Connect with us

Sports

Senegal Wako Tayari Kutetea Ubingwa Asema Kocha Diallo

Published

on

SENEGAL

SENEGAL-Wanajiita The Lions of Teranga kwa jina la Utani.

Ni mabingwa watetezi wa kombe la CHAN wakishinda kombe hilo na lao la pekee mwaka 2022 mjini Algiers Aljeria.

Kocha mkuu wa kikosi hicho ni Pape Thiaw ila majukumu ya kipute cha CHAN yamepewa aliyekua mchezaji wa taifa hilo Souleymane Diallo kuongoza vijana hao akiwa pia amenoa kikosi cha vijana chipukizi wasiozidi umri wa miaka 20.

mkufunzi huyo amesema lengo lao kuu ni kutetea ubingwa wa taji hilo kwani wana kikosi bora na wamejipanga vilivyo.

“Sisi ni mabingwa na tunakuja kutetea ubingwa wetu katika kombe la CHAN mwaka huu tuna kikosi chipukizi na nina amini wako tayari kwa changamoto yoyote ile.”

Vijana hao waliadhibu Taifa la Liberia magoli 3-0 nyumbani kabila ya kutoka sare ya goli 1-1 mechi ya marudio na kujikatia tiketi hiyo.

Wachezaji nyota wakuangaziwa katika kikosi cha The Lions of Teranga ni pamoja na mshambulizi Oumar Bar anayekipiga na kilabu ya US Goree ya taifa hilo mwingine ni kiungo Baye Assane Ciss miongoni mwa wengine.

Timu hiyo inajivunia nyota Lamine Camara ambaye alingaa mwaka 2022 na sasa anapiga na Monaco ya Ufaransa baada ya kupata ufanisi mkubwa.

Senegal wako kundi D pamoja na mataifa ya Congo,Sudan na Nigeria.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Tuko Tayari Kwa CHAN Asema Kocha Wa Angola-Pedro

Published

on

By

SIKU 9 KUNGOA NANGA KWA CHAN
ANGOLA-Mabingwa wa Taji La COSAFA.
Wanajiita The Black Antelopes kwa jina la utani ila bado hawajashinda kombe la CHAN katika historia yao.
Taifa hilo limeshiriki kombe hilo miaka minne ikiwa ni miaka ya  (2011, 2016, 2018, 2022) zote wakiambulia patupu.
Kocha mkuu wa timu hiyo ya taifa anaitwa Pedro Gonçalves ambaye ameongoza timu za taifa hilo kuanzia kwa vikosi chipukizi wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17 taji la AFCON NA COSAFA ya chipukizi kabila ya kuongoza taifa hilo kushinda kombe la COSAFA wakishinda Afrika Kuisini magoli 3-0 kwenye fainali mwezi jana.
Akizungumza kabila ya timu hiyo kuwasili jijini Nairobi mwalimu huyo amesema lengo lao ni kuendeleza walipoachia ; “Tumefanya vizuri sana Cosafa na sasa lengo letu kushinda Chan pia nina kikosi ambacho kiko tayari na tutafanya kila kitu kuibuka washindi.”
Mwalimu huyo pia ameongoza taifa lake katika kombe la AFCON mwaka 2024 wakitolewa kwenye robo fainali nchini Ivory Coast.
The Sable Antelopes ilimaliza nafasi ya nne taji la Chan katika fainali ya mwaka 2011 nchini Sudan.
Badhi ya wachezaji wa kuangaziwa katika kikosi cha vijana hao ni pamoja na ;mshambulizi Jó Paciência wa kilabu ya Bravos do Maquis nchini humo mabeki Eddie Afonso na Hossi.
Mabingwa hao wa COSAFA wako kundi A pamoja na Kenya,Morocco,DR.Congo na Zambia.
Continue Reading

Sports

Finali Ya Euro Ya Akina Dada Ni Kati Ya Uhispania Na Uingereza Jumapili

Published

on

By

Timu ya Taifa ya Wanawake ya Uhispania imetinga fainali ya kombe la Mataifa ya Ulaya kwa Wanawake mwaka 2025, WEURO 2025 kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Ujerumani katika dimba la Letzigrund mjini, Zürich kwenye nusu fainali.

Timu zote mbili zilikosa nafasi kochokocho za kufunga katika mchezo huo huku Uhispania wakilenga zaidi ya mashuti 10 langoni ila haikuzaa matunda katika dakika 90 za mchezo.

Mchezo huo ulilazimika kuamuliwa kwenye muda wa ziada ambapo mshambulizi wa Barcelona Aitana Bonmati alifunga goli la kipekee dakika ya 113 baada ya dakika 90 kumalizika bila bao.
Uhispania itachuana na Mabingwa watetezi, England kwenye fainali siku ya Jumapili.
England waliwabandua Italia magoli 2-1 katika nusu fainali ya kwanza siku ya Jumanne.
Continue Reading

Trending