Connect with us

News

Rais Ruto: Tumeweka mikakati kuimarisha maendeleo Pwani

Published

on

Rais William Ruto amesema wanaendeleza mikakati thabiti katika kuhakikisha kuna miradi mingi ya maendeleo ambayo inatekelezwa kaunti ya Kilifi na kanda ya Pwani kwa jumla.

Rais Ruto ambaye aliwahutubia waombolezaji katika hafla ya mazishi ya Gedion Baya Mung’aro ambaye ni babake gavana wa kaunti ya Kilifi, Gedion Maitha Mung’aro eneo Dabaso katika wadi ya Watamu, alisema shilingi bilioni 3 zimetengwa kufanikisha mradi wa umeme kutoka Malindi kupitia Weru hadi Kilifi.

Rais Ruto pia alisema zaidi ya nyumba elfu 20 zitaunganishwa na mradi wa umeme na pia shilingi bilioni mbili na laki mbili zimetolewa kuhakikisha hilo linafanikishwa.

“Ni jukumu la serikali kuu kuhakikisha kila eneo hapa nchini linatekelezewa miradi ya maendeleo bila kutengwa na pwani ni miongoni mwa maeneo hayo ambayo yanafaa kupata maendeleo’’ Alisema Rais Ruto

Wakati huo huo, Rais Ruto akizungumzia bima ya afya ya SHA, alisema hakuna mkenya ambaye atakosa kutibiwa hospitalini kutokana na ukosefu wa fedha na kuwashinikiza wenyeji wa kaunti ya Kilifi na Wakenya kwa jumla kujisajili kwenye bima hiyo ili watibiwe bila changamoto zozote.

“Tunasema matibabu ni haki ya kila mkenya sababu katiba ndio inasema hivyo’’ Alisema Rais Ruto.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Godhana, awataka wakaazi kutoingiza siasa miradi ya maendeleo

Published

on

By

Gavana wa kaunti ya Tana River Dhadho Godhana amewataka wenyeji wa kaunti hiyo kujiepusha na wanasiasa ambao wanaingiza siasa kwenye masuala ya maendeleo.

Godhana alisema hilo limechangia kaunti ya Tana River kusalia nyuma kimaendeleo hali ambayo itasababisha miradi mingi kuzidi kukwama.

Godhana alisema ni lazima viongozi na wenyeji wa kaunti ya Tana River washirikiane na uongozi wa kaunti ili kuafikia utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo Godhana aliesema mradi wa Village Cluster ambao umekuwa ukipingwa ndio utakaosaidia kudhibiti changamoto ambazo zinaikumba kaunti ya Tana River.

Naye Mahat Ali Loka ambaye ni Naibu Gavana wa kaunti ya Tana River, aliwaonya wanasiasa kutoka kaunti zingine dhidi ya kuingilia siasa za kaunti hiyo huku Spika wa bunge la kaunti hiyo Osman Noor Galole, akitoa onyo kwa wafanyikazi wa umma dhidi ya kujumu la serikali ya kaunti ya Tana River.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Mwili wapatikana baharini Shelly Beach Likoni

Published

on

By

Polisi kaunti ya Mombasa wanachunguza kisa ambapo mwili wa mwanamme ambaye hajafahamika umepatikana ukielea katika maji ya bahari hindi kwenye ufuo wa Shelly Beach eneo bunge la Likoni.

Ripoti ya polisi ilibaini kuwa mwili huo uligunduliwa na wavuvi eneo hilo, ambao walipiga ripoti katika kituo cha polisi cha Shelly Beach kuhusiana na tukio hilo.

Polisi walisema hawakubaini mara moja anakotoka mtu huyo.

Vile vile haikubainika iwapo marehemu alizama au aliuawa kabla ya mwili wake kutupwa baharini.

Polisi walisema hawajakutana na stakabadhi zozote za kumtambulisha mtu huyo huku wakiwasihi wananchi kutoa taarifa iwapo wanafahamu familia ya marehemu.

Mwili unahifadhiwa katika hifadhi ya maiti katika hospitali ya Rufaa ya Coast General Mombasa wakati uchunguzi zaidi ukiendelea.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending