Connect with us

Sports

Nataka Stars Kwenye Fainali Ya Chan Asema Mvurya

Published

on

Waziri wa Michezo Salim Mvurya amesema kwamba lengo lake ni kuona timu ya Soka Harambee Stars katika fainali ya kombe la CHAN linalongoa nanga mwezi ujao hapa nchini.

Akizungumza na wanahabari Mvurya amesema kwamba miondo misingi iko tayari na wanaipa timu ya soka kila kitu kufanya vyema katika mashindano hayo yanayoandaliwa kwa mara ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki Kenya,Uganda na Tanzania.

“Kwa sasa naweza nikathibitishia Wakenya tuko vizuri kwa kombe la CHAN,kuna wakati timu zetu zimkeua zikitatizika mpaka kucheza mechi za kufuzu nje ya nchi kwani hatukua na uwanja wa kutumia ila sasa ni furaha kuwa na viwanja vya viwango kama Kasarani na Nyayo.”

Waziri huyo ameongezea kwamba kwa sasa Stars ina kocha mwenye tajriba na serikali kupitia kwa Wizara yake itaipa sapoti kocha huyo kuleta matokeo chanya.

Kwa mujibu wa Mvurya itakua vyema zaidi Stars wakifika Fainali ambayo inachezwa ugani Kasarani Agosti 30.

“Lengo letu ni kuona Stars kwenye Fainali maanake itakua bora zaidi fainali inaypigwa Kasarani,mashabiki wajitokezee tusapoti vijana wa nyumbani.”

Stars wanafungua kampeini yao dhidi ya DR.Congo Agosti 3 ugani Kasarani.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Makocha Saba pekee Wameshinda Taji La CHAN

Published

on

By

CHAN COUNT DOWN 16 Days to Go

Huku muda ukizidi kuyoyoma kwa kipute Cha CHAN nchini ebu tumulike wakufunzi na Mataifa ambayo yameshinda Kombe hili Tangu kuasisiwa mwaka 2009
Wa Kwanza ni Coach Santos Muntubile na Taifa la DR Congo marufu The Leopards mwaka 2009
Wa Pili ni Kocha Sami Trabelsi na The Carthage ya Tunisia mwaka 2011
Wa Tatu ni Kocha Jalal Damja na Taifa la Libya mwaka 2014
WA nne ni Kocha Florent Ibengé na Taifa la DR Congo mwaka 2016
Wa Tano ni Kocha Jamal Sellami na The Atlas Lions ya Morocco mwaka wa 2018
Wa sita ni Kocha Houcine Ammouta na Morocco mwaka 2021(kombe ambalo lilikua liandaliwe 2020)
Kocha wa Saba ni Pape Thiaw na Senegal mwaka 2022
Continue Reading

Sports

Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Published

on

By

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.

Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.

Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.

Continue Reading

Trending