News
Odinga, awasuta wapinzani dhidi ya kauli ya Wantam

Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga ameonekana kuunga mkono ushirikiano kati ya chama cha UDA na ODM, na akawasuta wapinzani dhidi ya kauli yao ya Wantam.
Odinga aliwataka wakenya na upinzani kuipa nafasi serikali kukamilisha ajenda yake na kisha wananchi watafanya uamuzi wao ifikapo uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2027.
Akizungumza wakati wa mazishi ya Pheobe Asiyo katika kaunti ya Homabay, Odinga aliweka wazi kwamba juma lijalo kutakuwa na mkutano wa Muungano wa wabunge ambao utaangazia masuala mbalimbali muhimu.
“Niko na imani kwamba masuala mbalimbali anayoihusu taifa yatatekelezwa na tunaomba mtupe nafasi kisha ikifika uchaguzi mkuu mwaka 2027 wakenya ndio wataambua sio tu kubweka bweka na Wantam wantam”, alisema Odinga.
Wakati huo huo aliitaka serikali kufanikisha mchakato wa fidia kwa wananchi ambao wamepoteza maisha yao wakati wa maandamano ya ghasia, akisisitiza suala kangazia majanga ya maandamano ya mwaka wa 2017.
Kauli za viongozi hao zimejiri baada ya kuafikiwa mpango wa kufanikisha ajenda 10 kwenye mkataba wa ushirikiano wa kitaifa kati ya chama cha UDA na ODM pamoja na kuidhinishwa kwa ripoti ya NADCO.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu wakamatwa, Malindi

Maafisa wa polisi Malindi kaunti ya Kilifi wanasema wamewanasa washukiwa 42 wa magenge ya uhalifu katika msako kwenye mitaa ya Karima, Soweto, Milano na Mgandini.
Polisi ilisema msako huo umewawezesha kuwakamata washukiwa 11 wa genge la “Wakali Mwisho” na wanawake watano kwa visa vya utovu wa nidhamu.
Msako huo unafuatia zaira ya kamanda wa polisi ukanda wa pwani Ali Nuno katika eneo hilo na kuwataka polisi kuongeza juhudi za kukabiliana na wanachama wa magenge hayo wanaoendelea kuwahangaisha wananchi.
Simu 14 zilizoshukiwa kuwa za wizi zilinaswa kutoka kwa mshukiwa Ahmed Ali.
Magenge ya uhalifu wakiwemo wale wanaojiita mawoza ni miongoni mwa makundi ya vijana ambao wamekuwa wakitatiza amani na usalama miongoni mwa wakaazi eneo hilo.
Idara ya usalama ilikuwa mbioni kuwasaka wahalifu katika mji huo wa kitalii katika juhudi za kurejesha amani na utulivu.
Vijana hao wamekuwa wakiwavamia wakaazi na kutekeleza vitendo vya wizi.
Taarifa ya Joseph Jira.
News
Mabadiliko ya tabianchi yatajwa kuchangia mapato duni ya samaki, Lamu

Wadau katika sekta ya mazingira kaunti ya Lamu wanasema mabadiliko ya hali ya anga yanayoshuhudiwa sawa na ujenzi wa bandari ya Lamu kumechangia mapato ya samaki kupungua katika bahari hindi.
Mahmoud Yusuf ambaye ni mwanazingira alisema zana za kizamani wanazotumia wavuvi kuvua samaki pia zinachangia mapato duni ya samaki.
Yusuf alisema tangu ujenzi huo wa bandari uanze, maji ya bahari chini yamekuwa na matope kutokana na kuchimbwa na kufukuliwa kwa bahari, hali iliyochangia samaki kutorokea bahari kuu.
Mwanamazingira huyo aliitaka serikali kuwapa wavuvi vifaa vya kisasa vya uvuvi sawa na meli za uvuvi zitakazowawezesha kufika maji makuu, baada ya bandari ya ndani kuharibika.
Taarifa ya Joseph Jira.