Connect with us

News

Serikali yashinikizwa kukabili ajira za utotoni.

Published

on

Maafisa wa idara inayoshughulikia maslahi ya watoto kaunti ya Kilifi wameshinikiza serikali kuu na zile za kaunti kuweka mikakati dhabiti ili kukabili suala la ajira za utotoni.

Wakiongozwa na Kevin Mugambi afisa wa idara ya watoto eneo la Kauma alitaja suala la umaskini kama chanzo kikuu cha watoto kushiriki aina hiyo ya ajira.

Akizungumza katika kipindi cha Coco asubuhi, Mugambi alisema raslimali zaidi zinafaa kuekezwa hasa katika mgao wa bajeti ya kitaifa utakaoelekezwa katika idara hiyo.

Kwa upande wake Omar Mohammed Afisa wa watoto eneo bunge la Ganze alionya wazazi kuepuka kuajiri watoto walio chini ya umri wa miaka 18, akisema watakabiliwa kisheria iwapo watapatikana.

“Kama wewe labda ni muajiri pahali popote ulipo na umeweza kuchukua mtoto ama mtu chini ya umri wa miaka 18 hiyo unaweza kushtakiwa, kwa hivyo kitu kizuri cha kufanya ni kwamba kama mtu hana kitambulisho cha kenya basi usimuajiri kwa sababu huyo ni mtoto na ikipatikana hiyo ni ajira ya utotoni”, Alisema Omar.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Wakaazi wa Voi waonywa dhidi ya ugonjwa wa MPOX

Published

on

By

Daktari wa magonjwa ya kuambukiza katika hospitali ya rufaa ya Moi mjini Voi katika kaunti ya Taita Taveta Urbanius Kioko amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kuzingatia maagizo ya Wizara ya Afya ili kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Akiongea kwenye warsha ya Wanahabari iliyofadhiliwa na Shirika la Stawisha Pwani, Daktari Kioko alisema wananchi wanapaswa kujikinga ili kudhibiti ugonjwa huo kuenea.

Kioko pia aliwataka wale ambao wana dalili za ugonjwa huo kufika kwenye vituo vya afya ili kutibiwa.

“Huu ugonjwa huwa unaenezwa kupitia kutangamana, kuvaa nguo za mwenzako na kupitia hewa wakati wa kuongea’’, alisema Kioko.

Wadau wa sekta ya Afya katika kikao na Wanahabari mjini Voi

Vilevile, Kioko alitaja kisa cha mgonjwa mmoja wa Mpox kilichothibitishwa siku ya Jumanne wiki hii mjini Voi huku visa vingi vikishamiri katika kaunti Mombasa.

Haya yanajiri huku Wizara ya Afya nchini ikishinikiza wananchi kujiepusha kula nyama za Wanyamapori miongoni mwa tahadhari zingine kama njia mojawapo ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Mpox.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mzozo kati ya Kenye na Tanzania waendelea kutokota

Published

on

By

Serikali ya Kenya imeiandikia barua jumuiya ya afrika mashariki kupinga vikwazo vilivyowekwa na Tanzania kuhusu kufanya biashara katika taifa hilo.

Katibu mkuu katika idara ya EAC Daktari Caroline Karugu, alisema kenya imebaini kuwa agizo hilo haliambatani kamwe na masharti muhimu ya itifaki ya soko la pamoja la EAC, ambayo inahakikisha uruhu wa watu kusafiri, kuhudumu na haki ya kuanzishwa kwa biashara na raia wa mataifa ya afrika mashariki.

Aidha Kenya iliasema imeandika rasmi barua kwa EAC kuiarifu rasmi jamhuri ya muungano wa Tanzania kuangazia upya agizo hilo ili kuhakikisha inafuata kikamilifu mkataba wa EAC na sheria za Jumuia.

Maafisa wa EAC kwa sasa wanafanya uchambuzi wa hatua hiyo na itawasilisha hatua zozote zilizokiukwa pamoja na kaununi zilizopo katika mkutano ujao wa baraza la kisekta la biashara, viwanda na uekezaji.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending