARS,MURNGA 1-0TALANTA,Shabana 1-1 Ulinzi Stars,Nairobi City Stars 0-0 Mathare United ,Sofapaka 1-2 Bidco United.

Vilabu vya Niarobi City Stars na Talanta vimeteremshwa ngazi huku Posta Rangers ikimaliza nafasi ya 16 na sasa italazimika kucheza mechi ya mchujo dhidi ya timu ya tatu ya ligi ya daraja ya pili NSL.

Continue Reading

Sports

Liverpool Yakubaliana Dili Ya Kerkez

Published

on

By

Kilabu ya Liverpool imekubaliana na AFC Bournemouth kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 4o kwa beki Milos Kerkez raia wa Serbia.

Tineja huyo anatarajiwa kuwasili Liverpool muda wowote kufanyiwa vipimo vya kimatibabu na kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa ligi kuu Uingereza.

Mchezaji huyo alikua nguzo muhimu kwa kilabu ya Bournemouth wakimaliza kumi bora akichangia magoli matano na kufunga mawili,anakua sajili wa tatu kwa kocha Arne Slot kwenye kilabu hio.

The Reds wakiwa wametumia pauni milioni 116 kumpata kiungo Florian Wirtz,pauni milioni 31 kupata Jeremie Frimpong.

Continue Reading

Trending