News
Ni Lazima Tushinde Paris Asema Arteta

Mkufunzi wa kilabu ya Arsenal Mikel Arteta angali na imani kwamba vijana wake watanyuka Psg ugenini na kufuzu kwenye fainali ya kilabu bingwa ulaya wiki ijayo mjini Paris.
Akizungumza baada ya The Gunners kukubali kichapo cha goli 1-0 mechi ya mkondo wa kwanza Arteta amedai kwamba mchezo huo walipoteza kutokana na vitu vichache vya kimbinu kipindi cha kwanza ambapo wapinzani wao waliwalemea kimbinu zaidi.
“Bado mechi haijaisha ni nusu tu,bado dakika zingine 90 mjini Paris na tunaenda kwa ajili ya kuvuna ushindi hakuna lingine,”Asema Arteta
Kwa mujibu wa mwalimu huyo wanahitaji kuwa katika ubora wao kuangusha Psg kwani wako na timu nzuri ila lengo lao linasalia pale pale kushinda na kufuzu kwenye fainali mwezi wa May 31.
“Ni lazima tuonyeshe uwezo wetu tokea dakika ya kwanza kwamba tunahitaji ushindi huo, nitafanyia mabadiliko ya kimbinu kikosi kabla ya kuelekea Paris na tuko tayari kupindua meza kule.”
Timu hiyo ililazwa goli 1-0 na miamba hao wa ufaransa kupitia goli lake Ousmane Dembele na sasa wanahitaji kushinda kwa zaidi ya magoli 2-0 mechi ya mkondo wa pili ugani Parc De Prince siku ya Jumatano wiki ijayo.
News
Mahakama kuu yatupilia mbali ombi la Gachagua

Mahakama kuu imetupilia mbali ombi la pili la aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua la kutaka jopo la majaji watatu wanaosikiliza kesi ya kupinga kubanduliwa wake mamlakani kuzuiliwa kuskiza kesi hiyo.
Gachagua alisema kwamba majaji hao watatu akiwemo Jaji Eric Ogola, Anthony Mrima na Fridah Mugambi wanafaa kuondolewa kwenye kesi hiyo kwa misingi kwamba uteuzi wao haujazingatia sheria.
Mahakama hiyo ilitupilia mbali ombi hilo, na kusema kwamba jopo hilo la majaji watatu liliteuliwa na Jaji mkuu Martha Koome kwa kuambatana na sheria na kanuni za idara ya Mahakama.
Mahakama imeshikilia kwamba jopo hilo la majaji wa Mahakama kuu litaendelea kusikiliza kesi hiyo hadi wakati wa kutoa uamuzi kwa kuzingatia sheria, na kanuni za idara ya Mahakama pamoja na Katiba ya Kenya.
Mahakama hiyo pia ilitupilia mbali ombi la Mwanaharakati Fredrick Mula ambaye alitaka kubadilishwa kuwa mlalamishi katika kesi nne za kuondolewa mashtaka dhidi ya aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua ambazo alikuwa amewasilisha awali na kisha kutaka kujiondoa.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi
News
Wazee wa Kaya wanataka bunge kupitisha sheria kudhibiti mauaji ya wazee

Muungano wa Wazee wa Kaya kaunti ya Kilifi umeitaka serikali kuu kupitia bunge la kitaifa kubadilisha sheria ya mwaka wa 1926 kuhusu uchawi ili kuwezesha utamaduni kudhibiti mauaji ya wazee yanayoendelea kushuhudiwa kaunti ya Kilifi.
Wakiongozwa na Stanley Kahindi Kiraga wamesema kuwa sheria hiyo imechangia pakubwa mauaji ya wakongwe Kilifi kutokana na swala kuwa haitambui uwepo wa uchawi na jinsi ya kuudhibiti.
Kiraga sasa anasema ni sharti sheria hiyo iondolewe au ifanyiwe ukarabati bungeni hali itayopelekea uchawi kudhibitiwa kupitia mila na utamaduni.
“Vijana wanaowaua wazee wakiwasingizia kuwa wachawi wanazidi kuongezeka na kwa sababu hakuna sheria ya moja kwa moja ya kuwashtaki na kuwafunga” amesema Kiraga akieleza kusikitishwa kwake na ongezeko la magenge ya vijana wanaolipwa kutekelezwa mauaji ya wazee kwa shutuma za uchawi.
Taarifa ya Hamis Kombe