Sports
Nataka Stars Kwenye Fainali Ya Chan Asema Mvurya

Waziri wa Michezo Salim Mvurya amesema kwamba lengo lake ni kuona timu ya Soka Harambee Stars katika fainali ya kombe la CHAN linalongoa nanga mwezi ujao hapa nchini.
Akizungumza na wanahabari Mvurya amesema kwamba miondo misingi iko tayari na wanaipa timu ya soka kila kitu kufanya vyema katika mashindano hayo yanayoandaliwa kwa mara ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki Kenya,Uganda na Tanzania.
“Kwa sasa naweza nikathibitishia Wakenya tuko vizuri kwa kombe la CHAN,kuna wakati timu zetu zimkeua zikitatizika mpaka kucheza mechi za kufuzu nje ya nchi kwani hatukua na uwanja wa kutumia ila sasa ni furaha kuwa na viwanja vya viwango kama Kasarani na Nyayo.”
Waziri huyo ameongezea kwamba kwa sasa Stars ina kocha mwenye tajriba na serikali kupitia kwa Wizara yake itaipa sapoti kocha huyo kuleta matokeo chanya.
Kwa mujibu wa Mvurya itakua vyema zaidi Stars wakifika Fainali ambayo inachezwa ugani Kasarani Agosti 30.
“Lengo letu ni kuona Stars kwenye Fainali maanake itakua bora zaidi fainali inaypigwa Kasarani,mashabiki wajitokezee tusapoti vijana wa nyumbani.”
Stars wanafungua kampeini yao dhidi ya DR.Congo Agosti 3 ugani Kasarani.
Sports
Makocha Saba pekee Wameshinda Taji La CHAN

CHAN COUNT DOWN 16 Days to Go
Sports
Matumaini Ya United Kupata Mbeumo Yanazidi Kudidimia

Matumaini ya kilabu ya manchester united kupata huduma za kiungo mshambulizi wa kilabu ya Brenford Bryan Mbeumo yanaonekana kufifia kila kuchao.
Haya yanajiri baada ya mazungumzo hayo kukwama kwa sasa baada ya kilabu hiyo ya London kuongeza ada ya malipo ya mchezaji huyo hadi pauni milioni 70.
Kilabu ya Manchester United haiko tayari kulipa zaidi ya pauni milioni 65 kwa mvamizi huyo raia wa Cameroon.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 alifunga magoli 20 ligi ya epl msimu jana.