Connect with us

News

Rais Ruto awapongeza maafisa wa Polisi nchini

Published

on

Rais William Ruto ameahidi kuwaunga mkono maafisa wa polisi katika kutekeleza majukumu yao ya kulinda haki za kila mwananchi.

Rais Ruto alisisitiza haja ya kulinda pia Katiba ya Kenya pamoja na kulinda usalama wa Taifa, akisema hatua hiyo itachangia zaidi taifa kushuhudia amani na uzalendo.

Akizungumza katika Ikulu ya Nairobi siku ya Jumanne tarehe 24 Juni, 2025 Kiongozi wa taifa aliwapongeza maafisa wa polisi wakiongozwa na Inspecta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja akisema wamejitolea kuhakikisha taifa la Kenya linaishi kwa Amani.

Rais Ruto alisema viongozi wanaojaribu kuwatishia maafisa wa polisi wanapotekeleza shughuli zao hawawezi kudhalilisha kitengo cha polisi mbele ya macho yake.

“Kuna viongozi wengine wenye kukejeli maafisa wa polisi wanapotekeleza majukumu yao, hiyo haifai tuwape nafasi polisi wetu waendeleza kazi zao kwa kuzingatia sheria na kulinda wananchi bila ya kusumbuana kwa sababu Kenya ni yetu sisi sote”, alisema Rais.

Vile vile alipongeza juhudi za maafisa wa usalama kutoka nchini Kenya ambao wao nchini Haiti katika katika oparesheni ya Kiusalama kama njia moja wapo ya kuleta Amani nchini humo.

Picha kwa hisani

Kwa upande wake Inspekta Jenerali wa Polisi nchini Douglas Kanja, aliahidi kwamba maafisa wa polisi watatekeleza majukumu kwa kuzingatia sheria na mwongozi wa Katiba.

Haya yanajiri huku Wanaharakati wa kutetea haki za kibinaadamu pamoja na vijana wa kizazi cha Gen-z wakishiriki maandamano ya kupinga ukatili unaotekelezwa na maafisa wa polisi nchini.

Hata Juni 25 siku ya Jumatano, vijana wa Gen Z walidai kwamba watashiriki maandamano ya amani kushinikiza kuwajibika zaidi sawa na kuchukuliwa hatua kwa maafisa wa polisi wanaohusika na mauaji ya wananchi kiholela.

Taarifa ya Elizabeth Mwende

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending