Connect with us

News

Rais Ruto: Mradi wa ujenzi wa nyumba za bei nafuu utaendelea

Published

on

Rais William Ruto amesema lengo kuu la serikali ya Kenya kwanza ni kuhakikisha wakenya wananufaika kimaendeleo na wala sio siasa za vurugu na migawanyiko.

Rais Ruto alisema mpango wa kujenga nyumba za bei nafuu katika maeneo mbalimbali nchini utaendelea ili kuhakikisha wakenya wanamudu gharama ya maisha kwani watakuwa na nafasi nzuri kwenye makaazi bora.

Akizungumza jijini Nairobi, Rais Ruto alisema viongozi wengi wamebali kushirikiana na serikali akiwemo Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga ili kuhakikisha wakenya wanafaidi na raslimali zao.

Kiongozi wa nchi, aliweka wazi kwamba atahakikisha miradi yote ya maendeleo nchini inatekelezwa kupitia ushirikiano wa viongozi na wananchi, huku akiwakosoa wale wanajaribu kurudisha nyuma juhudi za maendeleo.

“Tuko na mpango wa kujenga nyumba za bei nafuu kwani wananchi wetu, watu wengi wanaisha katika nyumba duni na alisema hii maneno tutafanya hata wale wengine waongee maneno mengi mimi nitahakikisha natekeleza jukumu langu”, alisema rais Ruto.

Wakati uo huo aliahidi wakenya kwamba serikali itaendelea na mpango wake wa bima ya afya ya jamii SHA, ili kuwawezesha wananchi wa kipato cha chini wanapata matibabu bila ya kuanganishwa huku akiwarai wakenya kujisajili na SHA.

“Kila mkenya ni lazima apate matibabu kwa gharama ya chini ndio tunasema ni vuzuri wakenya wajisajili katika SHA na tayari wale ambao waliweza kujisajili wameona manufaa ya SHA na kweli tumesajili watu zaidi ya milioni 20”, aliongeza Rais.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

LSK yamtaka Inspakta Kanja kuweka wazi kifo cha Ojwang’

Published

on

By

Chama cha mawakili nchini LSK kinamtaka Inspakta jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja kuhakikisha kuna uwazi kufuatia kifo tatanishi cha mwanablogu Albert Ojwang’.

Akihutubia Wanahabari siku ya Jumatatu, rais wa LSK Faith Odhiambo alimwagiza Kanja kutangaza majina ya maafisa ambao wanazuiliwa wakiwemo wale waliomsafirisha Ojwang’ kutoka kaunti ya Homabay hadi jijini Nairobi.

Kanja alitangaza kuzuiliwa kwa maafisa polisi waliokuwa zamu katika kituo cha polisi cha Central jijini Nairobi wakati Ojwang’ alipowasilishwa kituoni ambapo baadaye alipatikana akiwa na majeraha mabaya ndani ya seli.

Odhiambo aliongeza kuwa taarifa iliyotolewa na Inspakta Jenerali Douglas Kanja kuhusu kifo cha mwanablogu huyo haitosheleza kufafanua yaliyojiri.

“Kwa nini hajataja majini ya maafisa waliozuiliwa? Mbona anaficha? Wacha wakenya wafahamu. Tunataka kujua maafisa waliomchukuwa Ojwang’ je wao ni miongoni mwa wanaozuiliwa?”, alisema Odhiambo.

Rais huyo wa LSK pia alilaumu jinsi maafisa wa usalama walivyomshikilia Ojwang’ hadi akakutana na mauti yake

“Jinsi walivyomhudumia Albert Ojwang’ ni ukiukaji wa haki zake pamoja na wananchi wakenya. Hiki hakiwezi kuchukuliwa kama kisa cha kawaida kwa sababu kinaashiria namna mamlaka inavyohudumu ndani ya huduma ya maafisa wa polisi”, aliongeza rais wa LSK.

Wakati huo huo waanadamanaji pamoja na wanaharakati walikusanyika nje ya makafani ya City jijini Nairobi wakishinikiza hatua za haraka kuchukuliwa kuhusiana na kisa hicho.

Taarifa ya Joseph Jira.

Continue Reading

News

Miraj awahimiza Wapwani kujisajili katika SHA

Published

on

By

Seneta mteule Miraj Abdillahi amewasihi wakaazi wa kaunti ya Mombasa kujisajili katika bima ya Afya ya jamii SHA.

Akizungumza katika eneo bunge la Mvita, Miraj alisema bima hiyo ina manufaa mengi hasa kwa wale ambao wanaugua magonjwa sugu kama ya Saratani na kuwaonya wale ambao wanasusia bima hiyo.

Abdillahi alisema usajili katika bima hiyo ni hatua muhimu ya kuhakikisha kila mkenya anapata huduma bora za matibabu.

“Bima ya SHA ni muhimu sana katika kupata huduma za matibabu na ikiwa kila mmoja atajisajili itakuwa vyema ili kutibiwa bila changamoto zozote’’, alisema Miraj.

Abdillahi pia aliwataka viongozi walioko maeneo ya mashinani kushirikiana na wizara ya afya nchini ili kuwahamasisha wananchi kuhusu umuhimu wa bima hiyo ya SHA.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending