Connect with us

Sports

Sare Tasa na Burkina Faso Yaahirisha Ndoto za Misri Kufuzu Kombe la Dunia

Published

on

Matumaini ya taifa la Misri la kufuzu Kombe la Duniabado  baada ya kutoka sare tasa ya 0-0 dhidi ya Burkina Faso kwenye mechi ya Kundi A iliyochezwa Ouagadougou, Jumanne.

Kikosi cha Hossam Hassan ambacho hakijapoteza mchezo wowote kimefikisha pointi 20 na kuongoza Kundi A kwa tofauti ya pointi tano dhidi ya Burkina Faso, huku kukiwa na mechi mbili pekee zikisalia kwenye mchujo.

Kwa kuwa ni washindi wa makundi pekee wanaofuzu moja kwa moja, mabingwa wa Afrika mara saba wanahitaji alama mbili pekee kutoka kwa michezo yao miwili ya mwisho ili kujihakikishia nafasi na kufanikisha ushiriki wao wa nne kwenye Kombe la Dunia. Watakutana na Djibouti na Guinea-Bissau mwezi Oktoba.

Kocha wa Misri, Hassan, hata hivyo, alisherehekea matokeo hayo ambayo yamewasogeza hatua moja karibu na kufuzu katika mashindano makubwa ya timu 48 yatakayofanyika Amerika Kaskazini mwaka ujao.

“Ni siku kubwa kwa watu wa Misri… Ningependa kuwashukuru kila mchezaji kwa juhudi zao dhidi ya timu ngumu ambayo ina wachezaji wanaocheza Premier League, Bundesliga na Ligue 1,” alisema Hassan, mshambuliaji wa zamani wa Misri aliyewaongoza kufuzu Kombe la Dunia mwaka 1990, akizungumza na kituo cha On Sport.

“Licha ya kucheza ugenini Burkina Faso, tulicheza kwa mtindo chanya na kuunda nafasi kubwa. Wakati huohuo, tulidumisha uwiano. Tungelikuwa tumefunga goli moja au mawili kabla ya mwisho,” aliongeza.

Misri ilipata pigo mapema baada ya mshambuliaji wa Manchester City, Omar Marmoush, kulazimika kutoka nje kwa majeraha dakika ya 9.

Fursa yao bora ilikuja dakika ya 67 wakati Mohamed Salah alipompasia Osama Faisal lakini shuti lake likakataliwa kwa kuotea. Trezeguet wa Misri alikosa nafasi ya kwanza ya mchezo baada ya jaribio lake kuokolewa na kipa wa Burkina Faso, Herve Koffi.

Wenyeji hawakuwa na mashambulizi mengi, huku mshambuliaji wa Sunderland, Bertrand Traore, akiongoza juhudi zao bora.

Misri walikaribia kufunga goli la ushindi dakika za mwisho, lakini Mostafa Mohamed alipoteza nafasi mbili muhimu.

Hassan, ambaye ndiye mfungaji bora wa muda wote wa Misri, anatarajiwa kuwa wa kwanza kuongoza taifa hilo kufika Kombe la Dunia akiwa mchezaji na pia kocha.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 alisema: “Lengo langu lilikuwa kufundisha timu ya taifa ya Misri. Nimekuwa nikiota kila mara jambo hilo. Nataka kutimiza ndoto ya mashabiki na kuishi kwa imani yao (kwa kuongoza timu kufuzu Kombe la Dunia).”

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Uingereza yawapa wapinzani onyo baada ya kuichapa Serbia 5-0, Haaland apiga mabao matano kwa Norway

Published

on

By

Timu ya taifa la Uingereza ilituma onyo kali kwa wapinzani wao wa Kombe la Dunia baada ya kuifumua Serbia 5-0 katika mchezo wa kufuzu siku ya Jumanne, huku Erling Haaland akifunga mabao matano na kuisaidia Norway kuendeleza rekodi ya ushindi wa asilimia 100.

Kwingineko barani Ulaya, Ureno na Ufaransa ziligeuza matokeo baada ya kuwa nyuma na kupata ushindi wa pili mfululizo katika harakati zao za kufuzu kwa michuano ya mwakani itakayofanyika Marekani, Mexico na Canada.

Ubora wa kikosi cha Thomas Tuchel ulitiwa shaka baada ya ushindi hafifu wa 2-0 dhidi ya Andorra siku ya Jumamosi huko Villa Park, lakini safari hii walitoa jibu tosha.

Uingereza ilidhibiti dakika za mwanzo mjini Belgrade na kufungua ubao dakika ya 33, wakati Harry Kane alipofunga bao lake la 74 la kimataifa kwa kichwa akimalizia kona ya Declan Rice. Wageni waliongeza bao dakika mbili baadaye, Noni Madueke akimalizia pasi nzuri ya kichwa kutoka Morgan Rogers na kumchambua kipa wa Serbia, Djordje Petrovic.

Bao la tatu lilipatikana dakika ya 52, Ezri Konsa akipiga shuti kufuatia mpira uliorudi baada ya adhabu ndogo na kufunga bao lake la kwanza la kimataifa.

Mpira mwingine wa adhabu uliopigwa na Rice ulipelekea bao la nne, Marc Guehi akiteleza na kufunga kufuatia faulo iliyofanywa dhidi ya Kane na Nikola Milenkovic, ambaye alionyeshwa kadi nyekundu moja kwa moja.

Mbadala Marcus Rashford alifunga kwa mkwaju wa penalti mwishoni na kukamilisha usiku bora kwa Uingereza.

Uingereza sasa inaweza kufuzu kwa Kombe la Dunia kwa mara ya nane mfululizo kwenye mchezo wao ujao wa Kundi K dhidi ya Latvia mwezi ujao.

Katika mechi nyingine ya kundi hilo, Albania ilipanda hadi nafasi ya pili baada ya kuishinda Latvia 1-0 jijini Tirana.

Continue Reading

Sports

Cape Verde Yashangaza Cameroon, Yakaribia Kufaulu kufuzu Kombe la Dunia kwa Mara ya Kwanza

Published

on

By

Visiwa vya Cape Verde, taifa dogo la kisiwa Afrika Magharibi lenye idadi ya watu wasiozidi 550,000, iliishinda Cameroon 1-0 siku ya Jumanne na kuimarisha matumaini ya kucheza Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.

Timu hiyo kwa jina la utani Blue Sharks wanahitaji alama tatu mwezi Oktoba kutoka mechi dhidi ya Libya na nyumbani dhidi ya Eswatini ili kushinda Kundi D, ambalo lilitarajiwa kudhibitiwa na Cameroon waliowahi kufuzu Kombe la Dunia mara nane.

Mshambuliaji anayekipiga Italia, Dailon Livramento, mwenye umri wa miaka 24 aliyezaliwa Rotterdam kwa wazazi wa Cape Verde, ndiye aliyeibuka shujaa mjini Praia baada ya kufunga bao la ushindi dakika ya 54. Hilo lilikuwa bao lake la tatu katika kufuzu Kombe la Dunia 2026, baada ya mabao mawili yaliyoiwezesha Cape Verde kupata ushindi wa kushtua dhidi ya Angola Machi iliyopita.
Ushindi dhidi ya Cameroon ulikuwa wa furaha zaidi baada ya Indomitable Lions kushinda 4-1 walipokutana Yaoundé mwaka jana.

Cape Verde wana pointi 19, nne mbele ya Cameroon, ambao watakabiliana na Mauritius ugenini na kisha kuwakaribisha Angola katika raundi mbili za mwisho za mchujo wa kufuzu ulioanza mwaka 2023.

Cameroon, ambao wamefuzu mara nane kwenye michuano ya dunia (rekodi ya Afrika), walipata pigo mara mbili kwani sasa wameshuka hadi nafasi ya tano miongoni mwa timu zilizoshika nafasi ya pili. Ni timu nne pekee zilizoshika nafasi ya pili zenye rekodi bora ndizo zitakazofuzu kwa mchuano mdogo, ambapo mshindi ataenda kucheza mchujo wa mabara mwezi Machi kwa nafasi mbili za Kombe la Dunia.

Kwa Cape Verde, kuwa ukingoni mwa kufuzu kwa mara ya kwanza Kombe la Dunia ni mabadiliko makubwa, baada ya kushika mkia kwenye kundi la kufuzu AFCON 2025 kwa kushinda mechi moja pekee kati ya sita.

Kocha wa timu hiyo Pedro Leitao Brito, anayejulikana kwa jina maarufu Bubista (miaka 55), amekuwa akiinoa timu ya taifa tangu 2020. Nahodha ni mshambuliaji anayecheza Uturuki Ryan Mendes, mwenye miaka 35.

Cape Verde wanashikilia nafasi ya 73 duniani, nafasi 22 nyuma ya Cameroon waliowahi kuwa mabingwa wa Afrika mara tano. Mafanikio yao bora ya kimataifa ni kufika robo-fainali ya AFCON mwaka jana.

Senegal walipindua meza 
Senegal walipindua matokeo kutoka nyuma kwa mabao mawili na kushinda DR Congo 3-2 mjini Kinshasa, na kuongoza Kundi B kwa tofauti ya pointi mbili.

Cedric Bakambu na sajili mpya wa Newcastle United Yoane Wissa waliwafungia wenyeji kabla ya kurejea kwa nguvu kwa Senegal katika kipindi cha pili, kilichoisha kwa kiungo wa Tottenham Pape Matar Sarr kufunga bao la ushindi.

Ushindi wa Senegal dhidi ya Sudan Kusini ugenini na nyumbani dhidi ya Mauritania mwezi Oktoba utawapa tiketi ya tatu mfululizo ya Kombe la Dunia.

Nigeria matatani 
Nigeria wako hatarini kukosa Kombe la Dunia kwa mara ya pili mfululizo baada ya kutoka sare ya 1-1 ugenini dhidi ya vinara wa Kundi C Afrika Kusini mjini Bloemfontein.

Mabeki wa Super Eagles walifunga mabao yote mawili kipindi cha kwanza: nahodha William Troost-Ekong akijifunga, kisha Calvin Bassey kusawazisha kwa kichwa.

Nigeria wako nyuma ya Afrika Kusini kwa pointi sita, na matumaini yao ya kufuzu Kombe la Dunia 2026 Amerika Kaskazini huenda yakategemea kumaliza nafasi ya pili na kufuzu mchujo.

Misri wasubiri kidogo 
Ushindi ungeihakikishia Misri kufuzu kutoka Kundi A, lakini walilazimishwa sare ya 0-0 na Burkina Faso walioko nafasi ya pili. Pharaohs wanahitaji pointi mbili zaidi kufanikisha kufuzu kwa mara ya nne.

Continue Reading

Trending