Connect with us

Sports

Sancho Kurejea Manchester United.

Published

on

Kilabu ya Chelsea imelipa ada ya pauni milioni 5 na kuvunja mkataba kati yao na winga wa Manchseter United Jadon Sancho ambaye amekuwepo kilabuni humo japo kwa mkopo.

The Blues walikua tayari kulipa ada ya pauni milioni 25 kwa Mashetani Wekundu kupata sahihi ya winga huyo ila matakwa ya binafsi ya mchezaji huyo ikiwemo mshahara wake wa kila wiki ilizua kutoelewana na badaye kilabu hiyo kubaki na si lingine ila kuvunja mkataba huo.

Sancho mwenye umri wa miaka 26 amekua na wakati mzuri ugani Stamford Bridge akisaidia Chelsea kumaliza ndaani ya nne bora Epl na kushinda kombe la Europa Conference Ligi baada ya kuwa na wakati mgumu Manchester akishindwa kutamba chini ya kocha Erik Ten Hag na badaye Ruben Amorim.

Kinachosubiriwa kuona iwapo atarejea katika kambi ya Manchester ama atasaka makao kwingineko msimu ujao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Chama Cha Raga KRU Yapata Mwenyekiti Mpya

Published

on

By

Chama Cha Raga nchini KRU kimemtangaza Harriet Okach kuwa mwenyekiti mpya kwenye shirikisho hilo kumrithi Sasha Mutai aliyejiuzulu wadhifa wake wiki jana.

Uteuzi huo uliothibitishwa siku ya Alhamisi inamaana kwamba Okach anakua mwanamke wa kwanza kuwa mwenyekiti katika Shirikisho hilo la mchezo wa Raga nchini KRU.

Kabla ya kuteuliwa kwake Okach amekua msimazi wa mauzo kwenye shirikisho hilo,na sasa amesema kwamba analenga kuboresha shirikisho hilo na mchezo kwa jumla anachukua hatamu ya uongozi.

“Nataka nichukue fursa hii kuwashukuru nyote kwa kunipa nafasi hii kwanza shirikisho KRU,washikadhau nimeheshimika mno na nimeahidi sitawangusha ,matumaini yangu ni kufanya Mchezo wa Raga na wachezaji wa Raga kuwa katika mandhari mazuri siku za usoni.”

Mutai alijiuzulu wadhifa wake katika Shirikisho hilo kwa kile alichokitaja ni kutopata ungwaji mkono baina ya washikadau wa mchezo huo nchini.

Continue Reading

Sports

Uhispania Yaikomoa Ufaransa Uefa Nations Ligi.

Published

on

By

UEFA NATIONS LEAGUE

Mabingwa watetezi wa taji la Uefa Nations Ligi Uhispania wameingia kwenye fainali ya taji hilo kwa kishindo Jumapili hii baada ya kunyuka Ufaransa magoli 5-4 hapo jana ugani Allianz Arena.

Winga matata wa Athletico Bilbao Nico Williams aliweka uongozini Uhispania dakika ya 22 kabila ya mshambulizi wa Arsenal Mikel Merino kuweka la pili dakika ya 25 kipindi cha kwanza.

La Furia Roja aliendeleza walipoachia kipindi cha kwanza katika kipindi cha pili huku winga wa Barcelona Lamine Yamal akiweka chuma ya tatu dakika ya 54,na lingine dakika ya 67 kabila ya Pedri kuweka la nne dakika ya 55 na kufanya mambo kuwa magoli 5-0

Hata hivyo Ufaransa walirejea kwa kishindo wakijipatia magoli kupitia Kyllian Mbappe dakika ya 59 naye Ryan Cherki dakika ya 79 Randal Kolo Muani dakika ya 93 uhispania pia wakijifunga kupitia beki Vivian.

Fainali ya Uefa Nations ligi ni kati ya Uhispania na Ureno jumapili saa nne usiku.

Continue Reading

Trending