Connect with us

Entertainment

Sikutaka Pesa, Nilitaka Furaha – Bango Likaleta Vyote, Manu Bayaz

Published

on

Afisa wa polisi ambaye pia ni muimbaji wa muziki wa Bango, Emmanuel Yaa Baya anayejulikana zaidi kwa jina la kisanii Manu Bayaz, amefichua kilichomsukuma kuingia kwenye muziki wa Bango.

Akihojiwa na Coco FM katika kipindi cha Coco Asubuhi, Bayaz alisema kwamba hajaanza muziki kwa ajili ya kutafuta pesa, bali alitaka kujifurahisha tu. Hata hivyo, nyimbo zake zilianza kuvutia watu wengi na kumpatia umaarufu mkubwa miongoni mwa mashabiki wa muziki wa Bango wengine wakiitisha huduma zake kwenye sherehe zao.

“Hapo awali haikuwa kwa ajili ya pesa. Nilianza kwa kujifurahisha, lakini watu wakaanza kupenda nyimbo zangu,” alisema Bayaz.

Kutokana na mafanikio hayo, Bayaz aliamua kubadili mtazamo na kuanza kuwekeza zaidi kibiashara kwenye muziki huo.

Akiendelea kuelezea safari yake ya muziki, alitaja changamoto kubwa aliyokumbana nayo kuwa ni kudhibiti kundi la wanamuziki, akisisitiza ugumu wa kuwaunganisha watu wenye malezi na mitazamo tofauti katika kundi moja.

“Kwenye bendi, kila mtu ametoka mazingira tofauti, amekuzwa kivyake. Kuwaunganisha watu kama kumi si jambo rahisi, lakini tunajitahidi,” alisema.

Bayaz analikumbuka kwa furaha tukio la malipo yake ya kwanza katika muziki wa Bango.

“Malipo yangu ya kwanza ndiyo experience nayoikumbuka maisha yangu ya mziki. Nililipwa shilingi elfu hamsini za Kenya (KSh 50,000), Mtu wa kwanza kumtaarifu habari hii  ni babangu,” alisimulia.

Alieleza pia kuwa mapenzi yake ya muda mrefu kwa muziki wa Rhumba ndiyo yaliyomsukuma kuimba Bango, akieleza kuwa Bango ni aina ya Rhumba yenye ladha ya Pwani.

“Mimi napenda sana Rhumba. Nilivyoanza kuimba nikaona niende kwenye hiyo njia. Bango ni Rhumba tu, ila lina ladha ya Kipwani.”

Bayaz alianza kuimba akiwa na Sumilani Band na baadaye Ministers Band. Hata hivyo, aliachana na Sumilani baada ya kutofautiana kuhusu jina jipya alilopendekeza kwa bendi hiyo.

Bayaz pia alieleza kuwa alinunua vyombo vyake vya muziki kutoka China ili kuimarisha safari yake ya muziki, huku akiendelea kufanya kazi na bendi ya Sumilani kabla ya kuondoka.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Published

on

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.

Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”

Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.

Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.

Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.

Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.

Continue Reading

Entertainment

Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Published

on

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.

“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.

“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”

Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”

Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.

“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.

Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.

“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.

Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;

Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”

Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule 😁.”

D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya 🇰🇪.”

Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”

Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”

Continue Reading

Trending