Connect with us

Sports

Nyota wa Liverpool Diego Jota Aaga Dunia.

Published

on

Mshambulizi wa Liverpool Diogo Jota amefariki dunia kufuatia ajali ya gari nchini Uhispania akiwa na umri wa miaka 28, vyombo vya habari vya Ureno vimeripoti.
Inasemekana Jota alikuwa akisafiri kwa gari pamoja na kaka yake Andre, ambaye pia ni mwanasoka mwenye umri wa miaka 26.
Tukio hilo lilitokea  katika jimbo la Zamora wiki mbili tu baada ya Jota kufunga ndoa na mpenzi wake wa muda mrefu Rute Cardoso huko Porto.
Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Rais Ruto Awapa Morale Kikosi Cha Stars Kambini

Published

on

By

Rais William Samoei Ruto mapema Leo ametembelea kikosi Cha timu ya Taifa Mpira wa Soka Harambee Stars Ugani Kasarani wanapofanyia mazoezi kwa Kombe la Chan 2025 mwezi ujao.
Hii ikiwa ni njia moja wapo ya kuwapa mortisha vijana wa nyumbani akiahidi Stars nchi nzima iko nyuma Yao.

Ruto amewatakia heri Stars na kuambia vijana wa nyumbani watapata sapoti yoyote wanayohitaji kutoka kwake wanapo peperusha bendera ya taifa hili kwenye kipute cha CHAN mwezi ujao.

“Nataka tushinde kombe hili katika nchi yetu,kila Mkenya yuko nyuma yenu kuwapiga jeki ili mpate matokeo chanya mimi na serikali yangu tunahidi kuwapa sapoti yote kwa kombe hili.”

Rais aliandamana na Waziri wa Michezo Salim Mvurya pamoja na waziri wa Ulinzi Soipan Tuya.

Vijana wa nyumbani wanafungua kampeini Agosti 3 dhidi ya DR. Congo ugani Kasarani ambapo watapiga mechi zao zote.

Continue Reading

Sports

Kasarani Na Nyayo:Uwezo Wa Kubeba Mashabiki Yapungua

Published

on

By

CHAN Siku 17 zimesalia kipute hicho kungoa nanga nchi za Kenya,Uganda na Tanzania.

Serikali ya Kenya kupitia Wizara ya Michezo imetumia Kima Cha zaidi ya Shilingi Bilioni 6.7 kufanyia Ukarabati uwanja wa Kasarani na Shilingi nyingine Bilioni 1.1 Uga wa Nyayo.

Uwanja wa Kasarani Ulifungwa mwaka 2023 Kwa shughuli hiyo ya ukarabati huku uga wa Nyayo ukifungwa mwaka mmoja badaye 2024 kwa Maandalizi ya kipute cha CHAN kinachotarajiwa kung’oa nanga chini ya siku 17 zijazo.
Viwanja hivyo sasa vinauwezo wa kubeba mashabiki 55,000 na 22,000 mtawalia.
Ikumbukwe kabila ya ukarabati wa uwanja wa Kasarani ulikuwa na uwezo wa kuwabeba takriban mashabiki 60,000 huku uwanja wa Nyayo ukibeba mashabiki 30,000.
Continue Reading

Trending