Connect with us

Business

Rais William Ruto aikabidhi bodi ya majani chai shilingi bilioni 2.65

Published

on

Rais William Ruto ameikabidhi bodi ya majani chai shilingi bilioni 2.65 zilizopatikana kwa benki ambazo zimeshindwa kujiendeleza.

Pesa hizo zilitoka kwa benki ya Chase na Benki ya emperial ambazo zilikuwa zimechukua pesa za wakulima wa majani chai kote nchini.

Kupitia shirika la bima wakulima wa majani chai watalipwa fidia ya hasara iliyosababishwa na kuporomoka kwa benki hizo.

Akizungumza na zaidi ya wakulima 600,000 wa majani chai katika ikulu ya Nairobi rais Ruto alitaka bodi ya majani chai kuhakikisha kuwa pesa hizo zinawafikia wakulima.

Kama juhudi ya serikali kuimarisha sekta hiyo rais ruto alisema kuwa bei ya majani chai imeongezeka katika kipindi cha miaka miwili kutokana na mageuzi yaliyoletwa katika sekta hiyo.

Aidha alisema mapato ya majani chai yamepanda kutoka shilingi bilioni 138 mwaka wa 2022 hadi shilingi bilioni 215 mwaka 2024, huku serikali ikilenga kufikia shilingi bilioni 280 ifikapo mwaka 2027.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Business

Bei ya vitunguu katika masoko ya humu nchini kuongezeka

Published

on

By

Bei ya Vitunguu katika masoko ya humu nchini huenda ikaongezeka hata zaidi kufuatia uhaba wa bidhaa hiyo.

Kufuatia hatua hiyo wafanyibiashara wa vitunguu humu nchini wamelazimika kuagiza bidhaa hiyo kutoka taifa jirani la Tanzania kufuatia kupanda kwa bei ya bidhaa hiyo.

Wakizungumza na vyombo vya habari, Wafanyibiashara hao walisema kuna uhaba mkubwa wa vitunguu jambo ambalo limefanya bei kupanda.

Kulingana na wakulima wa zao hilo, hawakupanda vitunguu kutakana na gharama ya juu ya mbegu pamoja na  changamoto za mabadiliko ya hali ya anga.

Aidha walisema kuwa gharama ya Kilimo cha vitunguu imekuwa juu ikilinganishwa na mapato ya chini na ukosefu wa bei nzuri sokoni.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Business

KEMFRI kuanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki

Published

on

By

Taasisi ya utafiti wa bahari na uvuvi nchini, KEMFRI, imeanzisha mradi maalum wa kuzalisha mbegu za samaki, ili kuongeza upatikanaji wao na kuinua sekta ya uvuvi nchini.

Akizungumza jijini Mombasa, kaimu mkurugenzi mkuu wa KEMFRI, Dkt. James Mwaluma, alisema kuwa mradi huo unatekelezwa katika eneo la Shimoni kaunti ya Kwale na unalenga kuzalisha samaki wa thamani kubwa kama vile kamba, matiko, na aina nyingine ambazo upatikanaji wake ni nadra.

Dkt. Mwaluma alisema kuwa mbegu zitakazozalishwa kupitia mradi huo zitasambazwa kwa vikundi vya vijana na wanawake wanaojihusisha na shughuli za ufugaji wa samaki, ili kuwawezesha kujitegemea kiuchumi.

Aidha, aliwahimiza vijana kote nchini wakumbatie fursa zilizopo kwenye uchumi wa baharini akisema ni njia mojawapo ya kujikwamua kimaisha na kupambana na ukosefu wa ajira.

Taarifa ya Pauline Mwango

Continue Reading

Trending