Entertainment
Self Love!!? Mulamwah Ajizawidi Gari la Kifahari Kusherehekea Siku ya Mazazi

Mchekeshaji na mtangazaji wa redio, David Oyando, maarufu kama Mulamwah, ameadhimisha siku ya mazazi kwa kujizawidi gari la kifahari aina ya Mercedes Benz S550.
Msanii huyo anayependwa kwa ucheshi wake wa kipekee unaochambua maisha ya kila siku, alitumia mitandao ya kijamii kuonyesha hadharani zawadi hiyo ya kipekee aliyojipa kwa siku yake ya kuzaliwa.
“Na kwa zawadi yangu ya birthday… kutoka E-Class Benz hadi Mercedes Benz S-550 ya kisasa, injini ya 4.8L V8 Bi-Turbo,” aliandika Mulamwah huku akiwapa mashabiki wake taswira ya gari hilo jeusi kutoka Ujerumani.
Katika mazungumzo ya wazi, mtangazaji alifichua kuwa fedha alizotumia kununua gari hilo hapo awali zilikuwa zimekusudiwa kugharamia harusi yake na mchumba wake wa zamani, Ruth K.
Hata hivyo, baada ya mahusiano yao kuvunjika, aliamua kutumia akiba hiyo kutimiza ndoto yake ya muda mrefu.
“Nilitumia pesa nilizokuwa nimewekeza kwa ajili ya harusi—lakini mambo hayaendi kama vile unapanga—kulinunua,” alikiri, akitoa mwanga kuhusu mabadiliko ya kihemko na kifedha aliyopitia.
Kupitia chapisho lenye tafakari ya kina, Mulamwah alitumia tukio hilo kuwatia moyo mashabiki wake kwa ujumbe wa matumaini:
“Kwa Mungu hakuna lisilowezekana. Kama kawaida, songa taratibu, songa kwa usahihi. Hata kama watu hawakuamini, wewe jiamini daima.”
Aidha, hakusita kuwashukuru mashabiki wake pamoja na washirika wa kibiashara waliomsaidia kufika alipo:
“Kwa mashabiki wangu na brandi zote, asanteni sana kwa kuniamini na kunisukuma kuendelea mbele,” aliongeza kwa shukrani.
Mulamwah amejiimarisha kama jina maarufu katika tasnia ya burudani nchini Kenya kupitia vichekesho vyake vinavyosambaa kwa kasi mitandaoni, ambavyo vimejikita kwenye maisha halisi ya Wakenya, pamoja na kazi yake ya utangazaji redioni.
Mchanganyiko wa ucheshi, uhalisia na msimamo wake thabiti umemjengea msingi wa mashabiki waaminifu, sambamba na nafasi ya kushirikiana na bidhaa mbalimbali zinazomhusudu kibiashara.
Licha ya kupitia vipindi vya misukosuko—ikiwemo kuvunjika kwa mahusiano na vuta nikuvute mitandaoni—Mulamwah amesalia imara katika utengenezaji wa maudhui na kukuza maisha yake binafsi.
Kuanzia uigizaji jukwaani, uendeshaji vipindi redioni hadi usimamizi wa chapa yake mitandaoni, ameendelea kukua kama msanii mwenye vipaji vingi na ushawishi mpana.
Entertainment
Joy to The World! Mke wa Michael Yena, Grace Santa, Ajifungua
Mwimbaji wa Injili Michael Yena na mkewe Grace Santa wamebarikiwa na mtoto wao wa kwanza. Jua zaidi kuhusu ujio huu wa neema na wimbo mpya ‘Ametutendea’ unaosindikiza tukio hilo la kipekee!

Ni shangwe! Ni nderemo! Ni vigelegele! Baraka kubwa imetua rasmi kwenye familia changa ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Michael Yena, baada ya mkewe kipenzi Grace Santa kujifungua mtoto wao wa kwanza! 🍼👶
Kupitia ukurasa wake rasmi wa Facebook, Yena alipakia picha na tulipomtafuta mda mchache uliopita akathibitisha habari hiyo njema.
Kwenye Facebook, Yena, aliandika:
“We give God all the Glory. #Ametutendea”
Lakini subiri kidogo! Ikiwa unataka kujua mtoto ni wa kike au wa kiume… tafadhali kaa mkao wa kusubiri 😅. Kulotia maongezi ya njia ya simu, Yena amesema, kwa sasa jinsia ya mtoto itabaki kuwa “fiche”, wakisubiri wakati maalum wa kufanya tangazo rasmi. Hii ni kama suspense ya movie nzuri—yaani hata mtoto wao anaingia duniani na style! 🎬✨
🎶 Wimbo Mpya Wenye Maana Kubwa: “Ametutendea”
Katika kusindikiza ujio wa mtoto wao, Michael Yena ameendelea kusukuma wimbo wake mpya “Ametutendea”—na kwa kweli, jina la wimbo linazungumza moja kwa moja na tukio la maisha yao. Ni ushuhuda wao.
👉 Tazama video ya wimbo huo hapa:
🔗 Ametutendea – Michael Yena (Official Video)
Wimbo huu ni wimbo wa ushuhuda, wa shukrani, na wa imani. Ukiusikiliza huku ukijua kuwa umetoka kwa mtu ambaye ameonja wema wa Mungu kwa kiwango hiki—huwezi kubaki vilevile!
💍 Safari ya Upendo Yao
Kwa wanaofuatilia historia yao ya kimapenzi na kiroho, Michael na Grace walifunga ndoa yao mwezi Aprili mwaka 2024. Kwa kipindi kifupi, wameonyesha mfano wa ndoa yenye msingi wa maombi, heshima na maelewano. Na sasa, wameingia katika ukurasa mpya wa maisha—ukurasa wa uzazi!
Tunawatakia kila la kheri katika safari yao ya kuwa wazazi. Dunia imepata mtoto mwingine wa neema, na hakika tunaamini huyu naye atakuwa baraka kwa vizazi. Kama ilivyo kwa mashairi ya wimbo wao mpya, tunaungana nao kusema kwa nguvu zote:
“AMETUTENDEA!” 🎉
📌 Endelea kutembelea www.cocomedia.co.ke kwa habari za utendeti, matukio ya kusisimua, habari na kila kinachohusu burudani.
Entertainment
Creative Economy Forum 2025: Ruby Kache Uso kwa Uso na Bien
Ruby Kache na Bien wakutana Nairobi kwenye Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu! 🌟

Jiji la Nairobi liling’aa zaidi wiki hii baada ya kuandaa Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu — tukio la kipekee lililowakutanisha wabunifu, wanamuziki, na wadau wa sanaa kutoka Kenya na Marekani. Mbali na mijadala ya sera na mipango ya maendeleo, tukio hili lilikutanisha watu mashuhuri.
Mrembo wa redio, Ruby Kache, alikutana na nyota wa muziki, Bien aliyekuwa kwenye kundi la maarufu Sauti Sol!
Kwa wanaosikiliza redio, jina la Ruby Kache si geni. Ni mtangazaji machachari wa kipindi cha “The Wave” kupitia Coco FM, kinachoenda hewani kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana. Kipindi chake kinajulikana kwa kuangazia maisha ya vijana, muziki wa kisasa, mitindo na mazungumzo yenye msisimko.
Katika kongamano hili, Ruby alihudhuria kama mshiriki, lakini kama ilivyo kawaida yake — aliiba spotlight bila kusema neno jukwaani. Uvaaji wake, tabasamu lake na muingiliano wake na wadau wengine ulitosha kuonyesha uwepo wake wa nguvu.
Moja ya highlights kubwa za siku hii ilikuwa ni wakati Ruby Kache alipokutana na Bien. Ruby alirekodi kipande kifupi na kukipakia kwenye ukurasa wake wa Facebook, huku mashabiki wakishangilia. Bien, nguli wa mziki anayeshikilia tuzo ya muimbaji bora Afrika Mashariki, alikuwa mgeni maarufu katika tukio hilo.
Baadhi ya waunda maudhui maarufu kutoka Pwani waliopamba hafla hiyo ni pamoja na Presenter Kai, Beka Ruga, Mwagwaya Ndani, na Princess Fynick, waliokuja kwa mitoko ya kisasa. Kwa upande wa muziki, Reagan Dandy alikuwa miongoni mwa wanamuziki wachache kutoka Pwani waliobahatika kuhudhuria tukio hilo la hadhi ya kimataifa.
Jukwaa la Uchumi wa Ubunifu limeibuka kama jukwaa muhimu kwa kuvunja mipaka kati ya sanaa, biashara na teknolojia. Kupitia mikutano kama hii, wasanii, waunda maudhui na wadau wa sekta ya ubunifu wanapata nafasi ya kuunganishwa na fursa za kimataifa, kujifunza kuhusu ulinzi wa kazi zao, na kuelewa jinsi ya kujitegemea kiuchumi kupitia vipaji vyao. Kwa kizazi kinachotegemea mitandao na ubunifu kama njia ya kujieleza, majukwaa haya yanakuwa daraja kati ya ndoto na mafanikio halisi.
Kwa washiriki kutoka Pwani na sehemu nyingine za Kenya, kongamano hili halikuwa tu mahali pa kuonekana, bali pa kujifunza, kuunganishwa na kuchochewa kufikiria ubunifu kama ajira na biashara. Uwepo wa majina maarufu kama Ruby Kache, Bien, na waunda maudhui wengine wakubwa ulitoa motisha kwa vijana, huku ikithibitisha kuwa sanaa inaweza kuwa nguvu ya kiuchumi na chombo cha mabadiliko chanya katika jamii.