Connect with us

National News

Mweni: Gavana Mung’aro Anafaa Kuwa Makini na Baadhi ya Viongozi

Published

on

Mwakilishi wadi ya Sokoke kaunti ya Kilifi Thaura Mweni ameibua madai kwamba kuna vijana ambao walilipwa kima cha shilingi elfu 50 ili kuzua vurugu katika mkutano uliofanyika eneo la Matano mane wakati wa hafla ya mashindano ya usomaji wa Quran mwishoni mwa juma.

Akizungumza na CocoFm, Mweni amesema vijana hao walilipwa ili kuzua vurugu dhidi yake kwa kile kinachoonekana kuwa tofauti za kisiasa baina yake na baadhi ya viongozi wanaoaminika kuwa wandani wa Gavana wa kaunti ya Kilifi Gideon Mung’aro.

Mweni amesema kwamba haina haja ya malumbano ya kisiasa bali ni vyema iwapo kutakuwa na ushirikiano baina ya viongozi wa kaunti ya Kilifi kwa manufaa ya wakaazi.

Wakati huo huo amepuuzilia mbali matamshi ya kiongozi wa wengi katika bunge la kaunti ya Kilifi Ibrahim Matumbo, akisisitiza haja ya Gavana Mung’aro kuwa makini na viongozi anaoshirikiana nao.

Continue Reading
Click to comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

National News

Kesi ya Lissu kusikilizwa katika Mahakama ya Masjala Ndogo

Published

on

By

Kiongozi wa upinzini nchini Tanzania Tundu Lissu, anapandishwa kizimbani katika Mahakama Kuu Masjala Ndogo mjini Dar es Salaam, kwa ajili ya kesi ya uhaini inayomkabili kwa ajili ya usikilizwaji wa awali (preliminary hearing – PH).

Kesi ya Lissu ambaye pia ni kiongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ilipangwa kusikilizwa siku Jumatatu Agosti 8, 2025 katika Mahakama hiyo na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Iringa, Dunstan Ndunguru lakini ilihairishwa

Lissu, alikamatwa mwezi Aprili na kushtakiwa kwa uhaini, shtaka ambalo iwapo akikutwa na hatia hukumu yake ni kifo, kutokana na kudaiwa kutoa wito kwa wafuasi wake kuzuia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba mwaka huu.

Kesi ya Lissu imekuwa ikifuatiliwa na mataifa ya kigeni zikiwemo nchi za Ulaya.

Taarifa Ya Elizabeth Mwende

Continue Reading

National News

Maafisa 8 wa polisi wajeruhiwa Garissa

Published

on

By

Takriban maafisa wanane wa polisi wamejeruhiwa kwenye shambulizi la kigaidi ambapo gari walilokuwa wakisafiria kukanyaga kilipuzi katika barabara ya Banabs-Yumbis kaunti ya Garissa.

Duru kutoka idara ya polisi zilisema kundi la maafisa hao walikuwa wakisafiri kutumia gari la kijeshi lenye uwezo wa kuhimizi mabomu- Mine Resistant Ambush Protected (MRAP) wakati wa tukio hilo.

Hii ni baada ya kikosi cha maafisa wa kuweka usalama mipakani kukabiliana kwa risasi na washukiwa wa ugaidi wanaoaminika kuwa wanamgambo wa kundi la alshabab.

Magaidi hao wanaaminika waliweka bomu la kutegwa ardhini.

Taarifa hiyo ilisema gari la polisi aina ya Land Cruiser lililokuwa na maafisa zaidi limefika eneo la tukio kuwaokoa maafisa wenzao ambao walikuwa wamekwama ndani ya gari hilo la MRAP.

Maafisa hao wamepata majeraha mabaya na kupelekwa katika hospitali iliyokaribu kwa matibabu ya dharura ambapo baadaye watafasirishwa kwa ndege hadi jijini Nairobi.

Polisi eneo hilo wamesema magaidi wamefanikiwa kutoroka eneo la tukio japo wakiibua hofu kuwa huenda wako karibu na eneo hilo linalokabiliwa na tishio la usalama.

Mpaka wa Kenya na Somalia unasalia kuwa hatari na imekuwa rahisi kwa magaidi kupenya nchini.

Taarifa ya Joseph Jira

Continue Reading

Trending