
Raila Azungumza Baada ya Kuanguka Uchaguzi wa AUC
Aliyekuwa mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa Tume ya umoja wa Afrika, AUC, kutoka Kenya, Raila Odinga, amevunja kimya chake na kuzungumzia uchanguzi wa nafasi hiyo uliyofanyika siku ya Jumamosi.
Akihutubia wajumbe wakenya akiwa jijini Addis Ababa nchini Ethiopia, Odinga amesema wakenya wanafaa kusitisha uvumi kwamba alishindwa kutokana na uzee, ama kukosa kufanya kampeni bora.
Odinga amesema kuna maswala muhimu ambayo yanafaa kuangaziwa ili changuzi zijazo iwe rahisi kwa Kenya kunyakua kiti hicho na wala sio kwa wakenya kuendeleza propaganda zisizo na manufaa yoyote.
Odinga hata hivyo amempogeza rais William Ruto kwa kuhakikisha kampeni zake zinafanyika vyema sawa na kumpangia vikao na marais wa mataifa ya Afrika ili kutafuta uugwaji mkono, japo hakufaulu.
International News
Musevani ateuliwa kuwania urais Uganda mwaka 2026

Chama tawala nchini Uganda, cha National Resistance Movement (NRM), kimemteua Rais Yoweri Museveni kuwa mgombea wake wa urais katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2026.
Akizungumza baada ya uteuzi huo uliofanyika katika makao makuu ya Tume ya uchaguzi ya chama cha NRM mjini Kampala, Rais Museveni alisema atazingatia zaidi masuala ya kuinua uchumi wa jamii na maendeleo.
Museveni alisema iwapo atachaguliwa tena kuliongoza taifa hilo basi atahakikisha Uganda inaendelea kushuhudia maendeleo licha ya kutawala taifa hilo kwa zaidi ya miaka 40 tangu mwaka wa 1986.
Japo taifa la Uganda limekuwa likiandaa chaguzi za kidemokrasia, Rais Museveni alishtumiwa kwa kukandamiza upinzani na kuendeleza utawala wa kidikteta.
Museveni na mkewe Janet wakiwasili katika makao makuu ya NRM
Akiwa uingozini, Rais Museveni alishinikiza kufanyika kwa mabadiliko Katiba ya nchi hiyo, kwanza mnamo mwaka wa 2005 kuondoa umri unaoruhusu mtu kuwania kiti cha urais nchini humo na kisha mnamo mwaka wa 2017, katiba hiyo ikafanyiwa marekebisho kufutiliwa mbali vipindi vya kiutawala.
Kufuatia hatua hiyo, sasa Museveni ana nafasi nzuri ya kuwania tena kiti cha Urais mwaka ujao wa 2026 wakati w auchaguzi mkuu nchini humo.
Upinzani ulishtumu vikali hatua hiyo ukisema ni ukiukaji wa Katiba huku Mpinzani mkuu nchini humo Kizza Besigye yuko korokoroni akikabiliwa na shtaka la uhaini ingawa hali yake ya afya inatajwa kuendelea kudhofika.
Taarifa ya Eric Ponda
International News
Matumaini ya kusitisha vita Gaza yaanza

Licha ya Rais wa Marekani Donald Trump kusema kwamba mpango wa usitishaji mapigano kwa siku 60 katika Ukanda wa Gaza unakaribia, kundi la Hamas limeeleza kwamba bado mazungumzo yanaendelea.
Katika kile kinachoonekana kama jibu la kwanza la Hamas tangu Rais Trump kutangaza kupatikana kwa mwafaka huo, kundi hilo lilisema kwamba bado linaendelea kuyatafakari mapendekezo mapya yaliyomo kwenye mpango huo.
“Tunalichukulia suala hili kwa uangalifu mkubwa. Tunafanya majadiliano ya kitaifa kuyatathmini mapendekezo ya ndugu zetu wapatanishi”, lilisema kundi hilo kupitia Kiongozi wao.
Mnamo siku ya Jumanne Julai mosi mwaka huu, Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba Israel ilikuwa imekubaliana na masharti ya kusitisha mapigano kwa siku 60 wakati mauaji kwenye ukanda wa Gaza yakiwa kwenye mwezi wake wa 21.
Trump alidai kwamba Misri na Qatar, ambazo ni wapatanishi wakuu, walikabidhiwa jukumu la kuwafikishia mapendekezo hayo Hamas lakini wakati huo huo akilitishia kundi hilo kutokuutakaa mpango huo.
“Tunaamini kwamba Misri na Qatar wanaendelea na mpango mzuri wa upatanisho na suala hili linafaa kuchukuliwa kwa uzito zaidi lakini pia ni lazma Hamas iwe waangalifu na kuzingatia masharti hayo”, alisema Trump.

Baraza la usalama lajadili upatishi Gaza.
Waziri wa Mambo ya nje wa Israel, Gideon Saar, alisema sehemu kubwa ya mawaziri kwenye serikali ya nchi yake wanaunga mkono makubaliano hayo ambayo yanajumuisha kuachiliwa kwa mateka.
Waziri huyo wa mambo ya kigeni aliongeza kwamba sehemu kubwa ya raia wa Israel wanaunga mkono makubaliano hayo kama inavyothibitishwa na uchunguzi wa maoni.
Hata hivyo, Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anatarajiwa kukutana na Rais Trump wiki ijayo mjini Washington, ili kuangazia zaidi mikakati na mipango ya kudhibiti.
Taarifa ya Mwahoka Mtsumi