Connect with us

News

Serikali kuwalipia wakenya milioni 1.5 gharama za SHA

Published

on

Serikali inasema itawalipia wakenya milioni 1.5 matozo ya bima ya afya – SHA kuanzia wiki ijayo.

Haya ni kwa mujibu wa rais William Ruto ambaye alisema kuwa watakaofaidika na mpango huo ni wale ambao hawana uwezo wa kulipia bima ya afya SHA.

Aidha rais Ruto alisema atafanya mkutano na magavana na wabunge ili wao pia wawalipie pesa hizo wakenya wengine milioni moja.

Kiongozi wa taifa aliongeza kwamba hatua hiyo inalenga kuwawezesha wakenya wote kupata matibabu bila malipo.

Wakati huo huo serikali iliahirisha mpango wa kuwahamisha zaidi ya wafanyakazi 7,400 wa huduma za afya kwa wote (UHC) hadi mwaka ujao 2026.

Aidha wizara ya afya itaendelea kuwalipa mishahara wahudumu hao katika muda huo ambapo watakuwa kwenye mpango wa ajira ya kudumu na yenye pensheni hadi mwezi Juni mwaka ujao.

Haya yameafikiwa baada ya mazungumzo ya kina kati ya waziri wa afya Aden Duale na baraza la magavana.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending