Connect with us

Entertainment

Ndoa Tano Tena: Ruby Kache Asitisha Mpango wa Ndoa kwa Miaka Mitano

“Nitangoja tena miaka mitano kabla sijafanya maamuzi ya kuolewa.” — Ruby Kache

Published

on

Mtangazaji wa kipindi cha The Wave, Ruby Kache, amefunguka kwa hisia kali kuhusu maamuzi yake ya ndoa — akisema kuwa atasubiri miaka mingine mitano kabla hajafanya uamuzi wowote kuhusu kuolewa.

Katika mjadala moto uliotikisa hewani kati yake na mtangazaji  mwenzake Hon. Baba Yaga, Ruby alieleza kuwa kauli ya Baba Yaga kwamba “mpango wa kando ni lazima katika ndoa” ilimvuruga sana na kumfanya arejee upya mtazamo wake kuhusu taasisi ya ndoa.

“Ndoa tano tena,” alisema Ruby.

Kauli ya ulizima wa mchepuko kwenye ndoa inaonesha jinsi taasisi ya ndoa inavyochukuliwa kwa mzaha. Na labda miaka mitano ni muda wa kutosha kwa Ruby kutafakari, na kujiandaa kwa maamuzi makubwa ya kuolewa.

Kauli hii ilitolewa wakati walikuwa wakichambua kisa cha mwanamume aliyemwandikia mpango wake wa kando ujumbe akimweleza kuwa matatizo ya uhusiano wao huathiri hata ndoa yake rasmi.

Katika maelezo yake ya kulinda mtazamo wa mwanaume huyo, Baba Yaga alitoa mfano tata akisema:

“Kama serikali inahitaji upinzani ili iwe na mwelekeo, basi hata ndoa inahitaji mpango wa kando ili iwe na mizani.”

Kauli hiyo ilizua sintofahamu, mshangao kwa Ruby Kache ambaye alitafsiri maneno hayo kama kejeli kwa taasisi ndoa.

Kipindi hicho kiligeuka kuwa jukwaa la kuibua maswali mazito kuhusu hali ya mahusiano na ndoa katika kizazi cha sasa — haswa kizazi cha Gen Z. Ni kweli kwamba kwa wengi wao, ndoa haionekani tena kama hitaji la lazima, bali kama chaguo la mwisho. Ruby alisisitiza kuwa hawezi kuwa sehemu ya maamuzi yenye msingi dhaifu wa kimaadili.

“Tunaishi wakati ambapo maadili yanapotea. Mapenzi yamegeuka bidhaa. Siwezi kuingia kwenye ndoa kwa sababu tu ni wakati au umri wangu. Nataka kuingia nikiwa na uhakika,” alisema Ruby kwa msimamo.

Jambo moja lililo wazi ni kwamba mjadala huu haujaisha. Katika jamii inayokumbwa na mabadiliko ya kitabia, kiuchumi na kiutamaduni, mtazamo wa vijana kuhusu ndoa unaendelea kubadilika. Je, kuchelewa kuoa au kuolewa ni hekima au hofu? Je, ndoa bado ni taasisi takatifu au ni tu mkataba wa kijamii usio na thamani ya kihisia?

Kwa Ruby Kache, jibu ni wazi: si kila mtu anahitaji ndoa haraka, na si kila ndoa ni salama. Muda ni kigezo muhimu cha kuamua mustakabali wa maisha ya wawili.

The Wave hurushwa kila Jumamosi kuanzia saa 4 asubuhi hadi saa 7 mchana kupitia Coco FM, ikiongozwa na Ruby Kache, Hon. Baba Yaga na Dj Capuchino. Kipindi hiki kinaendelea kuvutia maelfu ya wasikilizaji kwa mijadala yake ya ukweli, yenye kuchokoza fikra.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Entertainment

Chris Brown Akanusha Shtaka la Kumshambulia Producer kwa Chupa

Published

on

Msanii nyota wa Marekani, Chris Brown, amekana mashtaka mawili mahakamani yanayohusiana na madai ya shambulio kwa kutumia chupa katika kilabu cha usiku jijini London miaka miwili iliyopita.

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 36 anatuhumiwa kumsababishia mtayarishaji wa muziki majeraha ya mwili katika tukio ambalo waendesha mashtaka wamelieleza kuwa “halikuwa na uchochezi wowote”.

Pia anakabiliwa na shtaka la kumiliki silaha hatari — ambayo ni chupa ya kileo.

Mashtaka haya mawili yaliongezwa mwezi uliopita kwenye shtaka la awali, kubwa zaidi, la kujaribu kumsababishia mtu majeraha mabaya ya mwili (GBH), ambalo tayari Bwana Brown alilishatupilia mbali kwa kujitetea kuwa si kweli.

Chris Brown anatarajiwa kufikishwa mahakamani kwa kesi hiyo mwezi Oktoba mwaka 2026.

Waendesha mashtaka wamesema kuwa mhanga wa tukio hilo, Abraham Diaw, alikuwa amesimama kwenye baa ya kilabu cha usiku kilichopo eneo la Soho mnamo tarehe 19 Februari 2023, wakati Chris Brown alimpiga kwa chupa mara kadhaa.

Mwimbaji huyo alikamatwa mwezi Mei katika hoteli ya nyota tano iliyopo Salford, Greater Manchester, baada ya kurejea Uingereza kwa ajili ya maandalizi ya ziara yake ya muziki barani Ulaya.

Alizuiliwa korokoroni kwa takriban wiki moja kabla ya kuachiliwa kwa dhamana baada ya kukubali kulipa ada ya dhamana ya pauni milioni tano (£5m) kwa mahakama.

Ada ya dhamana ni kiasi cha fedha kinachowekwa kama dhamana ya kifedha kuhakikisha mtuhumiwa atarudi mahakamani kwa kesi yake. Brown anaweza kupoteza fedha hizo endapo atakiuka masharti ya dhamana, ambayo yaliendelezwa katika kikao cha mahakama siku ya Ijumaa.

Kwa mujibu wa masharti hayo, Chris Brown anatakiwa kuishi katika anwani iliyopo Uingereza akisubiri kesi hiyo, na aliamriwa kukabidhi pasipoti yake kwa polisi.

Hata hivyo, ameruhusiwa kuendelea na ratiba ya ziara yake ya kimataifa ya Breezy Bowl XX kwa masharti kwamba atakabidhi pasipoti kila anapomaliza safari, na kuirudishiwa anapohitaji kusafiri kwa ajili ya maonesho.

Katika wiki za hivi karibuni, Brown amekuwa akitumbuiza kwenye viwanja na kumbi mbalimbali za burudani kote Uingereza na Ulaya, na kumaliza burudani mjini Paris mwishoni mwa wiki iliyopita. Sehemu ya ziara hiyo inayofanyika Marekani Kaskazini inatarajiwa kuanza baadaye mwezi huu na kufikia tamati tarehe 18 Oktoba.

Kikao kingine cha mahakama kimepangwa kufanyika tarehe 24 Oktoba.

Chris Brown ni miongoni mwa wanamuziki wakubwa zaidi wa R&B nchini Marekani, akiwa mshindi wa tuzo mbili za Grammy na nyimbo 19 zilizofika katika nafasi 10 za juu kwenye chati za Uingereza, zikiwemo Turn Up The Music, Freaky Friday, With You na Don’t Wake Me Up.

Mshitakiwa mwenza, Omololu Akinlolu, raia wa Marekani mwenye umri wa miaka 39 anayefahamika kisanii kama HoodyBaby, naye pia alikana shtaka la kumsababishia mtu majeraha ya mwili. Awali, alikana pia shtaka la kujaribu kusababisha majeraha mabaya ya mwili.

Chanzo: BBC

Continue Reading

Entertainment

Justin Bierber Arejea na Album Mpya ‘SWAGG’

Published

on

Msanii nyota wa muziki wa kimataifa, Justin Bieber, hatimaye ameachia rasmi albamu yake mpya na ya saba kwa jina “Swag”, ikiwa ni albamu yake ya kwanza tangu mwaka 2021 alipotoa Justice. Albamu hii imetoka leo na tayari imeanza kutikisa majukwaa mbalimbali ya muziki duniani.

Swag imejumuisha mastaa kadhaa akiwemo Gunna, Sexyy Red, Cash Cobain, pamoja na wasanii wengine wa kizazi kipya.

Albamu hiyo ina jumla ya nyimbo 20 na tayari baadhi ya vibao kama “Go Baby”, “Soulful” na Butterflies “zimeanza kupokelewa vizuri kwenye mitandao ya Spotify, Apple Music na YouTube.

Hii ni mara ya kwanza kwa Bieber kuachia albamu tangu alipopata matatizo ya kiafya mwaka 2022 yaliyosababisha asitishe ziara yake ya kimataifa ya Justice World Tour ambayo ilikuwa iendelee hadi mwaka 2023.

Ziara hiyo ilisitishwa mnamo Septemba 2022 baada ya Bieber kupatwa na maradhi ya Ramsay Hunt Syndrome, ugonjwa uliomsababishia kupooza upande mmoja wa uso.

Kwa kipindi cha miaka minne bila kazi mpya, mashabiki wa Justin Bieber duniani wamekuwa wakimsubiria kwa hamu ujio wa kazi mpya kutoka kwake. Kupitia Swag, msanii huyo ameonyesha kurejea kwa nguvu na ubunifu wa hali ya juu, huku akiwa katika hali nzuri kiafya na kisaikolojia.

Taarifa na Francos Mzungu

Continue Reading

Trending