Connect with us

Sports

Napoli yatangaza kumsajili Rasmus Hojlund kwa mkopo kutoka Manchester United

Published

on

Kilabu ya Napoli hapo jana imetangaza kumsajili mshambuliaji Rasmus Hojlund kwa mkopo kutoka kilabu ya Manchester United ikiwa na wajibu wa kumnunua kwa mkataba wa kudumu, hatua inayomaliza kipindi chake kigumu kwenye klabu ya Old Trafford.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uingereza, Napoli italipa pauni milioni 38 (sawa na dola milioni 51.5) kwa mkataba wa kudumu wa Hojlund msimu ujao.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 raia wa Denmark alisajiliwa na United akitokea Atalanta miaka miwili iliyopita, lakini alihangaika kuthibitisha thamani ya ada yake ya pauni milioni 64 kwenye kikosi kilichokuwa kinakosa ufanisi. Alifunga mabao 26 katika mechi 95 za mashindano yote akiwa na miamba hiyo ya Ligi Kuu ya England, lakini aliachwa nje na kocha Ruben Amorim kabla ya kuanza kwa msimu huu.

Hojlund alipata wakati mgumu katika ligi ya Uingereza msimu uliopita, akifunga mabao manne pekee katika mechi 32, japokuwa alifunga mara sita katika safari ya United kufika fainali ya Europa League.

Napoli walihitaji mshambuliaji mpya baada ya Romelu Lukaku kujeruhiwa paja wakati wa maandalizi ya msimu, huku vyombo vya habari vya Italia vikidai anaweza kuwa nje hadi mwaka 2026.

Hojlund aliwahi kucheza Italia na Atalanta, akifunga mabao 10 katika mechi 34.

Kikosi cha Antonio Conte, Napoli, kilitwaa Scudetto kwa tofauti ya alama moja mbele ya Inter Milan msimu uliopita.

Napoli wameanza vyema kampeni ya kutetea ubingwa, wakishinda mechi zao mbili za mwanzo huku usajili wao mpya wa kiangazi Kevin De Bruyne akionyesha kiwango cha kuvutia.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Sports

Matumizi ya Rekodi ya Pauni Bilioni 3 Katika Usajili wa Majira ya Kiangazi Yaimarisha Ligi Kuu England Kama “Ligi Zaidi Duniani”

Published

on

By

Matumizi ya rekodi ya pauni bilioni 3 ($4 bilioni) katika dirisha la usajili la majira ya kiangazi yamezidi kuimarisha hadhi ya Ligi Kuu ya England kama “ligi yenye ushindani zaidi katika soka la dunia”, kulingana na wataalamu wa kifedha wa Deloitte.

Dirisha hilo lilifungwa kwa mtindo wa kipekee Jumatatu usiku baada ya Liverpool kutangaza usajili wa rekodi ya Uingereza wa pauni milioni 125 kwa mshambuliaji wa Newcastle, Alexander Isak, kufuatia siku iliyojaa uhamisho mkubwa.

Kwa mujibu wa Deloitte, matumizi hayo ya jumla ya zaidi ya pauni bilioni 3 ni ya juu kwa karibu pauni milioni 650 kuliko rekodi ya awali ya pauni bilioni 2.4 iliyowekwa mwaka 2023. Hii ni mara ya tatu mfululizo majira ya kiangazi ambapo matumizi yamezidi pauni bilioni 2, na mara ya kwanza kufikia pauni bilioni 3.

Matumizi hayo yamepita yale ya jumla katika ligi tano kubwa za Ulaya (La Liga, Bundesliga, Serie A na Ligue 1), yakichangia asilimia 51 ya matumizi yote kati ya makundi hayo.

Tim Bridge, mshirika kiongozi katika Deloitte Sports Business Group, alisema:
“Rekodi hii ya tatu ya matumizi ya majira ya kiangazi ya Ligi Kuu England katika kipindi cha miaka minne ni ishara tosha kwamba, licha ya matumizi kuwa madogo barani Ulaya kwa jumla, klabu hazina mpango wa kupunguza uwekezaji wao katika bidhaa ya uwanjani.

“Kwa idadi kubwa zaidi ya timu za Kiingereza kushiriki katika mashindano ya Ulaya kuliko ligi nyingine yoyote barani humo, klabu za Ligi Kuu zinalenga kuvutia vipaji bora na kuimarisha zaidi ligi hii kama ligi inayoshindana zaidi duniani.”

Continue Reading

Sports

Rasmi:Mshambulizi wa Uhispania Marco Asensio ajiunga na Fenerbahce

Published

on

By

Kiungo mshambuliaji wa Paris Saint-Germain (PSG), Marco Asensio, amejiunga na klabu ya Uturuki ya Fenerbahce siku ya mwisho ya dirisha la usajili, vilabu vyote viwili vilithibitisha Jumatatu.

“Klabu yetu imefikia makubaliano na Paris Saint-Germain kwa ajili ya usajili wa moja kwa moja wa kiungo wa Kihispania Marco Asensio,” Fenerbahce ilitangaza kwenye mitandao ya kijamii bila kufichua kiasi kilicholipwa.

“Asaini mkataba wa miaka 3 na nyongeza wa mwaka mmoja, akijitolea kwa rangi zetu za manjano na buluu nyeusi.”

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alijiunga na PSG akitokea Real Madrid mwaka 2023, baada ya kipindi chenye mataji mengi katika uwanja wa Bernabeu ambapo alishinda mataji matatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na mataji matatu ya La Liga.

Asensio alitumia nusu ya pili ya msimu uliopita kwa mkopo katika klabu ya Ligi Kuu ya England Aston Villa, akifunga mabao 8 katika mechi 21 za mashindano yote.

Kimataifa, Asensio ana caps 38 na timu ya taifa la Uhispania, akifunga mabao mawili, huku akiitwa mara ya mwisho mwaka 2023.

Anawasili Fenerbahce baada ya klabu hiyo ya Istanbul kuachana na kocha wa Kireno Jose Mourinho, kufuatia kushindwa kufuzu Ligi ya Mabingwa mwishoni mwa Agosti.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Uturuki, Fenerbahce pia wanatarajiwa kutangaza rasmi usajili wa kipa wa Kibrazili Ederson kutoka Manchester City katika saa chache zijazo.

Continue Reading

Trending