Connect with us

News

Ndoto ya Matiang’i kuwania urais 2027 yaingia doa

Published

on

Mbunge wa Gem Elisha Odhiambo ametangaza mipango ya kumchukulia hatua za kisheria aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani Dkt Fred Matiang’i kutokana na madai ya mauaji ya kiholela wakati wa utawala wa serikali ya Jubilee.

Mbunge huyo alifichua kuwa anakamilisha ombi la kutaka kumzuia Dkt. Matiang’i kuwania urais, akimwajibisha kwa kile alichokitaja kama dhuluma zilizoidhinishwa na serikali – haswa kutupwa kwa miili katika Mto Yala.

“Kama mbunge wa Gem, nilifanya mkutano na mawakili jana usiku baada ya kusikiliza kauli ya Matiang’i akithibitisha kuwa Wakenya kadhaa waliouawa kwa kuchinjwa walitupwa kwenye mto Yala, tunaenda katika mahakama ya rufaa ili tuweze kumshtaki kama mtu binafsi kwa miile kutupwa kwenye mto Yala ili awajibike kama afisa wa zamani wa afisi ya usalama wa kitaifa,” ilisema Odhiambo.

Odhiambo alimshutumu waziri wa zamani wa mambo ya Ndani kwa kusimamia utawala wa ugaidi uliosababisha uharibifu wa mazingira na kibinadamu katika baadhi ya maeneo ya eneo bunge la Gem.

Alidai kuwa miili mingi iligunduliwa ikiwa imetupwa katika mto Yala wakati wa uongozi wa Matiang’i, akitaja tukio hilo kama “ugaidi wa mazingira” na doa kwa ustawi wa jamii.

Akizungumza katika mahojiano ya kipekee na runinga moja nchini siku ya Jumanne mwezi juni 2, 2025, Matiang’i alisema alifuatilia suala la miili ya River Yala kwa Inspekta Jenerali wa polisi wakati huo Hillary Mutyambai, ambaye alishikilia kuwa walihitaji familia hizo kutambua miili hiyo ili kufichua ukweli.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

News

Mahakama ya Malindi yawaachilia washukiwa 3 wa kesi ya Kwa Binzaro

Published

on

By

Mahakama Kuu ya Malindi imewaachilia washukiwa watatu wanaohusishwa na kesi ya mauaji ya halaki ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro eneo bunge la Magarini kaunti ya Kilifi.

Hakimu wa Mahakama hiyo Joy Wesonga aliagiza kuachiliwa huru kwa Safari Kenga Nzai, Gona Charo Kalama na Kahindi Kazungu Garama wote wakiwa wakaazi wa kijiji hicho cha Kwa Binzaro.

Watatu hao walikuwa wamekamatwa baada ya kudaiwa kuuza shamba la ekari tano kwa mshukuwa mkuu wa mauaji ya watu katika kijiji cha Kwa Binzaro Sherleen Temba Anido.

Hakimu Wesonga aliwaagiza washukiwa hao kuhakikisha wanasalimisha nakala za vitambulisha vyao vya kitaifa kwa idara husika, kuripoti kwa Naibu Chifu wa eneo hilo mara mbili kwa wiki pamoja na kujisalimisha kwa maafisa wa upelelezi wa kesi hiyo mara moja kila baada ya wiki mbili.

Miili iliyofukuliwa katika kijiji cha Kwa Binzaro 

Wakati huo huo upande wa mashtaka ukiongozwa na Naibu mkurugenzi wa mashtaka ya umma Jamie Yamina, uliomba kuwasilisha watu wengine wanne Mahakamani ikiwemo Jairus Otieno na mkewe Lilian Akinyi, Kahonzi Katana Karisa na Loise Zawadi waliojionda kama washukiwa na kugeuka kuwa mashahidi wa serikali.

Upande wa mashtaka pia uliaka kupewa siku 60 zaidi kuendelea kuzuiliwa kwa washukiwa wakuu Sherleen Temba Anido, James Kahindi Kazungu, Thomas Mukunwe na Kahidi Kazungu Garama katika kituo cha polisi cha Ngerenya, Kilifi, Watamu na Kijipwa ili kukamilisha uchunguzi wao kwani wanne hao wanakabiliwa na mashtaka ya itikadi kali, ugaidi, kujihusisha na uhalifu na kupanga mauaji.

Taarifa ya Mwahoka Mtsumi

Continue Reading

News

Chrispus aomba msahama bunge la kaunti ya Taita Taveta

Published

on

By

Mwakilishi wadi ya Bomani mjini Taveta kaunti ya Taita Taveta Chrispus Tondoo ameliomba bunge la kaunti hiyo msamaha kutokana na matamshi aliyoyatoa hapo awali akikashifu bunge hilo kwa madai ya kushamiri kwa visa vya ufisadi na utepetevu.

Tondoo akiomba msamaha katika bunge hilo alisema alitambua athari zilizosababishwa na matamshi hayo kwa wenyeji wa kaunti hiyo na bunge hilo, hali ambayo imemfanya kuchukua hatua hiyo ya kuomba msamaha.

Aidha Tondoo aliahidi kuliheshimu bunge hilo kwa mujibu wa kanuni na Sheria za bunge la kaunti ya Taita Taveta.

‘’Naomba msamaha kutokana na matamshi ambayo niliyatoa tarehe 2 na tarehe 3 mwezi wa Juni mwaka huu wa 2025 kwani hayakuwa yenye heshima kwa wenyeji wa Taita Taveta na bunge la kaunti’’, alisema Tondoo.

Tondoo alikuwa Mwakikishi wa wadi wa pili kuomba msamaha baada ya Mwakilishi wa wadi ya Kaloleni mjini Voi Ahmed Azari kuchukua hatua hiyo mwezi mmoja uliyopita.

Haya yalijiri baada ya kaimu spika wa bunge hilo Anselim Mwadime kuapa kuwachulia hatua za kisheria wanachama wanne wa bunge hilo, wawili wakiwa ni Tondoo na Azari ambayo tayari wameomba msamaha huku wawili wakiwa wamesalia bila kuomba msamaha.

Taarifa ya Janet Mumbi

Continue Reading

Trending