Connect with us

Sports

Starlets Watambaa Dhidi Ya Crested Cranes Ya Uganda

Published

on

Timu ya Taifa ya soka akina dada Harambee Starlets imeendeleza ilipoachia mechi ya pili taji la CECAFA ukanda wa Afrika Mashariki baada ya kunyuka Crested Cranes ya Uganda kipigo cha magoli 4-0 mechi ya pili Ugani Azam Sports Complex mjini Dar es salaam Tanzania.

Kiungo wa kilabu ya Kenya Police Bullets Diana Wacera aliwaweka uongozini vipusa wa nyumbani kunako dakika ya 19,Huku nyae beki wa kimataifa Dorcas Shikhobe akiweka kambani goli la pili kunako dakika ya 27,mshambulizi wa kimataifa Violet Wanyonyi Nanjala akifunga goli la tatu dakika ya 29 naye kiungo wa kilabu ya Vihiga Queens Martha Amunyolet akifunga goli la nne na la mwisho dakika ya 81 kipindi cha pili.

Huu ukiwa ni ushindi wa pili kwa timu hiyo chini ya kocha Beldine Odemba katika mechi ya kwanza walishinda Burundi magoli 3-0 siku ya Jumapili.

Katika mechi nyingine Twiga Stars ya tanzania walirindima Burundi magoli 6-0 katika uga uo huo.Kituo kinachofuata kwa Starlets ni dhidi ya Sudan Kusini Alhamisi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Liverpool Yakubaliana Dili Ya Kerkez

Published

on

By

Kilabu ya Liverpool imekubaliana na AFC Bournemouth kuhusiana na uhamisho wa pauni milioni 4o kwa beki Milos Kerkez raia wa Serbia.

Tineja huyo anatarajiwa kuwasili Liverpool muda wowote kufanyiwa vipimo vya kimatibabu na kumwaga wino mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa ligi kuu Uingereza.

Mchezaji huyo alikua nguzo muhimu kwa kilabu ya Bournemouth wakimaliza kumi bora akichangia magoli matano na kufunga mawili,anakua sajili wa tatu kwa kocha Arne Slot kwenye kilabu hio.

The Reds wakiwa wametumia pauni milioni 116 kumpata kiungo Florian Wirtz,pauni milioni 31 kupata Jeremie Frimpong.

Continue Reading

Sports

Starlets Kucheza Fainali Ya CECAFA Dhidi Tanzania

Published

on

By

Kikosi cha soka akina dada kushuka dimbani kucheza dhidi ya Twiga Stars Ya Tanzania kwenye fainali ya kipute cha CECAFA Afrika Mashariki ugani Azam Sports Complex.

Vipusa wa kocha Beldine Odemba wameshinda mechi zote tatu ikiwemo kuwalaza Sudan Kusini magoli 4-0 mechi ya siku ya Alhamisi huku wakiwa wamekusanya alama 9 sawa na wenyeji Tanzania kwenye mashindano ya mwaka huu.

kwa mujibu wa mwalimu huyo wanatarajia mechi ngumu dhidi ya wapinzani wao kwani wako nyumbani na timu bora pia.

“Tuko tayari kwa mechi ya mwisho ambayo pia ni fainali kila mmoja anajua tumekua vizuri katika mashindano haya ila Tanzania ni mpinzani mkubwa katika fainali ya leo kwa sababu pia hawajapoteza mechi kama sisi.”

Mechi hiyo inangoa nanga saa 12.00 jioni.

Continue Reading

Trending