Connect with us

News

Rais Ruto, Amteua Ethekon kuwa Mwenyekiti wa IEBC

Published

on

Rais William Ruto amemteua Erastus Edung Ethekon kuwa Mwenyekiti wa Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini IEBC na makamishna 6 wa tume hiyo ili kufanikisha shughuli za uchaguzi nchini.

Katika chapisho la gazeti rasmi la serikali, Rais Ruto amezingatia kipengele cha 250 ibara ya pili {a} ya Katiba ya Kenya na mwongozo wa uteuzi wa makamishna wa sehemu ya 5 na 7 na kutekeleza jukumu hilo.

Katika chapisho hilo lililotiwa saini na Mkuu wa utumishi wa umma nchini Felix Koskei, Rais amezingatia muongozo wa Katiba na kuwateua makamishna 6 wa tume hiyo akiwemo Ann Njeri Nderitu kutoka kaunti ya Nyandarua, Moses Alutalala Mukhwana kutoka kaunti ya Kakamega na Mary Karen Sorobit kutoka kaunti ya Uasin Gishu.

Wengine ni pamoja na Hassan Noor Hassan kutoka kaunti ya Mandera, Francis Odhiambo Aduol kutoka kaunti ya Kisumu pamoja na Fahima Araphat Abdallah kutoka kaunti ya Lamu.

Sasa majina ya makamishna hao na Mwenyekiti mpya wa IEBC yatawasilishwa bungeni kupigwa msasa na kuidhinishwa kabla ya kuapishwa ili kuanza majukumu yao ya kikazi.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Anselim, ashutumu utovu wa usalama Taita Taveta

Published

on

By

Kaimu Spika katika bunge la kaunti ya Taita Taveta Anselim Mwadime alieleza kusikitishwa na mauaji ya mhudumu mmoja wa bodaboda aliyeuliwa na kisha pikipiki yake kuchukuliwa katika eneo la chuo kikuu cha Taita Taveta.

Mwadime alisema kuna baadhi ya abiria ambao ni wahuni hubebwa na kisha kuwashambulia wahudumu wa pikipiki hadi kuwaua au hata kutoweka na pikipiki.

Aidha, Mwadime alisema kama viongozi wa kaunti ya Taita Taveta hawataruhusu visa hivyo kuendelezwa katika kaunti hiyo.

Vilevile, Mwadime aliishinikiza idara ya usalama kwenye kaunti ya Taita Taveta kuwajibika ipasavyo ili kudhibiti visa vya utovu wa usalama katika sekta ya bodaboda na wanaohusika wakabiliwe kisheria.

“Hili jambo linafaa kufuatiliwa kwa undani. Na tunalilaani vikali sisi kama viongozi wa Taita Taveta’’ alisema Mwadime.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

News

Viongozi wahimizwa kushirikiana kubuni ajira kwa vijana

Published

on

By

Mwakilishi wa wadi ya Sabaki eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi Rose Baraka alitoa wito kwa viongozi wa kaunti ya Kilifi kushirikiana na mashirika ya kijamii pamoja na wawekezaji katika kaunti ya Kilifi ili kudhibiti changamoto za ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana.

Rose alisema hatua hiyo itasaidia pakubwa kuwaepusha vijana kujiingiza kwenye utumizi wa mihadarati sawa na uhalifu.

Akizungumza wakati wa kikao kilichowaleta pamoja maafisa wa shirika la SHOFCO pamoja na wakaazi wa Sabaki, Rose aliahidi kushirikiana na mashirika mbalimbali ya kijamii katika juhudi za kuwasadia wananchi kujiendeleza kupitia mpango wa ajira.

“Vijana ni wengi, kazi ni kidogo. Sisi kama viongozi tunastahili kutia bidii kutafuta haya mashirika ili tuangalie vijana wetu wasaidika vipi’’ alisema Rose Baraka.

Kwa upande wake Afisa wa Shirika la SHOFCO eneo la Magarini Kelvin Mtawali Karisa aliupongeza ushirikiano wa mwakilishi wa wadi huyo na shirika hilo na kuwataka vijana kujiunga kwenye makundi mbalimbali ili waweze kupata mikopo ya kujiendeleza kimaisha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending