Sports
Omanyala Amaliza Wa Tatu Mjini Rome

Mkenya na bingwa wa Bara Afrika Ferdinand Omanyala ameweza kumaliza wa tatu mbio za msururu wa Diamond Ligi mjini Rome Italia usiku wa kuamkia leo.
Omanyala alitumia muda wake bora wa sekunde 10.01 nyuma ya mwamerika Trayvon Brommel aliyemaliza wa kwanza kwa kutumia sekunde 9.84 naye Emmanuel Eseme wa Cameroon akimaliza nafasi ya tatu na 9.99.
Haya yanajiri siku chache tu baada ya bingwa huyo kumaliza tena nafasi ya tatu mashindano ya Kip Keino Classic jijini Nairobi.
katika mbio zingine Mkenya Beatrice Chebet alikimbia mbio za kasi zaidi wa dakika ya 14.03.69 na kushinda mbio za mita 5000 ikiwa ni muda bora zaidi mwaka huu akiwapiku wenzake Freweyni Hailu (Ethiopia) na Nadia Battocletti (Italy.
Continue Reading
Sports
Manchester United Ndiyo mabingwa wa ‘PREMIERE LEAGUE SUMMER SERIES’

Manchester United imetwaa ubingwa wa kombe la ‘Premier League Summer Series’ kufuatia sare ya 2-2 dhidi ya Everton katika dimba la Mercedes-Benz, Atlanta, Georgia Marekani.
Michuano hiyo ya maandalizi ya msimu mpya ilishirikisha timu nne za Ligi Kuu England Man United, West Ham United, Everton na Bournemouth ambapo Mashetani hao Wekundu wamemaliza kileleni pointi 7 baada ya mechi tatu, wakishinda mechi mbili na kutoka sare mechi moja.
Kiungo Bruno Fernandes aliwaweka uongozini United dakika ya 18 kupitia mkwaju wa Penalti au Tuta kisha Iliman Ndiaye akisawazishia The Toffees dakika ya 40,United tena walichukua uongozi kupitia kwa kiungo mshambulizi Mason Mount dakika ya 69 kabila ya beki Ayden Heaven kujifunga dakika ya 75.
MSIMAMO:
1. Man UTD — mechi 3 — pointi 7
2. West Ham mechi 3 — pointi 6
3. Bournemouth mechi 3 — pointi 3
4. Everton mechi 3 — pointi 1
Sports
Stars yaanza vema CHAN kwa ushindi goli 1-0 dhidi ya DR-Congo

Timu ya Taifa ya Kenya (Harambee Stars) imechukua alama zote tatu kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kwenye mchezo wa kwanza wa Kundi B wa kombe la Mataifa Afrika CHAN 2024 katika dimba la Moi Sports Centre, Nairobi.
Goli hilo la kipekee lilitiwa wavuni na kiungo mshambulizi Austine Odhiambo dakika 45 kipindi cha kwanza.
Rais William Ruto ambaye alifuatilia mechi hiyo uwanjani alitembelea kikosi katika chumba cha kubadilisha na kukabidhi ahadi yake ya shilindi milioni moja kwa kila mchezaji baada ya ushindi huo.
Stars wamekwea kileleni mwa kundi A na alama Tatu kundi ambalo pia lina Morocco,Zambia na Angola Mechi ijayo ya Stars ni dhidi ya Angola ni Agosti 7.