Connect with us

News

Odinga, anataka fedha za NG-CDF kusambazwa kwa kaunti

Published

on

Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga amependekeza fedha zote zinazosambaza kwa hazina ya NG-CDF na NGAAF, kufanywe marekebisho ili fedha hizo kusambazwa kwa serikali za kaunti.

Odinga alisema kila kitu ambacho wakenya wamefanya ni kurudisha utawala bora, na wamefanya hazina ya NG-CDF kuwa ya kizamani na kwamba fedha hizo zinafaa kutumwa kwa serikali za kaunti kwani hazina hiyo hatambuliki kikatiba.

Akihutubia Kongamano la Ugatuzi katika kaunti ya Homabay, Odinga alishikilia msimamo wake kwamba ni lazima ugatuzi upewe kipau mbele na masuala yote yaliyogatuliwa kusimamiwa na serikali za kaunti. 

“Hazina ya NG-CDF na NGAAF zinapokea fedha nyingi na kutumika kwa mambo ya basari, hii pesa inafaa kutumwa kwa serikali za ugatuzi kwani hazina ya NG-CDF ilipitwa na wakati na hatambuliki kikatiba na iwapo kutafunywa marekebisho basi pesa hizo zitasaidia ugatuzi kuimarika zaidi”, alisema Odinga.

Kinara wa Chama cha ODM Raila Odinga katika Kongamano la ugatuzi, Homabay{Picha kwa hisani}

Wakati huo huo amevisuta vyombo vya habari, akisema baadhi ya vyombo vya habari nchini vimekuwa vikilipwa ili kufichua sakata za ufisadi nchini, akisema ni lazima kila mmoja achukue jukumu la kupambana na ufisadi.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi

Published

on

By

Mahakama ya Kilifi imetoa hukumu kwa wanaume 6 wanaokabiliwa na mashtaka ya unajisi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Ivy Wasike alimhukumu Lucky Munga na Hassan Daniel kifungo cha miaka 30 gerezani baada ya Mahakama kubaini kwamba walihusika kwa kuwatendea unyama watoto wa umri wa miaka 13 na 15.

Safari Karisa Lewa alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa kumnajisi mtoto wake mwenyewe wa umri wa miaka 14 huku Eric Ruwa na Lucky Katana Kenga wakihukumiwa kifungo cha miaka 6 gerezani kwa kosa sawa na hilo.

Hata hivyo Mahakama hiyo ilimhukumu kifungo cha miaka 3 Kithi Kombe kutokana na kesi hiyo kwa mtoto wa miaka 15, japo baadaye Mahakama ikabaini kwamba mshukiwa sio baba halali wa mtoto aliyezaliwa baada ya Kithi kumnajisi mtoto huyo.

Akizungumza wakati wa vikao vya Mahakama baada ya kutoa hukumu hizo, Hakimu Wasike alisema Mahakama umezingatia ushahidi uliyotolewa Mahakamani huku akiwarai wananchi kujitenga na visawishi vibaya ili kuepuka mkono wa sheria.

Hakimu Wasike alihoji kwamba washtakiwa wa haki ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama lakini kwa kuzingatia taratibu zote za Mahakama na sheria.

Taarifa ya Teclar Yeri

Continue Reading

News

Thoya: Serikali kuu iongeze mgao wa fedha kwa sekta ya Afya

Published

on

By

Naibu gavana wa kaunti ya Mombasa Francis Thoya ametoa changamoto kwa serikali kuu kuongeza mgao wa fedha ili kufanikisha utaoji wa huduma za afya.

Akizungumza katika kaunti hiyo, Thoya alisema kuwa huduma nyingi za afya katika kaunti hiyo ya Mombasa zinakabiliwa na changamoto ya raslimali ndogo hali ambayo inakwamisha juhudi za kuwahudumia wananchi ipasavyo.

Thoya pia alitaka serikali kuhakikisha inaharakisha kuajiri wahudumu zaidi wa afya ili wenyeji wa Mombasa waweze kupata huduma bora za matibabu bila changamoto zozote.

Aidha, Thoya alisema kwamba hali ya uhaba wa wahudumu wa afya ni changamoto kuu ambayo inazuia utoaji wa huduma bora za matibabu hali inayowafanya wale wachache waliopo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending