Connect with us

Sports

Omanyala Amaliza Wa Tatu Mjini Rome

Published

on

Mkenya na bingwa wa Bara Afrika Ferdinand Omanyala ameweza kumaliza wa tatu mbio za msururu wa Diamond Ligi mjini Rome Italia usiku wa kuamkia leo.

Omanyala alitumia muda wake bora wa sekunde 10.01 nyuma ya mwamerika Trayvon Brommel aliyemaliza wa kwanza kwa kutumia sekunde 9.84 naye Emmanuel Eseme wa Cameroon akimaliza nafasi ya tatu na 9.99.

Haya yanajiri siku chache tu baada ya bingwa huyo kumaliza tena nafasi ya tatu mashindano ya Kip Keino Classic jijini Nairobi.

katika mbio zingine Mkenya Beatrice Chebet alikimbia mbio za kasi zaidi wa dakika ya 14.03.69 na kushinda mbio za mita 5000  ikiwa ni muda bora zaidi mwaka huu akiwapiku wenzake Freweyni Hailu (Ethiopia) na Nadia Battocletti (Italy.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Harambee Stars Kuvaana Na Chad Mechi Ya Kirafiki.

Published

on

By

Timu ya Taifa Harambee Stars chini ya kocha Benni Mccarthy kushuka dimbani majira saa kumi jioni Ugani Stade de Marrakech Morocco ikiwa ni mechi ya kirafiki.

Kwa mujibu wa mwalimu wa Stars Mccarthy mechi hizi ni muhimu kujenga kikosi kwa majukumu ya siku za usoni lakini pia kwa taji la Chan sawa na Afcon mwaka 2027.

“Ni muda mzuri mimi kufahamu vijana wangu na kuanza kuanda timu yenye ubora kwa minajili ya siku za usoni na wachezaji wa nyumabani watasaidia sana CHAN mwezi Agosti.”

Baada ya mechi hiyo Stars watacheza mechi nyingine na taifa hilo Juni 10.

Rais wa Fkf Hussein Mohammed amekariri kikosi hicho kitaelekea Uarabuni kwa maozezi kabambe kabila ya Chan humu nchini.

Continue Reading

Sports

Kenya Pipeline Yaanza Kwa Kishindo Fainali Ya Voliboli

Published

on

By

Kilabu ya Kenya Pipeline ilianza kwa kishindo fainali ya taji la akina dada mchezo wa voliboli mashidano yanayondelea uwanjani Kasarani Indoor Arena jijini Nairobi.

Hii ni baada ya vipusa hao chini ya kocha Godfrey Omondi kuwatandika wenzao DCI seti 3-0 mechi ya ufunguzi uwanja huo ukifurika hadi pomoni.

Kikosi hicho kilishinda mechi hiyo kwa seti 25-19,25-20,25-14 na kuibuka na ushindi huo mnono kabila ya mechi ya pili jumamosi.

Nahodha wa KPC Gladys Ereng amesema kwamba mechi haikua rahisi kwani DCI walikua vizuri ila walipambana kwa ushindi huo.

“DCI ni timu nzuri walicheza vizuri kipindi cha kwanza kwani tulianza kwa utepetevu ila tukazungumza na kujikusanya vyema na kupata ushindi huo muhimu kwetu.”

Kwa Upende wake kocha wa DCI Patrick Sang amedokeza kwamba hakucheza kwa umakinifu waliotarajia;”Hatukucheza kwa mipangilio yetu mazungumzo pamoja na utulivu haikuwepo lakini ndio hali ya mchezo nipongeze wenzetu.”

Kilabu ya General Service Unit (GSU) upande wa  wanaume ilianza vema kusaka taji la upande wa Wanaume baada ya kushinda mechi ya mkondo kwanza sati 3-0 katika uwanja huo huo.

Hii ni baada ya kuwatandika Kenya Ports Authority (KPA) seti 3-0 za 25-15,25-22,30-28

Continue Reading

Trending