Entertainment
Self Love!!? Mulamwah Ajizawidi Gari la Kifahari Kusherehekea Siku ya Mazazi

Mchekeshaji na mtangazaji wa redio, David Oyando, maarufu kama Mulamwah, ameadhimisha siku ya mazazi kwa kujizawidi gari la kifahari aina ya Mercedes Benz S550.
Msanii huyo anayependwa kwa ucheshi wake wa kipekee unaochambua maisha ya kila siku, alitumia mitandao ya kijamii kuonyesha hadharani zawadi hiyo ya kipekee aliyojipa kwa siku yake ya kuzaliwa.
“Na kwa zawadi yangu ya birthday… kutoka E-Class Benz hadi Mercedes Benz S-550 ya kisasa, injini ya 4.8L V8 Bi-Turbo,” aliandika Mulamwah huku akiwapa mashabiki wake taswira ya gari hilo jeusi kutoka Ujerumani.
Katika mazungumzo ya wazi, mtangazaji alifichua kuwa fedha alizotumia kununua gari hilo hapo awali zilikuwa zimekusudiwa kugharamia harusi yake na mchumba wake wa zamani, Ruth K.
Hata hivyo, baada ya mahusiano yao kuvunjika, aliamua kutumia akiba hiyo kutimiza ndoto yake ya muda mrefu.
“Nilitumia pesa nilizokuwa nimewekeza kwa ajili ya harusi—lakini mambo hayaendi kama vile unapanga—kulinunua,” alikiri, akitoa mwanga kuhusu mabadiliko ya kihemko na kifedha aliyopitia.
Kupitia chapisho lenye tafakari ya kina, Mulamwah alitumia tukio hilo kuwatia moyo mashabiki wake kwa ujumbe wa matumaini:
“Kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Kama kawaida, songa taratibu, songa kwa usahihi. Hata kama watu hawakuamini, wewe jiamini daima.”
Aidha, hakusita kuwashukuru mashabiki wake pamoja na washirika wa kibiashara waliomsaidia kufika alipo:
“Kwa mashabiki wangu na brandi zote, asanteni sana kwa kuniamini na kunisukuma kuendelea mbele,” aliongeza kwa shukrani.
Mulamwah amejiimarisha kama jina maarufu katika tasnia ya burudani nchini Kenya kupitia vichekesho vyake vinavyosambaa kwa kasi mitandaoni, ambavyo vimejikita kwenye maisha halisi ya Wakenya, pamoja na kazi yake ya utangazaji redioni.
Mchanganyiko wa ucheshi, uhalisia na msimamo wake thabiti umemjengea msingi wa mashabiki waaminifu, sambamba na nafasi ya kushirikiana na bidhaa mbalimbali zinazomhusudu kibiashara.
Licha ya kupitia vipindi vya misukosuko—ikiwemo kuvunjika kwa mahusiano na vuta nikuvute mitandaoni—Mulamwah amesalia imara katika utengenezaji wa maudhui na kukuza maisha yake binafsi.
Kuanzia uigizaji jukwaani, uendeshaji vipindi redioni hadi usimamizi wa chapa yake mitandaoni, ameendelea kukua kama msanii mwenye vipaji vingi na ushawishi mpana.
Entertainment
Penzi Lao Lazaa Matunda: Jux na Priscilla Watarajia Mwana

Binti wa mwigizaji mashuhuri wa Nollywood, Iyabo Ojo, ambaye ni Priscilla Ojo, na mumewe, nyota wa muziki kutoka Tanzania Juma Jux, wametangaza kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza.
Wapenzi hao walishiriki habari hizo njema kupitia mtandao wa Instagram kwa picha maridadi za ujauzito, ambapo Priscilla alionekana akionyesha tumbo lake la ujauzito. Picha hizo zilifuatana na maandishi mafupi: “Mum & Dad.”
Safari ya kimapenzi ya wawili hao imekuwa ikifuatiliwa kwa karibu, ikijumuisha harusi kadhaa zilizofanyika nchini Nigeria na Tanzania, hatua ambayo iliangazia muunganiko wa tamaduni zao mbili.
Juma Jux alimvisha pete ya uchumba Priscilla mara mbili, ambapo ombi la pili lilikuwa la kipekee na lisilosahaulika, lililofanyika jijini Lagos, Nigeria.
Wapenzi hao waliadhimisha safari yao ya ndoa kwa sherehe mbalimbali, zikiwemo harusi ya kitamaduni ya Kiyoruba, harusi ya kanisani (white wedding), na sherehe nyingine zilizoandaliwa kwa fahari kubwa mnamo Aprili 17 na 19, zote zikiwa jijini Lagos.
Kadiri wanavyojiandaa kwa ujio wa mtoto wao wa kwanza, pongezi na salamu za heri kutoka kwa mashabiki na jamaa zimekuwa zikitiririka kwa wingi.
Entertainment
Lisemwalo Lipo, Apewe Nafasi Afunguke, Kaa la Moto Amkingia Kifua Kelechi Africana

Msanii nguli wa muziki Afrika Mashariki, Kaa la Moto, amekingia kifua kauli ya msanii mwenzake Kelechi Africana aliyedai kuwa “kinachowafelisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”
Akizungumza na meza ya burudani ya Coco FM, Kaa la Moto alieleza kuwa anaamini nia ya Kelechi si ya kubeza bali ya kutaka kuona mabadiliko chanya kwenye tasnia ya muziki kutoka ukanda wa Pwani.
“Ameona ndio maana anayakemea,” alisema Kaa la Moto kwa utulivu.
“Naamini kwamba ana ufahamu sahihi, na pia naamini kuwa ni kijana ambaye anataka maendeleo ya sanaa kutoka mkoa wake. Kwa hiyo watu walipatie fikra—kwa sababu lisemwalo lipo. Labda ana kitu, akipewa nafasi atazungumza zaidi.”
Kauli ya Kelechi ilizua hisia mseto mitandaoni baada ya kupachikwa kwenye ukurasa wake wa Facebook, ambapo aliandika: “Kinacho felisha wanamuziki wa Mombasa ni ukahaba.”
Wengine waliona ni matusi kwa jumuiya ya wasanii, lakini kwa Kaa la Moto, ilikuwa ni hoja yenye mzizi wa ukweli. Alisisitiza kuwa hakuna hoja inayopaswa kupuuzwa kabla ya kueleweka kwa undani.
“Sipingi hoja yake kwa sababu kila hoja ipo huru kwa aliyeifikiria na kuiwaza. Naamini anajaribu kuinspire vijana wenzake,” aliongeza Kelechi.
Katika mazungumzo hayo, Kaa la Moto pia alitumia fursa hiyo kueleza kinachomuweka relevant kwenye muziki licha ya mabadiliko ya ladha, mitindo, na majina mapya kwenye game kila mwaka.
“Kitu ambacho kimeniweka hadi leo ni nidhamu. Nidhamu kwenye maisha, kwenye kazi, kwenye watu,” alisema kwa msisitizo.
Baadhi ya mashabiki waliopena maoni yao kwenye post ya Kelechi walisema;
Tamara Black, “Shida tu unaingililia watu hawana shughuli yako.Put that effort in Use ututolee kazi kali umbea achia watoto wa kike.”
Raisi Wakitaa, “Apo umenena nimepata mwenzangu sasa wakusema ukweli wanaboesha Sana Kwanza uyo my wife ndo kabisa simuelewi kila siku post ya mtu mmoja demu mwenyewe alishaliwa na wahuni toka enzi za shule .”
D Jay Ricious,”Wapashe adi wagutuke maana tulio chini ni huko juu ndio twaja kwa nafasi zetu. #coast music occupy kenya .”
Hamza Ahmed Lama, “Acha kutafuta Kiki’kai anapiga hela na anamadili kibao.”
Knasty Snaty, “Wew nawew wataka dera kazi yako ni umbea tu acha mziki uanze umbea.”