Business
CBK: Bei za bidhaa za chakula zaendelea kupanda

Utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Benki Kuu ya Kenya (CBK) katika sekta ya Kilimo umebainisha kuwa kuna ongezeko la bei ya bidhaa muhimu za chakula, ikiwemo Mahindi, Sukari, na Mafuta ya kupikia.
Ripoti hiyo ilionyesha kuwa mabadiliko haya ya bei yanachochewa na sababu mbalimbali za kitaifa na kimataifa, zenye athari kubwa kwa walaji wa kawaida na sekta ya biashara kwa ujumla.
Kwa mujibu wa CBK, bei ya Mahindi imekuwa ikiongezeka tangu wiki za mwisho za mwezi Mei.
Hali hii imepelekea ongezeko la bei ya paketi ya kilo 2 ya unga wa Mahindi kwa wastani wa shilingi 6, hatua ambayo wasagaji wa unga wa Mahindi wameitaja kuwa imesababishwa na uhaba wa Mahindi sokoni.
Kukabiliana na changamoto hiyo, Wizara ya Kilimo nchini imeingilia kati kwa kusambaza magunia laki mbili ya Mahindi kwa wasagaji mbalimbali kote nchini, ili kusaidia kudhibiti bei na kuhakikisha upatikanaji wa unga kwa wananchi kwa gharama nafuu zaidi.
Wakati huo huo, bei ya sukari na mafuta ya kupikia pia inatarajiwa kuendelea kupanda.
Ongezeko hili linahusishwa na mabadiliko ya bei katika masoko ya kimataifa, hasa kutokana na kupungua kwa uzalishaji katika baadhi ya nchi zinazouza bidhaa hizo kwa wingi, pamoja na gharama za usafirishaji zinazoendelea kuongezeka.
Business
Wavuvi Old Ferry Wageukia Biashara ya Mahindi Kutokana na Uhaba wa Samaki

Baadhi ya wavuvi kutoka eneo la old ferry kaunti ya kilifi wamegeukia biashara ya kuchoma mahindi machanga kutokana na kutoweza kuingia baharini.
Wavuvi hao wamesema kuwa msimu huu wa kusi hakuna samaki hali ambayo imefanya kuingilia biashara ya kuchoma mahindi ili kujiendeleza kimaisha.
Kulingana na wavuvi kutokana na uhaba wa vifaa vya kisasa hawawezi kuingia katika maji marefu ili kuvua samaki.
Hata hivyo wameitaka serikali kuwawezesha na vifaa vya kisasa ili waweze kuvua katika maji marefu.
Business
Wanawake Pwani Wataka Ushirikishwaji Zaidi Katika Uchumi wa Majini

Wanawake kutoka maeneo ya Pwani wanaitaka serikali kuu na zile za kaunti kuhakikisha wanashirikishwa kikamilifu katika sekta ya uchumi wa majini ili kujiendeleza kimaisha.
Wakiongozwa na Mercy Mghanga, wanawake hao wamesema licha ya wanawake wengi kujihusisha na uvuvi na shughuli nyingine za baharini, bado wanakosa vifaa na msaada wa kukuza biashara zao.
Kwa upande wake Linda Shuma wa shirika la Women and Girls Empowerment CBO, amesema kuna haja ya wanawake kushiriki katika michezo ya majini, utalii na usafiri wa baharini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi.